GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 7,648
- 10,843
Utaenda tu mkuu! Penye nia pana njia.Nataman na mimi siku moja niende huko
Utaenda tu mkuu! Penye nia pana njia.Nataman na mimi siku moja niende huko
Maajabu! Hayo ndiyo nayasikia leo. Nilijua ukishajulikana ni Mtanzania unatetemekewa kumbe ni kinyume chake?Sikuwa najua basi nikajua ukisema mtz na vile story zetu sijui za kupigania uhuru na bra bra zingine ntaonekana mwamba dah niliukana utz on the sport warundi na wamalawi wanaaminika kidogo
Sababu hasa za vurugu zilisukumwa na nini kama unakumbuka?....ni raia wa kundi lipi walilengwa zaidi ?Zile kwa sehemu kubwa zinatokea Gugu lethu na Keiricha huku Capricorn ni WA colored ambao hawana sana hayo mambo so sikuweza kuzishuhudia zaidi ya kuzisikia
Zilitokea 2008 nikiwepo haikuwa poa mji ulikaa kimachale sana binafsi nilikuwa na Lungile sikuwa na shida
Seen.Nimeona watu wakishare namna walivyopambana na baadhi ya matukio katika maisha Yao nami nimeona sio mbaya Leo nikaeleza namna nilivyonusurika kifo katika harakati za kutafuta maisha.
Mwaka 2007 nikiwa kijana mdogo 18yrs niliamua kwenda kutafuta maisha South Afrika nikitokea Dar na hii ni baada ya serikali kuwa imevunja maduka na vibanda pale kariakoo chini ya ndugu Kandoro akiwa mkuu wa mkoa wa Dar
Kama ilivyokuwa kwa baadhi ya vijana nami nikiwa mmoja wao tuliona Giza mbele yetu binafsi nikaamua kuja kufungua duka Ukonga Mombasa ambapo baadae niliona kama halinipi maisha niliyokuwa nayataka(duka la Mangi)hivyo niliamua kumuita mama na kumkabidhi Ile biashara na kumuambia mi nataka kwenda SA kutafuta maisha.
Mama hakukubaliana na wazo langu Moja kwa Moja ila unajua sisi vijana wa kiume huwa tukiamua tena dam changa inakuwa sio rahisi kutuzuia basi hakuwa na namna aliruhusu nikafanya taratibu za pasipoti na viza (sikutaka kuzamia)nikapata na safari ya SA ikaanzia pale ubungo muelekeo ukiwa ni kupitia Zambia
Sasa mi nilikuwa naelekea Cape town maana huko ndio nilisikia maisha yapo na kusema kweli Kuna rafiki alikuwa kule (mrundi)alipita mitaa yangu nikamsaidia kwenda huko basi akawa anasema njoo.
Sasa kitu nilichemka ni hela maana kuhofia nisifilisi duka na kumuacha mama mnyonge ilibidi nijaze sana duka Kisha nichukue hela kidogo sana nadhani ilikuwa haizidi laki 3 ambayo niliichange kwenye dollar na Randi
Siku ikafika nikapanda basi hadi tunduma Mbeya kufika pale basi likadumu pale siku nzima ambapo Sasa tukajichuja na wanaoenda SA tukaonana rasmi na tukaanza kushare story za ndoto yetu hii kuu tulikuwa kama 6 mmoja mwenyeji si wengine wageni ila Hawa wengine 5 walikuwa wanajuana
Nikiwa tunduma pale ndio niligundua kuwa nimechukua hela kidogo kichwa kikawaka moto ila nikasema liwalo na liwe sirudi nyuma ,kufika jioni tukaenda kugonga pasipoti pale mpakani yule askari akaniuliza unaenda SA!?nikasema ndio akahoji mbona hujui kiingereza sikumjibu ukweli pale ndio nikajua umuhimu wa kingereza nje ya Tanzania
Safari yetu iliendelea hadi Lusaka ambapo tulifika asubuhi na kuunganisha gari kuelekea Zimbabwe
Tulifika Zimbabwe usiku kidogo pale Harare Kisha tukachukua hiace hadi mahali pengine ambapo ndio tulitakiwa kuchukua gari kwenda Beit Bridge hapa tulilipa nauli kubwa sana sijui kama niliibiwa au lah ila ndipo hela ilipoishia na nikabaki na Randi 120 pekee mfukoni hapa kumbuka kwa vile sikuwa na hela basi nililazimika kujizuia kutokula kwa hiyo nilikuwa na njaa sio poa
Tulifika Beit bridge asubuhi kama saa Moja hivi Sasa hapa ndio wale jamaa watano baada ya kuona kama vile story zetu haziendani wakaniambia hapa Sasa si tutaenda njia yetu na wewe inabidi uende njia Yako Mungu akipenda tukutane Joburg nikasema poa sikutaka kuonesha huruma
Nikatembea hatua kadhaa mbele yangu ikapaki hiace kubwa (dungu)na wakaniuliza "my friend Jo burg !?"nikasema Yes basi wakachukua ka begi kangu hadi ndani nami nikaingia nakutulia!!!!
Ndugu zangu hapa ndio muujiza ulipotokea na hadi Leo sijawahi kusahau
Ile hiace haikuvuka mpaka Bali ilirudi nyuma na kupaki kwenye kaeneo kama kaliko jitenga hivi Kisha jamaa aliyekuwa kama kiongozi wa Ile gari akaanza kunipa interview ya natoka wapi na naelekea wapi Kisha akaniambia kuwa Kuna abiria wanawangoja Kisha tutaondoka lakini mi nikiangalia gari naona imejaa ila ni vijana na mabinti ambao wote wanaonekana kujuana
Majira ya mchana hivi jamaa walichukua pasipoti yangu na Randi 100 Ile Randi 20 nilikuwa nimeificha sehem nyingine hapo Sasa nikajua kuwa siko mahali salama ila nikatulia sana pasi na kuonesha hofu yoyote
Jamaa kwanza wakaenda kuninunulia chakula supermarket ila nilikataa kula nikawaambia nimefunga na kuweka nadhiri kwa Mungu nitakula nitakapokanyaga SA (hii ni kweli) basi hawakunilazimisha
Siku ikaendelea nikawa nimetoa biblia na kuendelea kusoma jambo lingine ambalo hawakulielewa wale jamaa ni kuwa lugha Yao ya kizulu ni kibantu hivyo nilikuwa naelewa Kila wanachoongea angalau kwa uchache
Majira ya saa Moja jioni ikaja gari Moja nyeusi inayoweza kubeba watu watano basi jamaa wakaniambia my friend ingia ndani ya hiyo gari itakupeleka Joburg nikasema poa hakuna shida sikuhoji hata kidogo
Ndani ya Ile gari nilikaa kati ya jamaa wakubwa hatari dereva na jamaa mmoja walikaa mbele tukaenda kuvuka mpaka wa Zimbabwe pale nikaona Kuna signal baina ya mtu wa uhamiaji Zimbabwe na jamaa mmoja wao nikapotezea ila nikaweka moyoni
Tukaenda kabla hujafika boda ya SA ya kukagua viza huwa Kuna ka boda kadogo pale kati ambapo mnavuka kwa miguu Ile sehemu nilikaguliwa hadi nikasema hapa Sasa mnirudishe TU tz basi tukaendlea hapa wale jamaa hawakukaguliwa ila jamaa walikuwa Kila hatua wameniweka kati wawili mbele watatu nyuma
Tulipofika Sasa kukagua viza pale boda ya SA watu ni wengi sana kwa hiyo mnapanga mstari na ule mstari ni mrefu sana na umejaa nidham ya hali ya juu hakuna kuvunja line basi tukaingia kwenye mstari kama kawaida mi Niko kati Sasa pale pembeni nikaona Bomba la maji nikasema hapa patam
Hapo walikuwa wamenirudishia pasipoti yangu ninayo mkononi nikaacha ule mstari ukaenda hadi kuingia ndani nikasema nasikia kiu ngoja nikanywe maji pale jamaa kama wakastuka ila wakapiga kimya
Nikatoka nikaenda pale bombani nikanywa maji kiuongo Kisha nikaenda ilipopaki gari kioo kilikuwa na nafasi nikakidandia nikatoa kibegi changu njia hadi polisi nikafika nikatulia pale polisi nikakuta Kuna polisi mmoja mbavu kinyama nikamwambia mkasa mzima jamaa akanielewa sijakaa dk hata moja jamaa wakaja kunitafuta pale polisi nikawaambia my friend siwaamini na naomba nisiongozane na nyie basi nikawa nimeponea namna hiyo
Yule polisi alinisaidia kuwasiliana na jamaa yangu Cape town ambae alikata tiketi ya treni kutoka Mesina hadi cape town asubuhi jamaa alinichukua na gari ya askari hadi Mesina akanipa maelekezo yote nilitumia Ile Randi 20 kupata chai asubuhi ndani ya SA jioni treni ikaja nikaanza safari yangu kuelekea Cape town
NB:huwa sio msimuliaji mzuri ila nimeona niweke hiki Kisa hapa ili siku Moja Nije kusoma na kukumbuka namna Mungu alivyonilinda ndani ya Ile nchi
Kama hujawahi kuishi SA basi hujui maana ya kuishi mahali penye hatari duniani Yale unayoona kwenye movie zao ni 4%ya uhalisia wa mitaa Yao
Niliishi Cape town kwa mwaka mmoja Joburg na Pretoria kidogo Kisha nikarejea kwenye nchi ya Samia
Mkuu, Wabongo wamefanyeje huko?Wamalawi nao siku hizi ni washenzi. Toka wajifananishe na wabongo na wenyewe wamekuwa wasela Mavi.
Wanakaba, wanapiga michomoko ya usiku, wanavaa kata K, na kupiga watu vitasa kama kawa.
Sio kwamba Nyerere hawamjui au Tanzania hawaijui au hawaipendi.Tusitishane basi mkuu!
Unataka kuniambia Warundi wanakubalika SA kuzidi Watanzania?
Hawamjui Nyerere?
Hata ukipanda la kuunga unga au moja kwa moja. Kama una document nzuri, na pia una maelekezo mazuri au una mwenyej wa kukuongoza basi hauwezi kukumbana na matatizo yoyote mpakani.Hata kwa abiria aliyepanda basi la moja kwa moja kutokea Dar kwenda SA kupitia Zimbabwe anaweza kukutana na hiyo changamoto ya kiusalama?
Ndio mkuu.Za Wazungu ni Kingereza na Kikaburu?
Nafikiri nishakufafanulia hapo chini mkuu.Kwa nini mkuu? Mimi nilijua ni Wanigeria ndiyo hawaaminiki.
Mkuu na hili pia nishalifafanua hapo chini.Mkuu, Wabongo wamefanyeje huko?
Mkuu Zimbabwe miaka ya 2000 kushuka chini, ilikuwa na uchumi mkubwa zaidi ya Kaburu.Mbona hakuna watu wanaopakimbilia huko kama nchi zingine?
Nilipata kidogo nikaja kukichanganya na makaratasi nikapata cheti kimoja(degree)basi Niko kwenye serikali nalalamikia daraja na seminarKwa huo muda ukioishi huko bila shaka ulijiwekea akiba na kuja kuanza upya Bongo!., ninn ndugu yangu alienda huko ile miaka ya mwanzo kabisa, hapo akapata demu za kiingereza wameenda kuishi Uk, wamepata watoto kadhaa, kiukweli hakuna alichofanya bongo.Baba, mama na ndugu wengine wamefariki hata kuja kutoa Pole ameshindwa...
Basi hapo wamepoteza point ila way back wao walikuwa na unafuu kidogoWamalawi nao siku hizi ni washenzi. Toka wajifananishe na wabongo na wenyewe wamekuwa wasela Mavi.
Wanakaba, wanapiga michomoko ya usiku, wanavaa kata K, na kupiga watu vitasa kama kawa.
Hawakupi maana nao hawazai sana Lungi nilimkuta na mtoto mmoja na hakuhitaji kabisa kuzaa tena ila mapenzi wanataka siku nzima (holiday)Ni kweli aisee, hawa watu kukuachia mtoto sio rahisi. Labda kama ana uhakika utaendelea kuishi hapa hapa, so anaweza kumleta mara moja moja.
Mi mara ya kwanza nilipambana imagine naokoa baiskel mara ya pili nilikutana na colored Wana panga za maana nikawauliza Nini wao Rand mbona niliwapa kiroho safi wakaondoka bila kunigusaHabari imefika,dogo wangu alilambwa visu mara 4.
Nilimpeleka mwenyewe akatafute maisha nikamrudisha mwenyewe.
Definitely jamaa wanakuwa na Lab kabisa ni unapigwa operations za maana viungo vinauzwa wanaenda kula nyama na pombe na vile afya iko poa wasingeacha kitu hata pale mpakani wako selective sanaHao jamaa walikuwa wanaenda kumfanya jamaa kitu mbaya walikuwa wanaenda kugawana viungo