Nimeibiwa 245,000/= MPESA VODACOM

Nimeibiwa 245,000/= MPESA VODACOM

Itakua umejiibia kama isemavyo serikali ya hawamu ya 5 kuwa watu wanajiteka sasa na wewe hyo utakua umejiibia!
 
Ndugu wana jamvi.
Jana saa mbili usiku nimeibiwa shilingi laki mbili na elfu arobaini na tano kwenye namba yangu ya vodacom yenye Mpesa. Fedha zimetolewa kwa wakala, na ujumbe nikaletewa kuwa nimepokea fedha taslimu toka kwa wakala huyo.

Ushahidi huu hapa.
6ES62D6M74W Imethibitishwa tarehe 28/5/19 saa 10:17 PM Pokea kiasi cha Tsh240,000.00 kutoka kwa 430185 - MWANAHAMISI RAJABU ISSA kwa ada ya Tsh5,000.00. Salio lako jipya la M-Pesa ni Tsh675.00.

Cha ajabu ni kuwa muda huo, mimi nilikuwa na simu yangu na sikufanya muamala huu.
Mara moja niliwapigia huduma kwa mteja Mpesa Vodacom ambao wamesema nisubiri masaa 72.
Swali kwa wataalam.
1.Ni nini hasa kimefanyika hadi namba yangu ikatoa fedha nipopajua ilihali simu yangu ninayo?
2. Je nitaweza kupata fedha zangu hizi?
3. Je niendelee kutumia namba hii au niachane nayo?


Nawasilisha.
Mimi nimewahi kuibiwa shs. 4,450,000/= kutoka benki ya DTB . Na bado fedha yangu haikurejeshwa, japo mwanzo walinipa matumaini ya kurejeshewa.

Kipindi hicho huduma ya mobile ktk mabenki ilikuwa haijawa kama leo. Wiki mbili zote, jamaa alikuwa anatoa pesa kupitia ATM visa card fake, bila mimi kujua kupitia mabenki mengine.

Mambo haya ni changamoto.
 
Uliza swali sehemu ambayo hujaelewa maana naamini hayo maelezo yamekamilika. Wanalijua ndio maana siku zote tunasisitizwa kutunza namba zetu za siri, watakuwa labda wanalitafutia mwarobaini
Nilitaka jua hill kwamba MTU akiweka namba yako kwenye simu yake akadownload mpesa apple na akawa anajua namba yako ya siri anakupiga?
 
Mimi nimewahi kuibiwa shs. 4,450,000/= kutoka benki ya DTB . Na bado fedha yangu haikurejeshwa, japo mwanzo walinipa matumaini ya kurejeshewa.

Kipindi hicho huduma ya mobile ktk mabenki ilikuwa haijawa kama leo. Wiki mbili zote, jamaa alikuwa anatoa pesa kupitia ATM visa card fake, bila mimi kujua kupitia mabenki mengine.

Mambo haya ni changamoto.
Aiseee!!
 
Huwa namba zinaingiliana.
kama uliwahi kabla wakala hajampa huyo mtu pesa...utazipata.ila kama ulichelewa...kuna mawili.
1 wakala kulipa
2 kupoteza.


Ni kwa mara ya kwanza kutokea? Endelea na mamba yako ila badili nenosiri.
Mambo ya kupigia huduma kwa wateja ndo yanafanya mtu ashindwe kupata hela yake sometimes.... Njia ni moja tu... kwenda kwenye ofisi zao.....
 
Kuna mtu anaejua namba yako ya siri aliweka line yako kwa simu yake akadownload Mpesa app
Hili nalo linawezekana.... but pia huyo mtu lazima aliijua namba ya siri ya jamaa... nje ya hapo asingeweza....
 
Yeah, anachukua line yako anaweka kwenye simu yake anadownload mpesa app then anaendelea kufanya transactions kwa kutumia app aliyodownload kwa kutumia line yako
Nilitaka jua hill kwamba MTU akiweka namba yako kwenye simu yake akadownload mpesa apple na akawa anajua namba yako ya siri anakupiga?
 
watu watakua wanalizwa sana kwa hii mpesa app, sio salama kama mtu mwingine anaweza kuitumia kutoa pesa kwa namba ya mtu. Waifanyie marekebisho kwa usalama wa fedha za watu
Usalama wa M-pesa ni namba yako ya siri bila hivyo utapigwa mpaka ukome
 
Mimi nimewahi kuibiwa shs. 4,450,000/= kutoka benki ya DTB . Na bado fedha yangu haikurejeshwa, japo mwanzo walinipa matumaini ya kurejeshewa.

Kipindi hicho huduma ya mobile ktk mabenki ilikuwa haijawa kama leo. Wiki mbili zote, jamaa alikuwa anatoa pesa kupitia ATM visa card fake, bila mimi kujua kupitia mabenki mengine.

Mambo haya ni changamoto.
Duuh aisee
 
Mfano wangekua wanatuma sms ya conrfimation code kwenye namba yako ambayo ungeiweka ili kuconfirm muamala nafikiri hapa ingeweza kutatua tatizo
Matter ni namba ya siri mkuu.... hii app me naipenda sana sababu nakumbuka kuna kipindi nilikuwa natoa hela kwa wakala hata kama line yangu ipo mbali....

Kama mtu anashindwa kutunza namba yake ya siri there is no way anaweza kusaidika....
 
Mimi nimewahi kuibiwa shs. 4,450,000/= kutoka benki ya DTB . Na bado fedha yangu haikurejeshwa, japo mwanzo walinipa matumaini ya kurejeshewa.

Kipindi hicho huduma ya mobile ktk mabenki ilikuwa haijawa kama leo. Wiki mbili zote, jamaa alikuwa anatoa pesa kupitia ATM visa card fake, bila mimi kujua kupitia mabenki mengine.

Mambo haya ni changamoto.
Mi ilishawahi kunikuta NBC kwa kuibiwa 2.1M hadi kuna uzi niliweka humu. Nilienda hadi BOT, pesa nilirudishiwa ila ilichukua takribani miezi 3.
 
Back
Top Bottom