Nimeamua kurudi CCM

Nimeamua kurudi CCM

Wahenga wanasema chanda chema huvikwa pete,na hili limethibika kuwa Ccm ni chanda chema kwa watanzania.

Niliamua kujiunga na Nccr Mageuzi nikiwa na imani kuwa ni chama ambacho kitakuwa mbadala wa kuiondoa Ccm na kukamata dola.

Ila kuna jambo moja limenifanya nirudi Ccm na hili ni kupambana na ufisadi,kisha pesa zilizokuwa zinaporwa na mafisadi kutumika kuwaletea maendeleo watanzania. Maana sekta ya afya,elimu,miundo mbinu na kila sekta imeimarishwa.

Ila jambo moja muhimu ni kuokoa zaidi ya bil 719 ambazo Iptl na Agreco walikuwa wanalipwa kila mwaka bila sababu ya msingi. Maaana sasa hakuna kampuni kama Iptl au Agreco ambayo inalipwa hizi fedha kifisadi na hakuna mgao wa umeme wala hakuna deal za kupiga pesa kama Richmond n.k.

Kwa ufupi zimebaki siku tano na kwenye karatasi ya kupigia kura Ccm ni namba moja,kwa hiyo naweka tick kwa Ccm na huku chini sipotezi muda kuangalia tena.
Msikilize Tundu Lissu akimsifu Magufuli.
 
Ccm ni chama cha Watanzania wote, kule Chadema ni mali ya mtu
Yeye katoka NCCR kaenda CCM!Sasa CDM inakuwashawasha nini?

NB:Mleta mada na wengine mnatambulika humu misimamo yenu kikada!Wala msijisumbue kufanya propaganda!Mnaeleweka
 
Nimekuambia CCM huwa inajitathimini ikifanya makosa. Na hilo ndio jibu sahihi kwako. Ndio maana wanaokoa Bil 719 hii leo.
Shehe ni yule yule ila kanzu tofauti!CCM ndio chanzo cha umasikini nchi hii!Ukisikia propaganda zao sijui wameokoa hiki na kile,wao ndio waliosababisha hayo in the first place so tusitishane saana!
Akili mpya inatakiwa iiingie kuja kufagia kabisa uozo wa CCM na nchi isonge mbele!
 
Hii propaganda ilibuma na zitto junior na kaka yake walipata aibu kubwa sana. Maana PAC walitoa majibu kuwa hakuna pesa iliyopotea.
Hoja haikuwa imeibiwa ila hoja ni kwamba mahesabu yale hayakupita mfuko mkuu wa serikali hivyo yanakuwa vulnerable to UFISADI.

So 1.5 T haikua accountable na ilikua na haja ya kuchakataliwa. Na hapo ndio faida ya upinzani, na serikali ikakiri kuna udhaifu wa kiuhasibu so imesaidia kuziba future mianya ya ufisadi.
 
Hoja haikuwa imeibiwa ila hoja ni kwamba mahesabu yale hayakupita mfuko mkuu wa serikali hivyo yanakuwa vulnerable to UFISADI.

So 1.5 T haikua accountable na ilikua na haja ya kuchakataliwa. Na hapo ndio faida ya upinzani, na serikali ikakiri kuna udhaifu wa kiuhasibu so imesaidia kuziba future mianya ya ufisadi.
Kwa hiyo ni ukweli ulipatiwa majibu,hakuna ufisadi wa 1.5 tril,bali maridhiano ya kimahesabu yalichanganya watu.
 
Kama ununuzi wa ndege hakuna ubadhirifu, kwanini wasipeleke mikataba yake bungeni? Alafu kwanini wanamkataza CAG asifanye ukaguzi kwenye michakato ya ununuzi?

Wanaficha nni
Ni kweli kaka? Maana mikataba ya Airbus,Dash 8 na Boeing ipo wazi kabisa.
 
Kwa hiyo ni ukweli ulipatiwa majibu,hakuna ufisadi wa 1.5 tril,bali maridhiano ya kimahesabu yalichanganya watu.
Mkuu ufisadi ni mchakato sio tukio, yaani ukiona pesa haionekani kwa mfuko mkuu ujue kuna dili la kuiba.

Kwahiyo kisheria ni lazima mapato yote yapite mfuko mkuu ili serikali ijue ina shingapi. Sasa ukifanya miamala nje ya mfumo huoni unaiweka kwa risk ya pesa kuibiwa? Huoni kuna sheria zimekiukwa maksudi kabisa ili pesa iibwe?
 
Back
Top Bottom