Nimefanikiwa kuingia Gamboshi - True Story

Nimefanikiwa kuingia Gamboshi - True Story

President of China

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2018
Posts
31,772
Reaction score
89,799
Gamboshi is real.
Ndungu zangu wanajamvi, wiki iliyopita nilikuwa katika safari zangu za kila siku za tafiti. Moja ya tafiti ambazo nimejikita nazo ni tafiti za kitamaduni na mali kale.
Kwanza nianze kwa kusema hivi uchawi upo, kila nchi inautumia kwa namna yake.
Nilitembelea katika kijiji kimoja huko mkoani shinyanga nikakutana na mzee anayejulikana kwa jina la Madeleke. Lengo langu ni kutaka kujua na kujifunza namna ya jamii za kale walivyoishi.

Tuliongea mambo mengi na alinifundisha vitu kadha wa kadha ikiwamo namna ya kufanya uchawi. Nikamwambi mzee nasikia habari za kuhusu gamboshi hivi kweli suala lipo.
Mzee aliniambia suala hilo lipo na yeye ni mmoja wa members wa gamboshi. Akaniahidi atanipeleka.
Tulifanya maandalizi kwa muda wa siku 6 kisha tukafunga safari kuelekea mkoani Simiyu.
Kusema kweli safari yetu ilikuwa ya ajabu sana, maana tulisafiri usiku wa manane. Usafiri uliotumika ni wa wanyama mithili ya fisi ila wao wapo juu kidogo.
Mida ya kama saa 8 za usiku niliona taa zikiwaka mbele yetu. Ni taa za kila namna.
Ndugu yangu, tuliingia kwenye lango lililo chini ya mlima na kukutana na watu wa kila aina. Walikuwepo wazungu, warabu, wachina na sisi waafrika.
Mzee kaniambia hapa ndio gamboshi.
Kulikuwa na chakula, vinywaji. Watu walikuwa wakisherehekea.
Wanawake wazuri wazuri walikuwepo. Na kuna wengine wasanii na wanasiasa wakubwa niliwaona. Niliwaona wachungaji kadhaa wanaohubiri wakijumuika.

Kweli uchawi upo na Gamboshi ipo.
Ninatarajia kwenda huko tena mwezi wa tano. Mzee ameniahidi ataenda kunitambulisha na mimi niwe member.
Ninayo mengi sana niliyojifunza. Watu wa gamboshi ni wakarimu na wanaupendo.
Kama kuna mtu yupo tayari aweze kuni PM tupange safari twende pamoja.

Asanteni.
 
Mi nipo huku kitambo...mbona sikukuona?
Kusema kweli ilikuwa ni mara ya kwanza kufika huko. Watu walikuwa ni wengi mno. Vilevile nilikuwa ninaogopa mno.
Labda mwezi wa tano kwakuwa mzee ameahidi kwenda kunitambulisha huenda tukajuana.
 
Nauli ni kutoka ulipo kwenda kwa mzee madeleke mkoani shinyanga. Kutoka hapo kila kitu anafanya yeye. Mimi kwa sasa nipo Dar es salaam, nipo Mbezi Beach karibu na kwa Joseph Kusaga.
Tuwasiliane tu.
Basi sawa.
 
mkuu acha chai bana wewe.....gamboshi ni kijiji kipo katikati ya mkoa wa shinganya na simiyu, ukipita njia ya shinyaga kuja bariadi utakutana na hicho kijiji, ni kijiji kama kijiji vingine acha kutupikia chai sahizi na jua kali lote hili.
 
Back
Top Bottom