Nimeachana na mpenzi kisa Facebook

Nimeachana na mpenzi kisa Facebook

Halafu na wewe kwani fb ndio sehemu ya kuonesha mapenzi ya dhati, na je kama ulikuwa unatafuta likes then umteme? Sio deal but anaweza kuwa yuko okay
 
Kila Mtu Kuna Asichopendelea, Usifos Mtu Akubaliane Na Unachoona Wewe Kinafaa, Muhimu Toa Details Zake Fb Alafu Mwombe Msamaha Yaishe, Muendelee Narelation, On Otherside Inawezekana Anahofia Kukamatika Kwa Another Bf Kuwa Yupo Nawe Mchunguze Ujue Why Hapendi Umweke Fb? Kama Sababu Nizamsingi Muondoe Msonge Mbele

Ni sawa kabisa sio kulazimishana
 
Wakati wewe unaachana na MWEZIO KISA FACEBOOK MI NDO ILINIPATIA MKE NA SASA TUNA WATOTO WAWILI NA TUNAISHI KWA fURAHA NA Amani na Upendo ndani yake.
 
Facebook wafanye marekebisho ziwepo nafasi hata za kutosha watu watatu basi ili iwe in a relation with 1....2...and 3...., ingekuwa hivu dem asingekuacha mngetosha wote,sa we unataka uwekwe peke ako tu?acha hizo bana!!!!
 
Hivi mapenzi yako kwake ni mpaka umuweke Facebook?Huna maadili hata kidogo na umepotoka sana,yaani hapo hata uchumba bado umeanza kujitangaza fb,je ukioa itakuaje?Wengine wanapoamua kuingia kwenye mahusiano si kwamba wanataka iwe wazi kwa kila mtu maana wapo ambao wana wazazi wenye maadili ambayo si kama ya kwenu kutangaza mapenzi kwenye mitandao.
Huyo msichana yupo sahihi sana na yafaa umtoe huko kwenye mtandao,subiri umuoe ndio utangaze si sasa.
 
duu ulichemka mkuu aliekuambia mapenzi matangazo ni nani? si kila mtu anapenda ulimwengu ufahamu mambo yake. angekuwa ana mambo mengi ungemshitukia toka muda mrefu sna.
 
Wanawake wa sasa wanakuwa na wanaume wawili kupima upepo akiona upepo unavumia huku na bendera itaelekea huko huku ambako hakueleweshi anatupilia mbali kwamaana nyingine mbadala lazima uwepo
Sasa ulivyoweka status hivyo unamvurugia mwenzako hali ya hewa
 
Back
Top Bottom