Msaada tafadhali,tofauti na mada.ambao tayari mmewahi kuagiza vitu kama simu nk online kwenye mitandao kama aliexpress,ebay mnatumia anuani gani kupokelea bidhaa mlizoagiza maana nimejaribu kuagiza anuani niliyotumia ni ya kampuni ninayofanyia kazi sasa nina wasiwasi na watu wa posta maana kuna malalamiko mengi yanayowahusu kwamba vitu vya thamani vinapoteleaga mikononi mwao baada ya kufika kwao.nanao uwezo wa kufungua anuani binafsi ya posta ila hilo tatizo ndio linanitatiza.sasa nilikuwa naomba msaada wa njia nzuri ya kupokelea parcel kama ipo.
NB.nimependa utaratibu wa kampuni ya KIKUU,wao wanatumia sana mawasiliano ya simu na unaletewa mzigo wako mpaka sehemu ulipo hii inasaidia hata kwa ambae hana anuani anaweza kufanya manunuzi.