Nilivyonusurika kifo Beit bridge

Nilivyonusurika kifo Beit bridge

Ni kweli na nashukuru Mungu nilifika mchana na kesho yake nikaanza kazi mama mwenye nyumba aliniambia"you are lucky I lived in cape town four years without a job and you came yesterday today you have a job"
Niliona uchungu wake ila baadae alinipenda sana kutokana na umri sikuwa na mambo mengi Wala migogoro Sasa ye umeme ukiisha nasikia sim TU "William come with power is finished"Binti yake asubuhi namtoa nauli basi maisha yakawa hivyo.
Kwa huo muda ukioishi huko bila shaka ulijiwekea akiba na kuja kuanza upya Bongo!., ninn ndugu yangu alienda huko ile miaka ya mwanzo kabisa, hapo akapata demu za kiingereza wameenda kuishi Uk, wamepata watoto kadhaa, kiukweli hakuna alichofanya bongo.Baba, mama na ndugu wengine wamefariki hata kuja kutoa Pole ameshindwa...
 
Sikuwa najua basi nikajua ukisema mtz na vile story zetu sijui za kupigania uhuru na bra bra zingine ntaonekana mwamba dah niliukana utz on the sport warundi na wamalawi wanaaminika kidogo
Wamalawi nao siku hizi ni washenzi. Toka wajifananishe na wabongo na wenyewe wamekuwa wasela Mavi.

Wanakaba, wanapiga michomoko ya usiku, wanavaa kata K, na kupiga watu vitasa kama kawa.
 
Mzungu hapana nilipata Mxhosa Lungile mi sikuishi sana kwa wazulu nimeishi na WA xhosa na colored
Huyu alikuwa mtoto wa mwenye nyumba nilikuwa namsaidia nauli sana Kila asubuhi mwisho tukawa kwenye mahusiano lakini yalikuwa ya ndani TU sikutaka kufatana kuepuka ligi za wazawa
Ulitisha sana bruh 😄
 
Mkuu,
Ukonga mombasa mitaa gani?
Wale jamaa hawakukufatilia tena?

Nafikiri wale wa kwanza na hao jamaa ni kitu kimoja na kile chakula walichokuwa wanakununulia huenda kilikuwa na madawa.

Sijui walitaka kwenda kukuuza
Pole sana kwa mkasa huo mkuu!
Wangeenda kummaliza wamnyofoe Figo wauze. Duniani ku a deal nyingi chafu. Nadhani kusoma bibilia kulimuokoa huyu
 
Nimeona watu wakishare namna walivyopambana na baadhi ya matukio katika maisha Yao nami nimeona sio mbaya Leo nikaeleza namna nilivyonusurika kifo katika harakati za kutafuta maisha.

Mwaka 2007 nikiwa kijana mdogo 18yrs niliamua kwenda kutafuta maisha South Afrika nikitokea Dar na hii ni baada ya serikali kuwa imevunja maduka na vibanda pale kariakoo chini ya ndugu Kandoro akiwa mkuu wa mkoa wa Dar

Kama ilivyokuwa kwa baadhi ya vijana nami nikiwa mmoja wao tuliona Giza mbele yetu binafsi nikaamua kuja kufungua duka Ukonga Mombasa ambapo baadae niliona kama halinipi maisha niliyokuwa nayataka(duka la Mangi)hivyo niliamua kumuita mama na kumkabidhi Ile biashara na kumuambia mi nataka kwenda SA kutafuta maisha.

Mama hakukubaliana na wazo langu Moja kwa Moja ila unajua sisi vijana wa kiume huwa tukiamua tena dam changa inakuwa sio rahisi kutuzuia basi hakuwa na namna aliruhusu nikafanya taratibu za pasipoti na viza (sikutaka kuzamia)nikapata na safari ya SA ikaanzia pale ubungo muelekeo ukiwa ni kupitia Zambia

Sasa mi nilikuwa naelekea Cape town maana huko ndio nilisikia maisha yapo na kusema kweli Kuna rafiki alikuwa kule (mrundi)alipita mitaa yangu nikamsaidia kwenda huko basi akawa anasema njoo.
Sasa kitu nilichemka ni hela maana kuhofia nisifilisi duka na kumuacha mama mnyonge ilibidi nijaze sana duka Kisha nichukue hela kidogo sana nadhani ilikuwa haizidi laki 3 ambayo niliichange kwenye dollar na Randi

Siku ikafika nikapanda basi hadi tunduma Mbeya kufika pale basi likadumu pale siku nzima ambapo Sasa tukajichuja na wanaoenda SA tukaonana rasmi na tukaanza kushare story za ndoto yetu hii kuu tulikuwa kama 6 mmoja mwenyeji si wengine wageni ila Hawa wengine 5 walikuwa wanajuana

Nikiwa tunduma pale ndio niligundua kuwa nimechukua hela kidogo kichwa kikawaka moto ila nikasema liwalo na liwe sirudi nyuma ,kufika jioni tukaenda kugonga pasipoti pale mpakani yule askari akaniuliza unaenda SA!?nikasema ndio akahoji mbona hujui kiingereza sikumjibu ukweli pale ndio nikajua umuhimu wa kingereza nje ya Tanzania
Safari yetu iliendelea hadi Lusaka ambapo tulifika asubuhi na kuunganisha gari kuelekea Zimbabwe

Tulifika Zimbabwe usiku kidogo pale Harare Kisha tukachukua hiace hadi mahali pengine ambapo ndio tulitakiwa kuchukua gari kwenda Beit Bridge hapa tulilipa nauli kubwa sana sijui kama niliibiwa au lah ila ndipo hela ilipoishia na nikabaki na Randi 120 pekee mfukoni hapa kumbuka kwa vile sikuwa na hela basi nililazimika kujizuia kutokula kwa hiyo nilikuwa na njaa sio poa

Tulifika Beit bridge asubuhi kama saa Moja hivi Sasa hapa ndio wale jamaa watano baada ya kuona kama vile story zetu haziendani wakaniambia hapa Sasa si tutaenda njia yetu na wewe inabidi uende njia Yako Mungu akipenda tukutane Joburg nikasema poa sikutaka kuonesha huruma
Nikatembea hatua kadhaa mbele yangu ikapaki hiace kubwa (dungu)na wakaniuliza "my friend Jo burg !?"nikasema Yes basi wakachukua ka begi kangu hadi ndani nami nikaingia nakutulia!!!!

Ndugu zangu hapa ndio muujiza ulipotokea na hadi Leo sijawahi kusahau
Ile hiace haikuvuka mpaka Bali ilirudi nyuma na kupaki kwenye kaeneo kama kaliko jitenga hivi Kisha jamaa aliyekuwa kama kiongozi wa Ile gari akaanza kunipa interview ya natoka wapi na naelekea wapi Kisha akaniambia kuwa Kuna abiria wanawangoja Kisha tutaondoka lakini mi nikiangalia gari naona imejaa ila ni vijana na mabinti ambao wote wanaonekana kujuana

Majira ya mchana hivi jamaa walichukua pasipoti yangu na Randi 100 Ile Randi 20 nilikuwa nimeificha sehem nyingine hapo Sasa nikajua kuwa siko mahali salama ila nikatulia sana pasi na kuonesha hofu yoyote
Jamaa kwanza wakaenda kuninunulia chakula supermarket ila nilikataa kula nikawaambia nimefunga na kuweka nadhiri kwa Mungu nitakula nitakapokanyaga SA (hii ni kweli) basi hawakunilazimisha

Siku ikaendelea nikawa nimetoa biblia na kuendelea kusoma jambo lingine ambalo hawakulielewa wale jamaa ni kuwa lugha Yao ya kizulu ni kibantu hivyo nilikuwa naelewa Kila wanachoongea angalau kwa uchache
Majira ya saa Moja jioni ikaja gari Moja nyeusi inayoweza kubeba watu watano basi jamaa wakaniambia my friend ingia ndani ya hiyo gari itakupeleka Joburg nikasema poa hakuna shida sikuhoji hata kidogo

Ndani ya Ile gari nilikaa kati ya jamaa wakubwa hatari dereva na jamaa mmoja walikaa mbele tukaenda kuvuka mpaka wa Zimbabwe pale nikaona Kuna signal baina ya mtu wa uhamiaji Zimbabwe na jamaa mmoja wao nikapotezea ila nikaweka moyoni
Tukaenda kabla hujafika boda ya SA ya kukagua viza huwa Kuna ka boda kadogo pale kati ambapo mnavuka kwa miguu Ile sehemu nilikaguliwa hadi nikasema hapa Sasa mnirudishe TU tz basi tukaendlea hapa wale jamaa hawakukaguliwa ila jamaa walikuwa Kila hatua wameniweka kati wawili mbele watatu nyuma

Tulipofika Sasa kukagua viza pale boda ya SA watu ni wengi sana kwa hiyo mnapanga mstari na ule mstari ni mrefu sana na umejaa nidham ya hali ya juu hakuna kuvunja line basi tukaingia kwenye mstari kama kawaida mi Niko kati Sasa pale pembeni nikaona Bomba la maji nikasema hapa patam
Hapo walikuwa wamenirudishia pasipoti yangu ninayo mkononi nikaacha ule mstari ukaenda hadi kuingia ndani nikasema nasikia kiu ngoja nikanywe maji pale jamaa kama wakastuka ila wakapiga kimya

Nikatoka nikaenda pale bombani nikanywa maji kiuongo Kisha nikaenda ilipopaki gari kioo kilikuwa na nafasi nikakidandia nikatoa kibegi changu njia hadi polisi nikafika nikatulia pale polisi nikakuta Kuna polisi mmoja mbavu kinyama nikamwambia mkasa mzima jamaa akanielewa sijakaa dk hata moja jamaa wakaja kunitafuta pale polisi nikawaambia my friend siwaamini na naomba nisiongozane na nyie basi nikawa nimeponea namna hiyo

Yule polisi alinisaidia kuwasiliana na jamaa yangu Cape town ambae alikata tiketi ya treni kutoka Mesina hadi cape town asubuhi jamaa alinichukua na gari ya askari hadi Mesina akanipa maelekezo yote nilitumia Ile Randi 20 kupata chai asubuhi ndani ya SA jioni treni ikaja nikaanza safari yangu kuelekea Cape town
NB:huwa sio msimuliaji mzuri ila nimeona niweke hiki Kisa hapa ili siku Moja Nije kusoma na kukumbuka namna Mungu alivyonilinda ndani ya Ile nchi
Kama hujawahi kuishi SA basi hujui maana ya kuishi mahali penye hatari duniani Yale unayoona kwenye movie zao ni 4%ya uhalisia wa mitaa Yao
Niliishi Cape town kwa mwaka mmoja Joburg na Pretoria kidogo Kisha nikarejea kwenye nchi ya Samia
Yaani wewe "dogo" mpaka nakuonea wivu! Kwa umri huo mdogo ulitinga South Africa peke yako, ukiwa hujui lugha! Sijui hiyo ndiyo inaitwa "kujilipua!"

Hongera 👏👏👏🙏
 
Hivyo ni vingi mno mkuu na mi sio msimuliaji mzuri ila tangu naingia Musina hadi nafika Cape ni miujiza TU
Kwanza pale Musina nilienda kunywa chai na slace ya mkate mama muuza akaniuliza unatoka nchi gani nikamwambia "Tanzania"akainuka kwa tahadhari kubwa na kuondoka pale ndio nikajua tz ni red flag kwa SA baada ya hapo kwa utulivu TU Nika switch ukiniuliza natoka wapi nasema Burundi basi
Sikutaka kutengwa
Tusitishane basi mkuu!

Unataka kuniambia Warundi wanakubalika SA kuzidi Watanzania?

Hawamjui Nyerere?
 
Aisee mkuu pole kwa yaliokukuta pale BeitBridge. Kiufupi watu wengi wamekutana na madhila makubwa na ya kutisha katika boda ile.

Nashukur Mungu mimi wakati nakuja kwa mara ya kwanz, nilikuwa na marehem mjomba wangu ambae alikuwa ni mwenyej wa muda mrefu hapa Kaburu. Na pia njia nyingi zenye usalama alikuwa anazijua.
Hata kwa abiria aliyepanda basi la moja kwa moja kutokea Dar kwenda SA kupitia Zimbabwe anaweza kukutana na hiyo changamoto ya kiusalama?
 
Ckuwa na chochote. ilikuwa ile miaka ya uenda wazim kuzamia. Nikapenya mpaka pale askari mmoja mzungu akaniuliza maswali flan akaniachia ile naanza kuingia askari mmoja mswahili akanistopisha ile kuniuliza baadhi ya mambo ckuwa na majibu japo nilikuwa na hela flan. Wakanikamata. Nikapikiwa kwenye gar nyumban. Kipindi hicho Harare ilikuwa safi Nairobi inasubiri
Aisee
 
Hahaha pole sana aisee. Kweli ulikuwa na bahati mbaya mkuu, maana ungefanikiwa kupenya maybe saa hizi ungekuwa mbali kimaisha.

Kuhusu Harare mpaka sasa bado iko vizuri, japo upatikanaji wa kazi, na gharama za maisha zimepanda ukilinganisha na miaka hiyo.
Mbona hakuna watu wanaopakimbilia huko kama nchi zingine?
 
Back
Top Bottom