👉 NILIVYONUSURIKA KUUWAWA MARA 2 NA MWANAMKE WANGU WA ZAMANI MUHA
1. Siku moja usiku ulitokea mgogoro kati yangu na yeye, bahati mbaya sana yule muha alikuwa akikasirika hata hekima hana na wala haogopi mtu yeyote. Anaweza akafanya matukio ya kijinga sana mpk aibu kwangu, mgogoro ulianza saa 4 usiku baada ya mimi kumuuliza jambo fulani na akanijibu hovyo, tulirushiana maneno ye akiwa amekaa chini mimi nipo kitandani nimejilaza, baada ya malumbano ya muda mrefu mi nikapitiwa na usingizi eeeeh nilikuja kushitushwa na kalamu ya biki ikichoma tumboni na kwa bahati nzuri nilikuwa nimejifunika shuka nzito hivyo ile pen ilichoma ikashindwa kupenya ikakatika, sa fikiria bic pen umchome nayo mtu ishindwe kupenya mpaka ikatike.
Maana yake kama nisingekuwa nimejifunika shuka hilo na npo kifua wazi pengine ningekufa siku hiyo usku mnene hapo inasoma saa nane usku.
2. Siku moja usku ulitokea mzozo kama kawaida alikuwa mtata mwenye dharau na mjeuri sana, ilikuwa usku tumelala vema kwa mgogoro, mi nilikuwa naamka alfajiri kuwahi kazini si mnajua mambo ya dsm.
Nimemaliza kujiandaa mida ya saa kumi alfajiri, nikafungua mlango nikatoka eeeh 😡 kumbe ile nmepiga hatua kadhaa tu mbele nashangaa chupa la uji wa mtoto linanipta kichwani na kuanguka mbele yangu, kisha nasikia matusi na maneno leo nongekuuua mbwa ww akafunga mlango, maana yake kama ile chupa ingenipata kwenye kichogo basi sjui ingekuaje sku hiyo.