Amicus Curiae
JF-Expert Member
- Sep 12, 2012
- 5,352
- 7,668
- Thread starter
-
- #81
Inasisimua na kutia huruma kwa mtoto ambaye ametelekezwa mikononi mwako... Nakushauri kaka mlee kama vile wakwako hadi hapo mama au ndugu wa mtoto watakapojitokeza ila nakusihi jitahidi kumfanyia ibada kupata kibali mbele za Mungu. Hatuwezi jua ametokea wapi.... Wengi wamesema ni baraka umeletewa, lakini pia kuna wakina Zinduna.
Mungu akubariki kwa moyo wa upendo ulio nao.
Mlee tu kaka. Vipi shem hana noma lakini isije akamtesa tu huyo malaika wa mungu?
Asante mkuu, sikajui hata jina, sijui nikape jina lingine?
Hongera sana,Mungu akupe uweza wa kumlea vema,na baya lolote lisitokee...
Imewahi kunitokea dar. Ni njia nzuri zaidi kuliko kuwatupa chooni ama kuwatelekeza majalalani. Ila kwa kufanya hivyo mi siku hizi simsaidii mwanamke yeyote kubeba mtoto. Mi nilitelekezewa kwenye daladala. Niliteseka sana na mtoto huyo
Ameen ya Rabb.kwa sote.Wow !! kumbe unajua kuchagua majina mazuri.... Nice name nice meaning !! nawe ubarikiwe SIMBA.
Nimekaacha kwa wazazi wangu, nakatafutia dada wa kukalea(yaya), mama amesisitiza kakae nyumbani umri wake usogee kwanza ndio kahamie kwangu
Mashkurra PromiseYou kwa ujuzi wako huo !! nikijaaliwa mtoto nakutafuta unipe nice and sweet name... plz. usipotee cheza karibu na uwanja wa MMU!!Ameen ya Rabb.kwa sote.
Nilikuja dar kikazi kwa takribani siku 4, sasa jana nikawa narudi mkoani kwangu. Wkt nipo Ubungo nimekaa kwenye dar express akaja mama mmoja mtu mzima mweupe amebeba mtoto, akaketi pembeni yangu, nikamsalimia nikapiga kimya.
Akaniomba nimbebee mtoto akajisaidie, nikakubali. Muda ukawa unazidi kwenda yule mama harudi! hadi basi linajaa hajarudi, mara kakaja kadem kamoja kakaketi kwenye ile siti ya yule mama nikapigwa na butwaa! nikamueleza kwamba ile siti ina mtu, akanionyesha tiketi yake ikabidi nimuamini kwamba kweli ile ni siti yake
Wkt basi linataka kuondoka ikabidi nimpe taarifa konda, tukashuka na konda na baadhi ya abiria hadi kituo kdg cha polisi ubungo, polisi hawakuniamini sana, wakadhani nafanya usanii nilipotaka kumuacha pale mtoto, ikabidi nipige copy vitambulisho vyangu na niache mawasiliano yangu niondoke na mtoto.
Wamama ndani ya basi wakawa wanapokezana kukabeba na kukalisha, ni katoto ka kiume, ka-handsome, baba, mama na girlfriend wangu nao hawaniamini, wanadhani ni mwanangu! Dah!
Nimekaacha kwa wazazi wangu, nakatafutia dada wa kukalea(yaya), mama amesisitiza kakae nyumbani umri wake usogee kwanza ndio kahamie kwangu
aisee pole sana....na hongera kwa moyo wako!
fanya mpango umuasili kabisa huyo mtoto ikiwa wewe na mchumbako mtakubaliana (nadhani itakuwa mkishaoana, si ndo iko ivo wakuu)
Pole na hongera.....mapenzi ya mungu na makusudi yake......muite Dar express.....jina sio baya
big up kwa hao wazaz wako
dah, pole sana. ila bora kakuachia wewe kuliko angetoa mimba au angemtupa dampo. hapo ana uhakika mtoto atalelewa atamtafuta ukubwani.