Mkuu wkt tupo kwny basi tulijadili kuhusu hili, wakubwa wakanishauri nisifanye hivyo, kuna impact kubwa sana.
Vip mkuu nikuchagulie jina, kama vip ukimbatiza mi ntakua baba ubatizo.... kuhusu jina waweza Davion au Delmonte majina mazuri hayo....
hongera kwakupata mtoto bila kukojoa...
Makubwa, ukiona wanakusumbua huko nyumbani kwenu tuwasiliane nije kukachukua nilee mwenzenu. Nahis mambo ya kukandamizwa na kuzaa siwezi tena.
Barack Obama Sr kamkimbia mtoto, leo rais wa Marekani.
Mpe jina la Baraka kisha mlee kama mwanao mpaka atakapokuw mtu mzima.. Huwezi jua mipango ya Mungu.
Mkuu fuata taratibu kabisa za kupata uhalali wa kuishi na huyo mtoto. Kwanza kabisa ungepata barua ya utambulisho toka kwa mkuu wa kituo ubungo akieleza kuwa umeachiwa mtoto hivyo ukifika unakoishi unatakiwa kwenda kuripoti polisi ili uende ustawi wa jamii wa wilaya yako ili upata maelekezo ya kuishi na huyo mtoto. Usije ukabugi stepu tu ukawa katika kundi la wahalifu wa biashara ya binadamu.
Asante mkuu, sikajui hata jina, sijui nikape jina lingine?
Hmm...this is weird! Yaani unakubali tu kuchukua jukumu/ uamuzi wa kumlea mtoto uliyeachiwa kwenye basi na mtu ambaye hata humjui? Je huyo mtu naye akiwa alimuiba huyo mtoto kwingine? Una uhakika gani kama huyo mama aliyekuachia huyo mtoto ndo mama mzazi wa huyo mtoto?
Ingekuwa mimi ningempeleka tu polisi na kumsalimisha huko ili taratibu za kutafuta wazazi au ndugu ziendelee.
Halafu kuna aliwahi kuja na stori kama hii yako hapa.
Pole na hongera.....mapenzi ya mungu na makusudi yake......muite Dar express.....jina sio baya
Kaacha copy za vitambulisho na mawasiliano polisi
kama wanataka mtoto wao wamtafute.....
Ungekuwa wewe ....bahati nzuri ni yeye kaamua kumchukua mtoto.