Nimeamua kwenda Arusha kutafuta maisha

Nimeamua kwenda Arusha kutafuta maisha

Nasakadoo

JF-Expert Member
Joined
Sep 18, 2014
Posts
343
Reaction score
169
Baada ya kukosa kazi ya kuniingizia kipato kwa hapa Dsm… na baada ya kupewa ahadi ya kusaidiwa namna ya kujikwamua kimaisha kuwa isiyotimilika…
Nimeamua kulikimbia Jiji la Dsm na kwenda Arusha.
Huko simjui mtu,sina ndugu wala mjomba. Naenda kupambana na hali yake. Labda kuishi Dar mda mrefu naona hakuna fursa kwangu tena! Lakini pia kuna labda kazi ambazo kwa hapa Dar zinaonekana siyo ila kwa Arusha na nje ya Dar zinaweza kuonekana ndiyo za maana! Vyote hivyo naviona akilini mwangu…
Kama nimepotea,potelea mbali! Ila namwomba Mungu anitangulie katika hili. Maisha ni magumu saana!
Wakazi wa Arusha,na viunga vyake,tengeru,moshono,kia,na Mererani nawaomba mnipokee aisee!! Nimekuja arusha kutafuta maisha. Ni hayo tu!
 
If YoU dOnT makE iT iN dAresSalAaM YouWoNt makE it In RcHugAaa. NendaMkoA mWinGine ila Sio cHuGaaa AriFuuuu
 
Kuna kampuni ya utalii arusha inatafuta secretary, interview jumamosi , kama upo tayari tuwasiliane fasta
 
Mimi Nipo arusha sijasoma natafuta kazi yeyote, naishi maisha magumu sana, yeyote mwenye aidea anisaidie, nimeishia kidato cha pili, hesabu za baa hazinisumbui
 
Kazi arusha Wachaga wanapeana sana kazi
 
Kuna kampuni ya utalii arusha inatafuta secretary, interview jumamosi , kama upo tayari tuwasiliane fasta

Aisee… tatizo mara nyingi huwa wanahitaji Ma secretary wanawake/wasichana.
mi dume! Au kuna option hiyo…
 
Karibu chalii yangu........mi nipo hapa. Mererani karibu tuje kufukuzia moto........

Nitakutafutaje…
Ni Inbox cont basi… safari moja huanzisha nyingine
 
All the Best joh, mi niko dsm but chuga is my born city keep hustling mkuu, everyting gona be mwake
 
Duh...kwa Arusha sijui utaanzia wapi mkuu....ule mji sio wa kukimbilia...hakuna mzunguko wa hela kabisa... hakikisha usitumie akiba yote..bakiza nauli ya kuondoka.....ingekua mimi ningekushauri nenda mwanza,mbeya au mtwara..uta make pande zile.

Arusha Mmmmhhh.
 
Duh...kwa Arusha sijui utaanzia wapi mkuu....ule mji sio wa kukimbilia...hakuna mzunguko wa hela kabisa... hakikisha usitumie akiba yote..bakiza nauli ya kuondoka.....ingekua mimi ningekushauri nenda mwanza,mbeya au mtwara..uta make pande zile.

Arusha Mmmmhhh.

Arusha hakuna mzunguko wa fedha???????
 
Halafu naenda sina hata wa kumfikia! Yaani maisha haya… unaweza kuwa chizi!
Vyovyote vile nitalala hata guest siku mbili… halafu nitakuwa nimejichanganya na wadau… naenda Mererani jamani'!
Duuh!! So sad…
 
Mimi Nipo arusha sijasoma natafuta kazi yeyote, naishi maisha magumu sana, yeyote mwenye aidea anisaidie, nimeishia kidato cha pili, hesabu za baa hazinisumbui

Kuna kampuni ya utalii arusha inatafuta secretary, interview jumamosi , kama upo tayari tuwasiliane fasta

Utakuwa na wewe dume nini wamudu hesabu za bar na kazi hapo kwa ofisi ya utalii 😳
 
If YoU dOnT makE iT iN dAresSalAaM YouWoNt makE it In RcHugAaa. NendaMkoA mWinGine ila Sio cHuGaaa AriFuuuu

[P. Diddy Talkin]
New york,if you can make it here, you can make it anywhere
We still here!!! And we buildin four more new towers!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom