Meta AI
JF-Expert Member
- Jul 12, 2021
- 1,564
- 4,018
Wanajamii mko fresh eee...
Ebwana haya maisha ni noma sana, mambo yanachanganya na mengine yanachosha moyo.
Baada ya kujitafuta sana kwa miaka mitano kwenye harakati mbalimbali, hatimaye leo nmeamua kubadili mwelekeo wa mambo.
Nilianza na kupanga chumba kimoja, baada ya mwaka nikaona nina uwezo wa kumudu nafasi kubwa zaidi... nikahamia chumba na sebule. Harakati hazikupoa, nikaona nioe.
Huko nikaishia kupigwa za uso na nikamfukuza mke. Maisha yakawa bomba sana kwa kiasi chake. Nikafanikiwa kununua viwanja vitatu, boda 2 na kuongeza msuli wa kazi.
Mwezi wa pili nilikaa nikaitafakari kazi + mazingira ninayoishi nikajiona ni kama mda wote sikuwa kwenye mstari ninaoutaka.
Niliamua kuuza kila kitu, viwanja vyote, boda zote na mzigo wa kazi nilokuwa naifanya hadi kila kitu cha ndani.
Nilikamata milioni 16 huku nikiwa sina hata pa kulala, japo chumba nilibaki nacho. Nilisepa nikaenda mkoa ambao sikuwahi hata kuufikiria, nikasoma upepo nikaona kuna fursa.
Nilinunua mashine 2 za kukamua alizeti pamoja na mashine 1 ya kuparata mkonge then nikaingia sokoni.
Niliajiri vijana 9 nikaanza kukimbizana na fungu la kupata au kukosa.
Kwa sasa maisha yameanza na ukurasa mpya. Hadi sasa nimesev milioni 7 tu kwa miez 2.... japo ka moyo kanadunda kwa maamuzi nilochukua.
Ila fresh... nimejilipua.
Ebwana haya maisha ni noma sana, mambo yanachanganya na mengine yanachosha moyo.
Baada ya kujitafuta sana kwa miaka mitano kwenye harakati mbalimbali, hatimaye leo nmeamua kubadili mwelekeo wa mambo.
Nilianza na kupanga chumba kimoja, baada ya mwaka nikaona nina uwezo wa kumudu nafasi kubwa zaidi... nikahamia chumba na sebule. Harakati hazikupoa, nikaona nioe.
Huko nikaishia kupigwa za uso na nikamfukuza mke. Maisha yakawa bomba sana kwa kiasi chake. Nikafanikiwa kununua viwanja vitatu, boda 2 na kuongeza msuli wa kazi.
Mwezi wa pili nilikaa nikaitafakari kazi + mazingira ninayoishi nikajiona ni kama mda wote sikuwa kwenye mstari ninaoutaka.
Niliamua kuuza kila kitu, viwanja vyote, boda zote na mzigo wa kazi nilokuwa naifanya hadi kila kitu cha ndani.
Nilikamata milioni 16 huku nikiwa sina hata pa kulala, japo chumba nilibaki nacho. Nilisepa nikaenda mkoa ambao sikuwahi hata kuufikiria, nikasoma upepo nikaona kuna fursa.
Nilinunua mashine 2 za kukamua alizeti pamoja na mashine 1 ya kuparata mkonge then nikaingia sokoni.
Niliajiri vijana 9 nikaanza kukimbizana na fungu la kupata au kukosa.
Kwa sasa maisha yameanza na ukurasa mpya. Hadi sasa nimesev milioni 7 tu kwa miez 2.... japo ka moyo kanadunda kwa maamuzi nilochukua.
Ila fresh... nimejilipua.