Habarini ndugu zangu natumaini ni wazima.....Nina muda mrefu tangu nianze kuota nafanya mapenzi usiku mpaka naandika uzi huu ni kutokana na jinsi jana nilipoota nafanya mapenzi na mwanamama aliekua amevalia nguo nyeusi kwa kweli nilienjoy kabisa kama nafanya mapenzi live.
Ndugu zangu nifanyeje niache kuota hivi ukizingatia mimi ni mwanamke halaf naota nafanya na wanawake wenzangu.
pole kwa matukio yanayokupata. kwenye ulimwengu wa roho hilo ni jambo la kawaida na linamadhara kwenye ulimwengu wa mwili na hata kiroho pia. Mara nyingi majini huja kwa mtu kwa kuitwa au kutumwa au kujileta yenyewe hasa yakiona yatapata faida fulani kwako.
Yakuitwa yankuja kwa faida ya muitaji, mfano mtu anayaita kibiashara au kimapenzi au yafanikishe jambo fulani, pia ya kutumwa huja kufanikisha malengo ya mtumaji mfano kuiba nyota, kumfanya mtu ateseke, kuvunja ndoa, kuharibu kazi na mengine mengi kwani ulimwengu una mengi sawa na idadi ya wakaazi wake.
Hawa wanaokuja wenyewe ni wabaya zaidi, kwani huja kwa mtu kupata faida ambazo mtu huyo anazo kulingana na talent ambazo Mungu amemuumba nazo. mfano mtu ananyota kali kibiashara, ni mzuri wa sura/roho na anavutia sana au anaufahamu wa kipekee kwenye jambo fulani na wanajua akibaki nalo linaweza kuleta madhara baadaye kwenye ulimwengu wa roho, hasi hutuma hayo majini ili yaharibu na kumlinda mtu huyo asije fanikiwa.
Na mara nyingi humfanya mlengwa duni kimaisha, kimawazo na kuleta upweke. huongeza hasira, hufukuza marafiki muhimu na watu ambao wangekuwa msaada, pia kufeli masoma na maisha ni moja ya njia ambazo hutumika kudunisha maisha ya mtu, wakati mwingine mambo yaliyokuwa yanakwenda huanza kurudi nyuma. Pia huzuia mahusiano ya kimapenzi na wanadamu wengine.
Namna ya kuondokana nao wafukuze kwa damu ya YESU, kama huwezi nenda kwa mtu mwenye ufahamu wa mambo ya MUNGU atakusaidia. Pia achakufutilia mambo yenye hisia za kingono, kwani hata yakiondoka kwani yako ndani yako yanaweza kurudi tena. Mungu anatulinda muda wote, lakini tukiingia kwenye dhambi hutuacha na ndiyo hayo madude hupata nafasi.