BILGERT
JF-Expert Member
- Feb 27, 2015
- 6,535
- 10,974
Plan yako uanze na kajumba ka room ngp mkuu.Life nshaanza ila sijajenga, nikianza maisha ya ujenzi naanza na nyumba ndogo baadae ntakuja ifanya Boys Quater!
Plan yako uanze na kajumba ka room ngp mkuu.Life nshaanza ila sijajenga, nikianza maisha ya ujenzi naanza na nyumba ndogo baadae ntakuja ifanya Boys Quater!
Dream house ya vyumba viwili,,????? Hongera mkuuHabari wana JF!
Uzi....
Mwaka 2017 nilikuwa na rafiki yangu akaniambia kuna mahali panauzwa Viwanja akashauri twende kuangalia, Mimi sikuwa na pesa kwa wakati ule ila nilienda, tulipofika kweli tukakutana na wahusika na viwanja vilikuwa vizuri tukaongea, kwakuwa mimi Sikuwa na kitu niliomba kile kiwanja niwe nalipa kwa installment, wakakulali nikawalipa pesa yao ndani ya kipindi fulani. Baada ya hapo nikawa na changamoto ya namna ya kukilinda kiwanja sababu eneo hilo palikuwa na janja janja flani hv so nikaamua kumwaga mawe ili kulinda eneo,
Nakumbuka nilikuwa namwaga trip moja kila mwezi, baada ya trip kadhaa nikaona pia haitoshi nikawa nalipia tofali kidogo kidogo. Nikawa sasa naanza kuwaza kujenga, nikawa natafuta ushauri kwa watu mbali mbali na mwisho nikaenda kwa architec akanichorea kabisa ramani ya dream house, Sasa bhana katika ile dream house nikamtafuta fundi anipe makadirio alooo nilipewa bajeti yangu ya miaka kama 10 hivi nikashtuka kidogo, Yaani ni hivi nilipiga hesabu ya kujenga ile nyumba nikagundua kuwa kutoka na kipato changu itanichukua si chini ya miaka 10 kumaliza, Yaani nitaishi kwenye nyumba ya kupanga nikilipa tena kodi kwa miaka 10 huku nimewekeza pesa zangu site na siwezi kizitumia. Sasa nikaona isiwe kesi nikarudi home nikamshirikisha Mke wangu, tukaona itakuwa ngumu kwetu hvyo tukakubaliana kuwa tufanye ujenzi ambao utaisha ndani Ya muda mfupi ili tuweze kujenga dream house lakini wakati huo huo tuwe tunaishi kwetu ambapo tutaishi kwa uhuru bila manyanyaso wala masimango ya mtu.
Basi kwa mfumo ule ule wa kuweka kidogo kidogo tulipambana na hatimae 2021 tulihamia kwenye nyumba yetu rasmi...
MWISHO:
Thread hii nimeandika kwa lengo la kukutia moyo na hamasa kuwa hatuhitaji pesa nyingi ndio tujenge, tunahitaji kujenga future zetu tungali bado vijana. Mambo yale yanayohitaji nguvu kubwa yote tuyafanye sasa tukiwa bado wadogo na ikiwa bado hatuna wategemezi wengi.
View attachment 2070738
Nyumba ya vyumba vitatu ingeenda 30MPesa yote hii si bora tuu ungejenga nyumba ya vyumba 3?
Naamini hujasoma post umejibu tu..kujifurahishaDream house ya vyumba viwili,,????? Hongera mkuu
hii ramani imechorwa na architect kweli? Sehemu vilipowekwa vyoo si sahihi. Hii imefanya kila chumba kiwe na dirisha moja tu
Hata hiyo bedroom mlango wake hauko sehemu sahihihii ramani imechorwa na architect kweli? Sehemu vilipowekwa vyoo si sahihi. Hii imefanya kila chumba kiwe na dirisha moja tu
acha dharau tunatofautiana kipatoMkuu hako kajumba ndo kakujenga since 2017? Inaonekana matumizi yako ni makubwa mno au mshahara wako ni mdogo mno!