Hismastersvoice
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 18,673
- 22,264
Mwaka jana 2022 Rais wa Zanzibar aliwahi kusema kuwa "ataongea na rais mwenzake wa Tanzania waone jinsi wanavyoweza kuanzisha mfuko wa mahujaji", mwisho wa kunukuu. Niliandika kuhoji ni vipi serikali itumie pesa za watanzania kwa ajili ya kundi moja kwenda Hija Macca! Ambao wangefaidika na pesa hizo walinibeza japo wengine walimezea.
Hao wanaolalama kuwa serikali inayapatia makanisa pesa wasidhani serikali nayo inatoa sadaka, pesa hizo ni kwa ajili ya kufidia huduma ambazo serikali imeshindwa kuzitoa na zinatolewa na makanisa kwa niaba yake. Ni hivi karibuni serikali ilifanya makubaliano na Aga Khan katika misingi hiyohiyo.
Hebu tujiulize ni waislamu gani waliojenga msikiti na makao makuu ya Bakwata Kinondoni? Ni waislamu gani waliojenga chuo kikuu cha kiislamu Morogoro? Mbona hakuna waliolalamika, tuamini kuwa serikali haigawi hela hivihivi ni lazima ziwepo sababu za msingi, jenga mradi utakao lenga jamii moja kwa moja serikali itakusaidia(ruzuku).
Hao wanaolalama kuwa serikali inayapatia makanisa pesa wasidhani serikali nayo inatoa sadaka, pesa hizo ni kwa ajili ya kufidia huduma ambazo serikali imeshindwa kuzitoa na zinatolewa na makanisa kwa niaba yake. Ni hivi karibuni serikali ilifanya makubaliano na Aga Khan katika misingi hiyohiyo.
Hebu tujiulize ni waislamu gani waliojenga msikiti na makao makuu ya Bakwata Kinondoni? Ni waislamu gani waliojenga chuo kikuu cha kiislamu Morogoro? Mbona hakuna waliolalamika, tuamini kuwa serikali haigawi hela hivihivi ni lazima ziwepo sababu za msingi, jenga mradi utakao lenga jamii moja kwa moja serikali itakusaidia(ruzuku).