Nilivyojenga kiutani utani. Anza na ulicho nacho

Habari wana JF!

Uzi....
Mwaka 2017 nilikuwa na rafiki yangu akaniambia kuna mahali panauzwa Viwanja akashauri twende kuangalia, Mimi sikuwa na pesa kwa wakati ule ila nilienda, tulipofika kweli tukakutana na wahusika na viwanja vilikuwa vizuri tukaongea, kwakuwa mimi Sikuwa na kitu niliomba kile kiwanja niwe nalipa kwa installment, wakakulali nikawalipa pesa yao ndani ya kipindi fulani. Baada ya hapo nikawa na changamoto ya namna ya kukilinda kiwanja sababu eneo hilo palikuwa na janja janja flani hv so nikaamua kumwaga mawe ili kulinda eneo,

Nakumbuka nilikuwa namwaga trip moja kila mwezi, baada ya trip kadhaa nikaona pia haitoshi nikawa nalipia tofali kidogo kidogo. Nikawa sasa naanza kuwaza kujenga, nikawa natafuta ushauri kwa watu mbali mbali na mwisho nikaenda kwa architec akanichorea kabisa ramani ya dream house, Sasa bhana katika ile dream house nikamtafuta fundi anipe makadirio alooo nilipewa bajeti yangu ya miaka kama 10 hivi nikashtuka kidogo, Yaani ni hivi nilipiga hesabu ya kujenga ile nyumba nikagundua kuwa kutoka na kipato changu itanichukua si chini ya miaka 10 kumaliza, Yaani nitaishi kwenye nyumba ya kupanga nikilipa tena kodi kwa miaka 10 huku nimewekeza pesa zangu site na siwezi kizitumia. Sasa nikaona isiwe kesi nikarudi home nikamshirikisha Mke wangu, tukaona itakuwa ngumu kwetu hvyo tukakubaliana kuwa tufanye ujenzi ambao utaisha ndani Ya muda mfupi ili tuweze kujenga dream house lakini wakati huo huo tuwe tunaishi kwetu ambapo tutaishi kwa uhuru bila manyanyaso wala masimango ya mtu.
Basi kwa mfumo ule ule wa kuweka kidogo kidogo tulipambana na hatimae 2021 tulihamia kwenye nyumba yetu rasmi...

MWISHO:
Thread hii nimeandika kwa lengo la kukutia moyo na hamasa kuwa hatuhitaji pesa nyingi ndio tujenge, tunahitaji kujenga future zetu tungali bado vijana. Mambo yale yanayohitaji nguvu kubwa yote tuyafanye sasa tukiwa bado wadogo na ikiwa bado hatuna wategemezi wengi.
View attachment 2070738
Dream house ya vyumba viwili,,????? Hongera mkuu
 
Tunauza mbao kwa bei za jumla
2*4 fut 12=4400
2*4treated fut 12=4800
1*6 fut 12 = 4400
1*8 fut 12= 8500
1*8 ya fisherboard=9500
1*10=13500
1*10 ya fisherboard= 15000
2*2treated fut 12=2500
2*2 fut 12=2300
2*4treated fut 18=9500
2*6 fut 12=8500
2*6treated fut 18=16000
2*2treated fut 18=5000
2*3 fut 12=3500
1*4 fut 18=4000
1*4 fut 12=2500
Tunafanya delivery popote ulipo kwa Dar-es-salaam ,tunapatikana kwa namba hizi hapa 0759630751,
0654830416,
0687371138
vile vile huduma ya kuchana,kuranda na kusize mbao inapatikana ofisini kwetu ..
Ofisi zetu ziko Mbuyuni -Bagamoyo road
 
Back
Top Bottom