Tamalisa
JF-Expert Member
- Feb 3, 2015
- 2,542
- 907
- Thread starter
- #41
Kwa unyenyekevu mkubwa (huku nimepiga magoti) naomba kusema neno. Hakuna ulevi mbaya kama wa kiimani, sii leo wala jana bali tangu enzi na enzi. Na wengi wenye kutoka mbele ya haraiki /hadhira na kujisifu juu yao na kujikweza kumfuata yeye alie juu watu hawa huitumia halihiyo kama kichaka cha maovu. Yesu wa nazareth alipokuja duniani watu wa kwanza kukosana nao walikuwa ni "mafarisayo & masadukayo". Hawa aliwafananisha na makaburi yenye kung'aa nje huku ndani yakificha "uozo".
Hili ni kweli ndugu yangu na ndio maana leo hii tunasikia habari nyingi mbaya juu ya hao waliookoka, lakini hupaswi kumuhukumu mtu kwa kugeneralize, ukimshuhudia mseme, ila kama hujamshuhudia tulia tu mwache aendelee na wokovu au imani yake, hii ndio busara kuu. Maana kuna watu waliwakejeli watumishi wa Mungu badae wairudi kupiga magoti wenyewe, cha msingi ni kuzidi kuombeana tu, sisi tunawaombea vijana wote Tz.