Nimeibiwa pesa kwenye akaunti yangu ya NBC

Nimeibiwa pesa kwenye akaunti yangu ya NBC

Kwani siku uliyoshtuka kuwa hela imepungua ulijuaje? na hukupata notification kuwa hela imetolewa, tupe mazingira ya tukio yalivyokuwa ili tusiwe na maswali zaidi.
Nilikuwa naangalia salio langu la bank kwa njia ya sim
 
Bors wewe umepewa siku hizo. Mimi CRDB walishanifanyia huo umafia wkt nilikuwa na ukata mbaya sana. Winiibia kama miliobi mbili hivi, na rekodi zao zilionyesha kwamba ni kadi yangu ndiyo ilitumika wakt wanasema hivyo transaction ya kwanza ilirekodiwa mm nikiwa angani kwenda SA, na nilipokuwa SA nilifanya Visa payment moja na withdrawal moja wao wakarekodi withdrawal s 4. Ku challenge ile rekodi yao wakasema hiyo ni Visa siyo wao na hii nyingine ni mimi so wao hawawajibiki. Wkt nafuatilia nilikutana na jamaa naye walimpiga 8m kwa njia hiyo hiyo. Toka siku hiyo CRDB nawasikia tu aisee! Pole sana

CRDB ndo wezi wakubwa hata serikali inafahamu ingekuwa benki ya mtu binafsi ingeshafungiwa. Malalamiko kama hayo nia wengi mno .rafiki walishampiga kama m.5. mpaka ameibrock akaunti yake
 
Itakuwa ni hizi simu zao za siku hizi. Zina raha yake na hii ni moja ya karaha zake.

Jamani natoka nje ya mada kidogo! Hizo ''simu zao siku hizi'' zina nini? Kwa sababu ni mara nyingi nimeona hapa JF watu wakikosea kuandika wanadai ni sababu ya ''simu''! Ni simu za Tanzania tu ndio zina mtindo wa ''kukosea kuandika''? Mbona nchi nyingine zilioni hilo tatizo? Au mnazinguliwa na ''text prediction'' wanazoweka kwenye simu ili zirahisishe uandikaji? Mbona ni rahisi kuzi-disable? BTW Tanzania kila kosa ''linasababishwa'' na kitu kingine chochote lakini si mwadadamu :smile-big:! Nilikutana na kisanga kimoja cha namba kukosewa kwenye karatasi nilipouliza nikajibiwa ''ni computer ilikosea'':wave:
 
Hiyo benki kweli ni majanga matupu, kuna jamaa yangu mmoja naye ilimtokea hela zake nyingi tu kupotea walimsumbua, ilibidi atoe taarifa BOT, BOT wakampa barua aipeleke NBC ndo baadaye wakamrudishia hela yake. Inabidi ukomae ukilegea kidogo tu ndo umeliwa hivyo.
 
Hiyo benki kweli ni majanga matupu, kuna jamaa yangu mmoja naye ilimtokea hela zake nyingi tu kupotea walimsumbua, ilibidi atoe taarifa BOT, BOT wakampa barua aipeleke NBC ndo baadaye wakamrudishia hela yake. Inabidi ukomae ukilegea kidogo tu ndo umeliwa hivyo.
Wasiponirudishia pesa yangu,tutafikishana mbali
 
Acheni kukurupuka kutoa majibu ya utumbo...mfanyakazi ataibaje ktk akaunti ya mteja kirahisi hivyo...
Ili suala lilishawahi kumtoa mwalim wangu wa chuo kakuta 6m hamna na inasemekana ni wizi wa kimtandao ambao unafanywa na watu wa mtandaoni wa kule South kwani wameweza kuingia katika mtandao wa Nbc so wakikuta akaunti ina fedha tu wanahamisha fasta kwani kwa hapa Tz benki ambayo inachezewa sn na hao jamaa ni iyo so vuta subira utarudishiwa tuu lakini si wafanyakazi km mnavyokurupuka kusema utumbo...
 
Hizi benki vimeo. Mimi nilifunga mapema sana akaunti yangu huko. Ila nmb nako matatizo. Wafanyakazi wanaiba hela kwenye akaunti za watu pia. Tamaa ya kununua magari, na kuwahonga mademu wao ndio inapelekea haya yote. Short cut. Nashukuru nmb wapo humu jf, good. Mabenki mengine na maofisi mengine nao waingie humu wawe wanajibu hoja. Nmb hongera

Hivi mfanyakazi anaweza vp kuchukua fedha ktk akaunti ya mteja...acheni kutoa shutuma zisizo na kichwa wala miguu tena unasema katiba eti kununua gari na kuhonga inaelekea akili yako inaumia sn na hao wafanyakazi wanavyomiliki hivyo vifaa...iyo tunaita stress zinakupelekea utoe shutuma tuu hovyo...
Hakuna mfanyakazi yoyote anayeweza kuingia katika akaunti ya mteja kutoa fedha hata siku moja labda awe amefanya kosa kutoa kwako kuweka kwa mtu mwingine tena mda wa masaa flani inajulikana so usitoe shutuma hovyo kwa wafanyakazi ukiwaona na mikoko na watoto wakali ukadhani wanakuibia fedha yqko ni stahiki zao zile mazee wanatumia...Over!!!
 
Acheni kukurupuka kutoa majibu ya utumbo...mfanyakazi ataibaje ktk akaunti ya mteja kirahisi hivyo...
Ili suala lilishawahi kumtoa mwalim wangu wa chuo kakuta 6m hamna na inasemekana ni wizi wa kimtandao ambao unafanywa na watu wa mtandaoni wa kule South kwani wameweza kuingia katika mtandao wa Nbc so wakikuta akaunti ina fedha tu wanahamisha fasta kwani kwa hapa Tz benki ambayo inachezewa sn na hao jamaa ni iyo so vuta subira utarudishiwa tuu lakini si wafanyakazi km mnavyokurupuka kusema utumbo...

Mbona unakuwa mkali au na wewe unafanya kazi hapo nini..!?
 
maukiddo,
Nimefanya kazi benk 2 na uwizi upo sema wewe hujui zinaibwaje.Na mishahara ya staff wa benki ni kawaida sana.wengi mnaringia hadhi za hizo benki!na mikopo ya riba nafuu,17% badala ya 21%.

ivi kuwa na gari na watoto wakali ni indicator ya maisha mazuri?mpaka mtu awe na stress?Sasa sisi tulio kweny level ya kutoa ajira kwa hao watoto wakali unatuweka kundi gani?
 
Hata mimi waliwai niibia (32000000)milioni tatu laki mbili waliniendesha kama mwezi hv nikawaambia nina shida na pesa yangu hawakunielewa kabisa majibu wanayonipa wananiambia subiria tujiridhishe atm kard unayo wewe na ndio iliyotumika kuchukuwa pesa nikamweleza rafiki yangu anafanya kazi TIB akaniambia niende makao makuu nimwome meneja wa kanda nikajitosa kwake ile kunyanyua waya kwa vijana nimeondoka pale akaniambia atalifanyia kazi ndani ya siku mbili itakuwa isharudi vijana wakaanza kunipigia cm na kiniuliza wewe umefikaje kwa mapunda nikawajibu mmeniibia pesa isitoshe mnanizingua wakati naitaji usiku haikufika saa 3 washarudisha mzigo wangu usipokuwa makini wanaweza hata wakakuzulumu mapunda alinipaga kard ya ngojea ntakutumia no zake tuwasiliane kwenye no 0786522229
 
Hivi tunapata nini huko nbc labda cha tofauti sana mbona crdb cjawai kusikia huu wizi
 
Hivi mfanyakazi anaweza vp kuchukua fedha ktk akaunti ya mteja...acheni kutoa shutuma zisizo na kichwa wala miguu tena unasema katiba eti kununua gari na kuhonga inaelekea akili yako inaumia sn na hao wafanyakazi wanavyomiliki hivyo vifaa...iyo tunaita stress zinakupelekea utoe shutuma tuu hovyo...
Hakuna mfanyakazi yoyote anayeweza kuingia katika akaunti ya mteja kutoa fedha hata siku moja labda awe amefanya kosa kutoa kwako kuweka kwa mtu mwingine tena mda wa masaa flani inajulikana so usitoe shutuma hovyo kwa wafanyakazi ukiwaona na mikoko na watoto wakali ukadhani wanakuibia fedha yqko ni stahiki zao zile mazee wanatumia...Over!!!

Inaonyesha wewe ni mmoja wapo wa wafanyakazi Wa bank...maan ulivyoandika yaan sipati picha
 
Akaunti nimeifunga nasikilizia huo uchunguzi wao hadi utakapokamilika.Ubaya wao NBC ukiweka pesa au kutoa pesa hawakupi taarifa kwa njia ya simu kama benki zingine

Hilo nalo NENO ndugu,umeongea point ya maana sana!
 
Mkuu pole sana. Ilishatolewa elimu humu jamvini. Kuibiwa hela kwa njia hii huitwa card skimming. Hakuna benki iko salama. Cha msingi ni kuwa makini tu unapotumia ATM card hasa kwa wale mnaopenda ku-swap kwenye manunuzi yenu. Wezi kwa njia hizi sasa hivi ni wengi mno.
Kama staff anahusika pia ni rahisi kumkamata we vuta subira
Hizo 45 days ni kwa sababu uchunguzi utawahusisha mastercard/visa na ndo utaratibu waliowekeana.
Uchunguzi unakuwa rahisi pale inapotokea hela inatoka na cents ama inatoka kuzidi kiwango cha kawaida cha kutoa pesa kwa ATM kwa siku

USER2013 Usisahau kuwa process ya kutoa hela ATM inaweza kuanzishwa hata ndani ya Benki bila hata ya ATM card! na hii ndiyo hatari zaidi. Ukiona taasisi inajihami kwa udi na uvumba ujue this is the method used.
 
Back
Top Bottom