Nimegundua kwanini wanaJF huitana "Mkuu"

Nimegundua kwanini wanaJF huitana "Mkuu"

Sema ukiongezea (ma) Mkuu uwezi tamani tena hicho cheo wakuu
 
Habarini wakuu!

Kama ilivyo kawaida yetu humu ndani tumezoea sana kuitana WAKUU bila kujali unayemwita ni kweli ni Mkuu au la!
Humu ndani kuna wazee na wajukuu zao, wazazi na watoto wao, watu waliotalakiana, wenye vyeti feki na halali, misukule na watu timamu: Lakini utamaduni wetu ni huu wa kuitana MKUU.

Nimegundua Kwanin tunalitumia sana neno MKUU;
Kwanza, humu ndani wengi tunatumia ID na AVATAR feki hivyo kila mmoja ana HOFU na mwenzake. Kuchati na mtu usiyemfahamu kunahitaji Busara yaweza kuwa unacomment thread ya babu yako, au mama au boss wako kazini Ndiyo maana wengi tunatumia neno MKUU.

Pili nadhani wengi wetu tunatumia MKUU ili tusitukanwe, wengi humu ukiwaquote na kucomment vibaya wanarudisha majibu ambayo yatakuharibia Siku na mood ya kufanya kazi itaisha.

Tatu, wengi wakianzisha Uzi hasa unaohitaji mchango wa mawazo, hutumia sana WAKUU ili kuvuta watu watiririke nondo za maana na kwakuwa tumeshavimbishwa bichwa kwa kuitwa wakuu, wengi tunauvaa uhusika wa UKUU ipasavyo.

Haya WAKUU, Mimi nimegundua hayo, ongeza na lako kama lipo.
Mkuu utafiti wako ni feki hakuna chochote nakuomba urudie na uchukue sampuli kubwa ili uje na majibu sahihi.

Neno mkuu, kaka, mzee yanatumika mara nyingi na jamii yetu watumia kiswahili na hayana maana nyingine zaidi ya kuonesha heshima.

Ni sawa na wabunge kujiita waheshimiwa wakati wengine wayatendayo hayastahili heshima hata kidogo.
 
Ukitaka watu wasikuvamie, bebea hela kwenye gunia chafu chafu.

Hii ndo style anayoitumia CHIKIRA MTABARI, ukiona jina na avatar unapotea zako, ila tunaojua nini kimo ndani tunabaki.
hahahahahahah shemeji hahahahaahahaha nimecheka kwa sauti, mwambie mwambie huyo "Padri" uchwara
 
Sawa mkuu umesomeka ulikuwa hupati mchango wa wana if ndio ukafanya kautafiti kidogo....sawa mkuu
 
Ndio maana Magu haipendi jf maana alitaka aitwe mkuu pekeako
 
Huwa natumia neno Mkuu kwasababu sijui jinsi ya muhusika lakini ningekuwa najua ningetumia vinginevyo pia, dada, kaka etc.

Uzuri humu JF wanawake wanajiita majina ya me na kujifanya me na wanaume wanajiita majina ya ke na kujifanya ke, sisi wengine tunamajina ambayo hayaelezi jinsi zetu dhahiri hiyo sehemu zingine tunajifanya ke, zingine me.

Ni hayo tu Mkuu.
 
hahahahahahah shemeji hahahahaahahaha nimecheka kwa sauti, mwambie mwambie huyo "Padri" uchwara

Mwache ajichanganye tu, huyo ni admirer kimoyomoyo ila anazuga anahate.

Mimi shemeji nakwambia kila siku endelea kuwachanganya na avatar hizo, wamezoea wakiona avatar nzuri wanakimbilia PM
 
Mwache ajichanganye tu, huyo ni admirer kimoyomoyo ila anazuga anahate.

Mimi shemeji nakwambia kila siku endelea kuwachanganya na avatar hizo, wamezoea wakiona avatar nzuri wanakimbilia PM
hahahahahah hizi avatar zangu hata Mondray kila mara anani sihi eti nizitoe hahahahahahaa
 
Back
Top Bottom