Mkuu crdb nako sio salama, mimi hapa nina kesi kama hii Toka crdb, wiki mbili zilizopita nikiwa nyumbani ziliingia message mfululizo kuwa kadi yangu imetumika kutoa hela kwenye atm wakati kadi yangu nilikuwa nayo mfukoni na siJawai kumpa mtu! Nilipiga customer care ya crdb akapokea dada mmoja mpuuzi akadai labda mke wangu ndio katoa, wakati naongea nae ikaingia tena msg ya hela kutoka lakini yule dada kichwangumu akaendelea kusisitiza nimempa mtu kadi(pu..bafu zake), mbaya zaidi msg zilionyesha hela iliyotolewa ilikuwa sio figure kamili na ina points(senti) kumueleza akawa anaJichekesha tu, nimefuatilia benki nimeJaza mikaratasi kibao, kila unayemplekea anakuambia mwenzie amekosea aina ya karatasi linalotakiwa kujazwa, niliwawakia Baada ya kubadilisiwa karatasi za kujaza mara tatu, hadi leo hela haiJarudisHwa