Jirani yangu kaniharibia makazi yangu

Dodoma moja

JF-Expert Member
Jan 3, 2014
307
177
Habari ya majukumu wakuu
Bila kuwachosha sana niende moja kwa moja kwenye mada, nilinunua kiwanja kwa ajili ya makazi pemebezoni mwa mji kipindi hicho bado palikuwa hapajachanganya sana kama sasa lakini kadri siku zilivyokuwa zinazidi kwenda paliendelea kubadilika na palichanganya sana kutokana na uwepo wa tawi la chuo kimoja maarufu na kufanya watu waongezeke kwa kasi na hata bei ya nyumba za kupanga kupanda maradufu.
Kipindi nanunua palikuwa hapajapimwa lakini tulipimiwa upimaji shirikishi na Halmashauri na ilipofika mwaka 2020 nikaanza kujenga taratibu hadi mwaka huu ambapo katika plan zangu ilikuwa ifikapo mwezi Mei nihamie lakini kipindi naanza ujenzi kulikuwa na eneo kubwa kidogo pembeni yangu nikawa nasikia linauzwa lakini kwa kuwa sikuwa na uwezo wa kulinunua na pia halikuwa akilini mwangu wala sikuhangaika nalo, siku moja nikasema ngoja niende site kukagua duh cha ajabu nikakutana na jengo linanyanyuka kwa kasi kwenye hilo eneo kuuliza majirani wakaniambia eneo limeuzwa na aliyenunua anajenga gesti yenye vyumba karibu 20 nikaishiwa pozi kuwa nitaishije na gesti pembeni yangu vip kuhusu ustawi wa familia yangu?
Sasa nimepata wazo na mim nimeamua kuibadilisha nyumba yangu kuwa lodge pia na fundi ameshanichorea ramani nitapata vyumba kama vitano ambavyo nitaanza navyo
Acha niendelee kubaki kwenye upangaji potelea pote although najua ninachokifanya lodge ikianza nitatumia ninachokipata kule nalipa kodi huku najenga taratibu sehemu nyingine uzuri nimeshanunua kiwanja kingine vilikuwa vinauzwa kwenye mradi wa Halmashsuri ambako hakuna ujinga wa mtu kujenga chochote anachojisikia tu baada ya kupata funzo kwa kilichotokea nikasema kwa sasa sitanunua squtter tena bora nigharamike kwa kununua bei kubwa lakin ni kiwanja ambacho nitajenga kwa amani na kuishi kwa amani pia

Naamini hata humu JF kuna wadau watakuwa walishakutana na changamoto kama yangu
 
Ajabu ni kwamba wote mtapata wateja kulingana na kiwango Cha ubora wa huduma zenu. Kwa hiyo unaweza kumkomoa au kujikomoa!

Pole mkuu...nimejifunza kitu. Pembeni mwa kiwanja kuna mtu anauza ngoje nijichange nikinunue.
 
Me nahisi ulivyoskia guest umehisi kama vile kutakuwa na malaya wanajiunza kama sinza.

Guest haina ishu kabisaa
 
Wewe jamaa inaonekana una umimi sanaaaaa, na wivu wa kijinga mnoo yaani... sasa hapo kakuaribiaje huyo jirani yako? Maswala ya yeye kuwek bati nyeupe wewe msouth etc ... Acha hizo,
 
Wewe jamaa inaonekana una umimi sanaaaaa, na wivu wa kijinga mnoo yaani... sasa hapo kakuaribiaje huyo jirani yako? Maswala ya yeye kuwek bati nyeupe wewe msouth etc ... Acha hizo,
Akizeeka atakuwa mchawi
 
Habari ya majukumu wakuu
Bila kuwachosha sana niende moja kwa moja kwenye mada, nilinunua kiwanja kwa ajili ya makazi pemebezoni mwa mji kipindi hicho bado palikuwa hapajachanganya sana kama sasa lakini kadri siku zilivyokuwa zinazidi kwenda paliendelea kubadilika na palichanganya sana kutokana na uwepo wa tawi la chuo kimoja maarufu na kufanya watu waongezeke kwa kasi na hata bei ya nyumba za kupanga kupanda maradufu.
Kipindi nanunua palikuwa hapajapimwa lakini tulipimiwa upimaji shirikishi na Halmashauri na ilipofika mwaka 2020 nikaanza kujenga taratibu hadi mwaka huu ambapo katika plan zangu ilikuwa ifikapo mwezi Mei nihamie lakini kipindi naanza ujenzi kulikuwa na eneo kubwa kidogo pembeni yangu nikawa nasikia linauzwa lakini kwa kuwa sikuwa na uwezo wa kulinunua na pia halikuwa akilini mwangu wala sikuhangaika nalo, siku moja nikasema ngoja niende site kukagua duh cha ajabu nikakutana na jengo linanyanyuka kwa kasi kwenye hilo eneo kuuliza majirani wakaniambia eneo limeuzwa na aliyenunua anajenga gesti yenye vyumba karibu 20 nikaishiwa pozi kuwa nitaishije na gesti pembeni yangu vip kuhusu ustawi wa familia yangu?
Sasa nimepata wazo na mim nimeamua kuibadilisha nyumba yangu kuwa lodge pia na fundi ameshanichorea ramani nitapata vyumba kama vitano ambavyo nitaanza navyo
Acha niendelee kubaki kwenye upangaji potelea pote although najua ninachokifanya lodge ikianza nitatumia ninachokipata kule nalipa kodi huku najenga taratibu sehemu nyingine uzuri nimeshanunua kiwanja kingine vilikuwa vinauzwa kwenye mradi wa Halmashsuri ambako hakuna ujinga wa mtu kujenga chochote anachojisikia tu baada ya kupata funzo kwa kilichotokea nikasema kwa sasa sitanunua squtter tena bora nigharamike kwa kununua bei kubwa lakin ni kiwanja ambacho nitajenga kwa amani na kuishi kwa amani pia

Naamini hata humu JF kuna wadau watakuwa walishakutana na changamoto kama yangu

Ni vizuri mkuu, kwa asiye na mawazo kama yako atatukana tuu na kusema atakavyo
 
Je vip kuhusu watu wanaoingia na kutoka kwa familia siyo sawa na kuna effect zake
Guest and lodge mpishano wake sio kihivyo kama unavyozani wewe na mpishano unafnyika usiku na asubuhi sana mda ambao watu hawapo.
Na most of them sio watu wa mtaa huo au kama ni wa mtaa huo ujue humo ndani kuna kipub au grocery.

Sema makelele ya minyanduo kama hawataweka vizuri miundombinu.
 
Weka bar yenye uwanja mkubwa nje; tafuta ramani nzuri ya kaunta, store, jiko, na vyoo; weka pavement, na pendezesha mazingira, na uanze kupiga hela; wakitoka kuvunja amri ya sita ndani, wanakuja kupata kipozeo hapo.

Maisha ya sasa yanataka pesa, usipojihurumia hakuna atakayekuhurumia.​
 
Back
Top Bottom