Niliuwa kwa kukusudia-1

Niliuwa kwa kukusudia-1

itabidi ungojee mpaka kesho ndio upate kuisoma hadithi yangu.

Acha ubahili wako hunipi (Like) Mpaka niombe?

Mnalalamika Story fupi basi hata kunipa (Like) Mnashindwa? ahhhh acha uchoyo wako sio mtu mzuri.

Mnalalamika Story fupi basi hata kunipa (Like) Mnashindwa? ahhhh wachoyo nyinyi sio watu wazuri.

Huwa natoa like yangu kwanza ndo naendeleza porojo zingine.
 
Niliua kwa Kukusudia-12-

ILIPOISHIA :
Nikaelekea kwenye kituo cha kupanda mabasi hadi Ubungo ambako nilichukua gari la kwenda Chalinze. Niliwasili Chalinze saa tatu na nusu asubuhi. Nikapanda baiskeli hadi nyumbani.
“Aiii, jamani dada,” alisema Inana baada ya kuniona na kunikimbilia kwa furaha kubwa.
SASA ENDELEA...


Habari za huko jamani dada?”
“Nzuri, sijui wewe?”
“Salama jamani.”
“Za hapa nyumbani vipi?”

“Mm! Nipo nahangaika hivyohivyo, Mungu anasaidia sana.”
Nilimlipa yule mwendesha baiskeli ya kukodisha ujira wake. Akaondoka na kutuacha na Inana.
“Nilikukumbuka sana mdogo wangu.”
“Hata mimi dada, unaendeleaje huko Dar es Salaam?”

“Vizuri, ngoja nikikaa nitakusimulia yote. Kwa sasa ngoja nipumzike kidogo.”
Hali niliyoikuta nyumbani ilinitia simanzi. Kijumba kibovu kilikuwa kimezidi kujiinamia. Nikamuangalia Inana. Moyo uliniuma mno. Hakika niliumia kupita kiasi.
Nikashindwa kuingia ndani kwanza, nikawa nakikagua kile kijumba chetu kwa macho.

“Dada,” Inana aliniita huku akinisogelea baada ya kupeleka ndani kifurushi nilichokuwa nimebeba.
“Bee,” niliitika huku nikijifuta machozi kwa kiganja cha mkono wa kushoto.
“Kuna jambo nataka nikuambie,” alisema Inana na kunifanya nimuangalie kwa umakini ili nisikie alichokusudia kunieleza.

“Ha! Sasa mbona unalia tena dada?”
“Maisha mdogo wangu, maisha Inana.”
“Kwani hujafanikiwa kupata kazi ?”
“Siyo hivyo.”
“Sasa kumbe nini tena?”

“Hii hali Inana, inaniuma sana kuona tuko katika hali hii.”
“Mmh!” Inana aliishia kuguna.
“Hee, wewe Inana wewe.”
“Vipi dada.”
“Yaani siku hizi una simu?” nilimuuliza Inana kwa taharuki kubwa baada ya kuona ameshikilia simu kwa mkono wa kushoto.

“Mmh!, ina maana dada ndiyo umeiona sasa hivi?”
“Eee, nilikuwa sijaona kabisa umenunua simu!” nilisema huku nikikaa kwenye mfuko wa foronya uliokuwa karibu na mahali tulipokuwa.
Mshangao na maswali yangu mengi, yakamfanya Inana asahau alichotaka kuniambia baada ya kuniita.
Inana alikuwa amenunua simu aina ya sumsung. Ilikuwa ni fupi yenye mwanga wa njano kila ikiwaka.
“Nimebangaiza polepole kwa kujinyima dada, maisha ni magumu sana,” alinieleza Inana akiwa anaishika simu yake.

“Sasa inakusaidia nini kwa sasa,” nilimuuliza huku nikimkazia macho ya udadisi mkubwa.
“Inanisaidia kwa mambo mengi mno dada.”
“Kama yapi?”
“Kuna wakati vibarua huwa vya shida sana, ninalazimika kukaa nyumbani, lakini vikipatikana, watu mbalimbali wenye namba zangu hunipigia na kunitaarifu kuwa sasa vinapatikana,” Inana alinijibu kwa kirefu na kunifanya nimuelewe.

“Haya bwana, nimekuelewa.”
“Vipi huko mjini, maisha yanaendeleaje?”
“Mungu anasadia sana.”
“Aisee.”
“Unamkumbuka yule mwarabu aliyenigonga kwa gari wakati ule?”
“Ee dada.”

“Basi nilikutana naye.”
“Ha! Ikawaje sasa,” Inana aliniuliza kwa shauku ya kutaka kujua kilichojiri.
Nikamweleza jinsi nilivyokutana na yule mwarabu.
Hadi jinsi alivyonisaidia kupata kazi hotelini kwake. Inana alishangaa sana kusikia nafanya kazi kwenye hoteli ya yule mwarabu.

“Aisee Mungu ni wa ajabu sana,” alijikuta akitamka maneno hayo na kunifanya nimwangalie tena usoni.
Moyoni nikajikuta nikipata hamu ya kununua simu.
Niliingia ndani na kukuta mazingira kama niliyoyaacha, japokuwa kuna baadhi ya vitu vichache ambavyo Inana alikuwa amevinunua kwa kuibangaiza na vibarua.
Niliendelea kuishi huko kijijini kwa muda wa juma moja, ndipo nikaamua kurejea tena Dar es Salaam.
“Kwa hiyo mimi naondoka kesho.”

“Sawa dada, lakini mimi niko mpweke sana hapa nyumbani,” alisema Inana na kunifanya nijisikie uchungu mkubwa sana moyoni. Maneno yake yalinichoma kwa hisia kali mno. Nikanyanyuka mahali nilipokuwa nimekaa na kumfuata Inana. Nikamkumbatia kwa upendo.
Tulibaki tumekumbatiana kwa muda, huku kila mmoja akisikiliza mapigo ya moyo ya mwenzake. Ulikuwa ni usiku wa maumivu mno kwetu. Kwa muda wa juma moja tulilokaa pamoja, tulizoeana sana.
Lakini sikuwa na jinsi zaidi ya kurejea kwenye kazi yangu.

Siku hiyo tukafanya agano kubwa na la ajabu mno maishani.
“Inana,” nilimuita mdogo wangu huku nikibubujikwa machozi yaliyolowanisha mgongo wake. Hali kadhalika kwa upande wake, naye alikuwa analia huku akinilowanisha kwa machozi mgongoni mwangu.
“Na...aaamu dada,” aliitika kwa sauti iliyojaa kwikwi na kigugumizi cha machungu na maumivu makali sana.

“Acha niende, nakwenda kukuandalia mazingira ya kupata kazi, baadaye nitarejea kukuchukua ili tuwe pamoja Dar es Salaam kupambana na maisha,” nilisema maneno hayo kabla ya kutulia kidogo.
“Nitashukuru sana dada,” alisema Inana kwa sauti ya utulivu.
“Kitu kimoja nataka nikuambie.”
“Nakusikiliza dada.”
“Katika maisha yetu hatutakufa masikini,” nilisema huku nikijinasua mikononi mwake na kubaki tumetazamana.

Nikamwambia ni lazima tufikie vilele mbalimbali vya mafanikio maishani mwetu. Kwa pamoja tukaapa kupambana na maisha kwa kiwango cha juu mno. Umasikini uliokuwa umetuzunguka ulitutia uchungu mkubwa.
Kwa muda wa saa moja na dakika kadhaa, tulibaki tumeshikana mikono na kupeana faraja ya matumaini.

“Sawa dada, nimekuelewa lakini tutatumia njia gani kufanikiwa?” Inana aliniuliza huku akinitazama kwa umakini mkubwa.
“Ipo njia, nitakuambia kesho asubuhi,” nilimjibu kwa ujasiri hali iliyomfanya ashituke.


Je, nini kiliendelea? Usikose kufuatilia leo jioni....
 
Niliua kwa Kukusudia-12-

ILIPOISHIA :
Nikaelekea kwenye kituo cha kupanda mabasi hadi Ubungo ambako nilichukua gari la kwenda Chalinze. Niliwasili Chalinze saa tatu na nusu asubuhi. Nikapanda baiskeli hadi nyumbani.
“Aiii, jamani dada,” alisema Inana baada ya kuniona na kunikimbilia kwa furaha kubwa.
SASA ENDELEA...


Habari za huko jamani dada?”
“Nzuri, sijui wewe?”
“Salama jamani.”
“Za hapa nyumbani vipi?”

“Mm! Nipo nahangaika hivyohivyo, Mungu anasaidia sana.”
Nilimlipa yule mwendesha baiskeli ya kukodisha ujira wake. Akaondoka na kutuacha na Inana.
“Nilikukumbuka sana mdogo wangu.”
“Hata mimi dada, unaendeleaje huko Dar es Salaam?”

“Vizuri, ngoja nikikaa nitakusimulia yote. Kwa sasa ngoja nipumzike kidogo.”
Hali niliyoikuta nyumbani ilinitia simanzi. Kijumba kibovu kilikuwa kimezidi kujiinamia. Nikamuangalia Inana. Moyo uliniuma mno. Hakika niliumia kupita kiasi.
Nikashindwa kuingia ndani kwanza, nikawa nakikagua kile kijumba chetu kwa macho.

“Dada,” Inana aliniita huku akinisogelea baada ya kupeleka ndani kifurushi nilichokuwa nimebeba.
“Bee,” niliitika huku nikijifuta machozi kwa kiganja cha mkono wa kushoto.
“Kuna jambo nataka nikuambie,” alisema Inana na kunifanya nimuangalie kwa umakini ili nisikie alichokusudia kunieleza.

“Ha! Sasa mbona unalia tena dada?”
“Maisha mdogo wangu, maisha Inana.”
“Kwani hujafanikiwa kupata kazi ?”
“Siyo hivyo.”
“Sasa kumbe nini tena?”

“Hii hali Inana, inaniuma sana kuona tuko katika hali hii.”
“Mmh!” Inana aliishia kuguna.
“Hee, wewe Inana wewe.”
“Vipi dada.”
“Yaani siku hizi una simu?” nilimuuliza Inana kwa taharuki kubwa baada ya kuona ameshikilia simu kwa mkono wa kushoto.

“Mmh!, ina maana dada ndiyo umeiona sasa hivi?”
“Eee, nilikuwa sijaona kabisa umenunua simu!” nilisema huku nikikaa kwenye mfuko wa foronya uliokuwa karibu na mahali tulipokuwa.
Mshangao na maswali yangu mengi, yakamfanya Inana asahau alichotaka kuniambia baada ya kuniita.
Inana alikuwa amenunua simu aina ya sumsung. Ilikuwa ni fupi yenye mwanga wa njano kila ikiwaka.
“Nimebangaiza polepole kwa kujinyima dada, maisha ni magumu sana,” alinieleza Inana akiwa anaishika simu yake.

“Sasa inakusaidia nini kwa sasa,” nilimuuliza huku nikimkazia macho ya udadisi mkubwa.
“Inanisaidia kwa mambo mengi mno dada.”
“Kama yapi?”
“Kuna wakati vibarua huwa vya shida sana, ninalazimika kukaa nyumbani, lakini vikipatikana, watu mbalimbali wenye namba zangu hunipigia na kunitaarifu kuwa sasa vinapatikana,” Inana alinijibu kwa kirefu na kunifanya nimuelewe.

“Haya bwana, nimekuelewa.”
“Vipi huko mjini, maisha yanaendeleaje?”
“Mungu anasadia sana.”
“Aisee.”
“Unamkumbuka yule mwarabu aliyenigonga kwa gari wakati ule?”
“Ee dada.”

“Basi nilikutana naye.”
“Ha! Ikawaje sasa,” Inana aliniuliza kwa shauku ya kutaka kujua kilichojiri.
Nikamweleza jinsi nilivyokutana na yule mwarabu.
Hadi jinsi alivyonisaidia kupata kazi hotelini kwake. Inana alishangaa sana kusikia nafanya kazi kwenye hoteli ya yule mwarabu.

“Aisee Mungu ni wa ajabu sana,” alijikuta akitamka maneno hayo na kunifanya nimwangalie tena usoni.
Moyoni nikajikuta nikipata hamu ya kununua simu.
Niliingia ndani na kukuta mazingira kama niliyoyaacha, japokuwa kuna baadhi ya vitu vichache ambavyo Inana alikuwa amevinunua kwa kuibangaiza na vibarua.
Niliendelea kuishi huko kijijini kwa muda wa juma moja, ndipo nikaamua kurejea tena Dar es Salaam.
“Kwa hiyo mimi naondoka kesho.”

“Sawa dada, lakini mimi niko mpweke sana hapa nyumbani,” alisema Inana na kunifanya nijisikie uchungu mkubwa sana moyoni. Maneno yake yalinichoma kwa hisia kali mno. Nikanyanyuka mahali nilipokuwa nimekaa na kumfuata Inana. Nikamkumbatia kwa upendo.
Tulibaki tumekumbatiana kwa muda, huku kila mmoja akisikiliza mapigo ya moyo ya mwenzake. Ulikuwa ni usiku wa maumivu mno kwetu. Kwa muda wa juma moja tulilokaa pamoja, tulizoeana sana.
Lakini sikuwa na jinsi zaidi ya kurejea kwenye kazi yangu.

Siku hiyo tukafanya agano kubwa na la ajabu mno maishani.
“Inana,” nilimuita mdogo wangu huku nikibubujikwa machozi yaliyolowanisha mgongo wake. Hali kadhalika kwa upande wake, naye alikuwa analia huku akinilowanisha kwa machozi mgongoni mwangu.
“Na...aaamu dada,” aliitika kwa sauti iliyojaa kwikwi na kigugumizi cha machungu na maumivu makali sana.

“Acha niende, nakwenda kukuandalia mazingira ya kupata kazi, baadaye nitarejea kukuchukua ili tuwe pamoja Dar es Salaam kupambana na maisha,” nilisema maneno hayo kabla ya kutulia kidogo.
“Nitashukuru sana dada,” alisema Inana kwa sauti ya utulivu.
“Kitu kimoja nataka nikuambie.”
“Nakusikiliza dada.”
“Katika maisha yetu hatutakufa masikini,” nilisema huku nikijinasua mikononi mwake na kubaki tumetazamana.

Nikamwambia ni lazima tufikie vilele mbalimbali vya mafanikio maishani mwetu. Kwa pamoja tukaapa kupambana na maisha kwa kiwango cha juu mno. Umasikini uliokuwa umetuzunguka ulitutia uchungu mkubwa.
Kwa muda wa saa moja na dakika kadhaa, tulibaki tumeshikana mikono na kupeana faraja ya matumaini.

“Sawa dada, nimekuelewa lakini tutatumia njia gani kufanikiwa?” Inana aliniuliza huku akinitazama kwa umakini mkubwa.
“Ipo njia, nitakuambia kesho asubuhi,” nilimjibu kwa ujasiri hali iliyomfanya ashituke.


Je, nini kiliendelea? Usikose kufuatilia leo jioni....

Asante #mzizimkavu japo utamu unakuja mara unakata...wabeja(asante) kwa kisukuma
 
Niliua kwa Kukusudia-13-

ILIPOISHIA :
Kwa muda wa saa moja na dakika kadhaa, tulibaki tumeshikana mikono na kupeana faraja ya matuamaini.
"Sawa dada, nimekuelewa lakini tutatumia njia gani kufanikiwa?," Inana aliniuliza huku akinitazama kwa umakini mkubwa.
"Ipo njia, nitakuambia kesho asubuhi," nilimjibu kwa ujasiri hali iliyomfanya ashituke.
SASA ENDELEA..."


Mm!," Inana aliishia kuguna na kuendelea kunitazama.

"Basi tujiandae kulala mdogo wangu," nilimsemesha kwa sauti ya juu kidogo iliyompelekea kushituka kutokana na kuzama kwenye lindi kubwa la mawazo.
Inana alinielewa, sote tukaachaana na kuongozana hadi kulipokuwa na kijitanda chetu kilichochakaa na kutandikwa kwa matambara mabovu.
Tulipiga magozti na kumshukuru Mungu kwa kutujaalia afya njema kwa siku hiyo, pia tulimuomba atulinde kwa usiku huo, tuweze kuamka tukiwa wazima wa buheri wa afya.
Baada ya maombi, tulijitupa na kuanza kuusaka usingizi kwenye kitanda hicho cha kuchosha.
Tukiwa kitandani, tulisimulizana simulizi mbalimbali kuhusu maisha, pia tulijikumbusha mambo ya nyuma ikiwemo nyakati za shule. Ni hapo ndipo kila mmoja wetu alipatwa na majonzi mazito moyoni.
Tulijikuta tukipitiwa na usingizi hadi asubuhi. Nilikuwa wa kwanza kudamka, nikakaa kitako na kumuangalia Inana aliyekuwa bado anaufaidi usingizi wa asubuhi ulioambatana na kibaridi cha kisurisuri.
Nikawa nawaza ni kwa jinsi gani nitamtafutia Inana kazi huko mjini, angalau tuanze kusaidizana majukumu mbalimbali.
Tulikuwa na vita kubwa iliyokuwa mbele yetu, vita ya kupambana na umasikini uliokuwa umezonga na kutuzunguka kila mahali penye uwepo wetu.
Hakika tulikuwa tumezama na kutitia kwenye tope la ufukara. Hii ilitokana na kuondokewa na wazazi wetu ili hali akili zetu zilikuwa bado nyembamba.
Baada ya kuwaza na kuwazua mengi kuhusu maisha, hatimaye kulizidi kupambazuka. Mwanga wa jua ukaimulika nchi na kulifukuzia mbali giza lote. Kulikuwa na utulivu wa hali ya juu mno.
Nikatoka nje na kuchuchumaa mlangoni. Milio ya ndege waliokuwa wakiruka kutoka tawi moja kwenda jingine wakifurahia mapambazuko na mwanzo wa siku mpya ilikuwa ikisikika kwa ustadi mkubwa.
Nikiwa naendelea kusikilizia milio hiyo mitamu ya ndege wa aina mbalimbali, nilisikia Inana akiniita. Bila kuitikia niliingia ndani haraka na kumkuta akiwa amekaa huku akiwa ameshika simu yake.
"Vipi?," nilimuuliza huku nikimsikiliza kwa umakini.
"Umeamka saa ngapi jamani?."
"Sasa ndiyo salamu hiyo Inana?," nilimuuliza na kumkazia macho.
"Samahani dada, shikamoo," Inana alinisabahi kwa heshima na hali ya uoga kidogo iliyoashiria kujutia kosa lake la kuanzisha mazungumzo bila ya kujuliana hali.
"Marhaba, umeamkaje?"
"Sijambo tu, sijui wewe?"
"Salama, najiandaa kuondoka mapema hii."
Tulizungumza mengi, lakini Inana akanikumbusha juu ya vipi tutaweza kutokana na hali yetu ya umasikini iliyokuwa ikitukabili kwa kiasi kikubwa, kama nilivyomuahidi jana yake usiku wakati wa mazungumzo yetu maalumu.
"Na wewe husahau tu jamani?"
"Siwezi kusahau dada, si unajua ninavyouchukia umasikini huu."
"Sikiliza Inana, njia pekee bora ya kutusaidia sisi kuondokana na umasikini tulionao, ni kufanya kazi kwa nguvu na bidii zote, kuwa na nidhamu katika matumizi ya pesa pamoja na na kumtanguliza Mungu katika kila tulifanyalo.
"maana yeye ndiye nguzo muhimu sana maishani mwetu, na bila yeye hakuna linazoweza kufanyika chini ya jua, tupendane sisi kwa sisi, tuwaheshimu watu na kuwatendea yaliyo mema kama jinsi ambavyo tungependa kutendewa na watu," yalikuwa ni maneno mazito mno yalivyoonekana kumuingia vilivyo Inana.
Inana aliangalia juu, akashusha macho chini na kuvuta pumzi kwa nguvu na kuishusha taratibu.
"Dada Tunu," Inana aliniita kwa sauti ya uchungu huku machozi yakianza kutengeneza mifereji kwenye mboni za macho yake.



Je, nini kiliendelea? Fuatilia baadae
 
Niliua kwa Kukusudia-13-

ILIPOISHIA :
Kwa muda wa saa moja na dakika kadhaa, tulibaki tumeshikana mikono na kupeana faraja ya matuamaini.
“Sawa dada, nimekuelewa lakini tutatumia njia gani kufanikiwa?,” Inana aliniuliza huku akinitazama kwa umakini mkubwa.
“Ipo njia, nitakuambia kesho asubuhi,” nilimjibu kwa ujasiri hali iliyomfanya ashituke.
SASA ENDELEA...“


Mm!,” Inana aliishia kuguna na kuendelea kunitazama.

“Basi tujiandae kulala mdogo wangu,” nilimsemesha kwa sauti ya juu kidogo iliyompelekea kushituka kutokana na kuzama kwenye lindi kubwa la mawazo.
Inana alinielewa, sote tukaachaana na kuongozana hadi kulipokuwa na kijitanda chetu kilichochakaa na kutandikwa kwa matambara mabovu.
Tulipiga magozti na kumshukuru Mungu kwa kutujaalia afya njema kwa siku hiyo, pia tulimuomba atulinde kwa usiku huo, tuweze kuamka tukiwa wazima wa buheri wa afya.
Baada ya maombi, tulijitupa na kuanza kuusaka usingizi kwenye kitanda hicho cha kuchosha.
Tukiwa kitandani, tulisimulizana simulizi mbalimbali kuhusu maisha, pia tulijikumbusha mambo ya nyuma ikiwemo nyakati za shule. Ni hapo ndipo kila mmoja wetu alipatwa na majonzi mazito moyoni.
Tulijikuta tukipitiwa na usingizi hadi asubuhi. Nilikuwa wa kwanza kudamka, nikakaa kitako na kumuangalia Inana aliyekuwa bado anaufaidi usingizi wa asubuhi ulioambatana na kibaridi cha kisurisuri.
Nikawa nawaza ni kwa jinsi gani nitamtafutia Inana kazi huko mjini, angalau tuanze kusaidizana majukumu mbalimbali.
Tulikuwa na vita kubwa iliyokuwa mbele yetu, vita ya kupambana na umasikini uliokuwa umezonga na kutuzunguka kila mahali penye uwepo wetu.
Hakika tulikuwa tumezama na kutitia kwenye tope la ufukara. Hii ilitokana na kuondokewa na wazazi wetu ili hali akili zetu zilikuwa bado nyembamba.
Baada ya kuwaza na kuwazua mengi kuhusu maisha, hatimaye kulizidi kupambazuka. Mwanga wa jua ukaimulika nchi na kulifukuzia mbali giza lote. Kulikuwa na utulivu wa hali ya juu mno.
Nikatoka nje na kuchuchumaa mlangoni. Milio ya ndege waliokuwa wakiruka kutoka tawi moja kwenda jingine wakifurahia mapambazuko na mwanzo wa siku mpya ilikuwa ikisikika kwa ustadi mkubwa.
Nikiwa naendelea kusikilizia milio hiyo mitamu ya ndege wa aina mbalimbali, nilisikia Inana akiniita. Bila kuitikia niliingia ndani haraka na kumkuta akiwa amekaa huku akiwa ameshika simu yake.
“Vipi?,” nilimuuliza huku nikimsikiliza kwa umakini.
“Umeamka saa ngapi jamani?.”
“Sasa ndiyo salamu hiyo Inana?,” nilimuuliza na kumkazia macho.
“Samahani dada, shikamoo,” Inana alinisabahi kwa heshima na hali ya uoga kidogo iliyoashiria kujutia kosa lake la kuanzisha mazungumzo bila ya kujuliana hali.
“Marhaba, umeamkaje?”
“Sijambo tu, sijui wewe?”
“Salama, najiandaa kuondoka mapema hii.”
Tulizungumza mengi, lakini Inana akanikumbusha juu ya vipi tutaweza kutokana na hali yetu ya umasikini iliyokuwa ikitukabili kwa kiasi kikubwa, kama nilivyomuahidi jana yake usiku wakati wa mazungumzo yetu maalumu.
“Na wewe husahau tu jamani?”
“Siwezi kusahau dada, si unajua ninavyouchukia umasikini huu.”
“Sikiliza Inana, njia pekee bora ya kutusaidia sisi kuondokana na umasikini tulionao, ni kufanya kazi kwa nguvu na bidii zote, kuwa na nidhamu katika matumizi ya pesa pamoja na na kumtanguliza Mungu katika kila tulifanyalo.
“maana yeye ndiye nguzo muhimu sana maishani mwetu, na bila yeye hakuna linazoweza kufanyika chini ya jua, tupendane sisi kwa sisi, tuwaheshimu watu na kuwatendea yaliyo mema kama jinsi ambavyo tungependa kutendewa na watu,” yalikuwa ni maneno mazito mno yalivyoonekana kumuingia vilivyo Inana.
Inana aliangalia juu, akashusha macho chini na kuvuta pumzi kwa nguvu na kuishusha taratibu.
“Dada Tunu,” Inana aliniita kwa sauti ya uchungu huku machozi yakianza kutengeneza mifereji kwenye mboni za macho yake.



Je, nini kiliendelea? Fuatilia baadae

asante.....
 
Niliua kwa Kukusudia-14-

ILIPOISHIA
Inana aliangalia juu, akashusha macho na kuvuta pumzi kwa nguvu na kuzishusha taratibu.
"Dada Tunu," Inana aliniita kwa Sauti ya uchungu huku machozi yakianza kutengeneza mifereji kwenye mboni za macho yake.

SASA ENDELEA...

Huo ndiyo ukweli Inana, inabidi tukabiliane na maisha kwa kutumia silaha hii," niliendelea kumwambia mdogo wangu huku nikijiandaa kwa safari ya kurejea Dar.

Ilipofika saa moja na nusu asubuhi, niliagana rasmi na Inana nikimuahidi kumtafutia kazi maalum ya kujipatia kipato angalau kama kile cha kwangu kuliko kuendelea kuhangaika na vibarua kama alivyokuwa akifanya kwa wakati huo.
"Sawa dada, nitafurahi kama utafanya hivyo maana nimechoka kubangaiza na vibarua vya leo vipo kesho hamna," alisema Inana wakati akinitoa nyumbani kuelekea kwenye stendi ya Chalinze.
Alinisindikiza hadi nilipopata baiskeli ya kukodi kuelekea stendi ya mabasi ya Chalinze. Inana akarudi nami nikapanda. Wakati baiskeli ikianza safari, niligeuka na kumuangalia Inana ambaye naye alikuwa akigeuka nyuma kuniangalia kila mara. Tulikutanaisha macho na kujikuta tukiachiana tabasamu.
Kwangu halikuwa tabasamu la furaha, bali lilimaanisha huzuni na maumivu makali ya ugumu wa maisha uliokuwa ukitukabili mimi na mdogo wangu.
Sikuacha kugeuka nyuma na kumuangalia hadi alipopotea kabisa kwenye upeo wa mboni za macho yangu ndipo nikaamua kuendelea na safari yangu. Nusu saa baadaye, tukawasili kwenye stendi ya mabasi ya Chalinze ambapo nilimlipa mwendesha baiskeli ujira wake nami kuendelea na ratiba zangu za safari.
Nilisimama kwa muda nikingojea basi la kuelekea Dar na muda mfupi baadaye lilifika basi la Morogoro liitwalo Hood. Nikapanda na kukaa kwenye siti iliyokuwa imebaki kwa nyuma kabisa. Safari ikaanza. Njia nzima nilikuwa nikitafakari ni jinsi gani nitaweza kutimiza ahadi ya kumtafutia kazi Inana. Nikawa namuomba Mungu kimoyomoyo. Nikamwambia hakuna wakati niliokuwa namhitaji kama kipindi hicho cha magumu nilichokuwa nakipitia. Niliendelea kusali moyoni kwa imani kubwa.
Safari ikaendelea, tulipofika Kibaha nilianza kuhisi usingizi mzito ukininyemelea, nikawa najikaza lakini sikuweza, hatimaye nililala. Katikati ya usingizi huo mtamu, nilijiwa na ndoto ambayo hakika ilinijaza nguvu na matumaini makubwa mno maishani mwangu.
Katika ile ndoto, mimi na mdogo wangu tulikuwa tunaishi maisha ya kitajiri na kifahari kupita kiasi. Kila kitu kilikuwa kimebadilika na kubaki historia tu. Tulikuwa na ukwasi wa hali ya juu uliotokana na kufanya kazi kwa bidii. Katika utajiri wetu, asilimia ishirini tuliitoa kwa watoto yatima ambao kila tukiwaangalia walitukumbusha maisha yetu ya zamani.
Ndoto yangu ikazidi kukolea, lakini nikiwa naendelea kuifaidi, ghafla niliamshwa na sauti nzito ya mwanaume akiniambia tumefika hivyo niamke. Nilifumbua macho. Niliangaza huku na kule ndipo kupitia dirisha la basi hilo nikakutana na maandishi yaliyosomeka ‘Ubungo Bus Terminal'. Tayari tulikuwa tumewasili Dar. Haraka nikajiandaa na basi liliposimama vyema nikashuka na kimzigo changu.
Nikaanza kutoka ndani ya stendi na kuelekea kwenye kituo cha mabasi ya kwenda Buguruni nilikokuwa nikiishi. Nikajikokota kwa uvivu uliotokana na usingizi hadi nikavuka upande wa pili wa barabara na kunyoosha hadi karibu na eneo la daraja ambapo nilisimama na kungojea mabasi ya Ubungo Posta ili nikashukie Buguruni-Malapa.
Basi lilifika nami nikapanda. Nilipokaa kwenye siti sikuwa na mazungumzo na mtu yeyote zaidi ya kuwa kimya na kuanza kutafakari kwa kina ile ndoto. Baada ya kuzama ndani ya mawazo nilijikuta nikifurahia moyoni. Lakini nilipoyafikiria maisha niliyomuacha nayo mdogo wangu Inana pamoja na ninavyoishi kwa tabu na shida kule Buguruni kwa shangazi, furaha yote iliyeyuka.
Yalikuwa ni maisha yaliyoumiza mno. Basi likaanza safari na baada ya dakika chache tukawasili Buguruni-Malapa. Nikapiga hatua hadi nyumbani. Sikumkuta shangazi lakini kwa kuwa mlango ulikuwa ni wa kuegesha tu, sikupata tabu sana. Nilifungua na kuingia.
Kutokana na uchovu niliokuwa nao, nilijilaza kwenye kile kigodoro changu kichafu ambapo nilijikuta nikipitiwa na usingizi tena. Nilipoanza kusinzia tu, shangazi aliingia na kuniamsha.
"Habari za siku?"

"Nzuri," niliitikia huku nikifikicha macho yaliyokuwa na usingizi mzito.
"Bora umerudi, kuna kitu nataka nikujulishe kuhusu makazi tunayoishi hapa," shangazi aliniambia kwa uso wa huzuni na kunifanya nihisi kitu kisicho cha kawaida.


Fuatilia katika Baadae...............
 
Niliua kwa Kukusudia-14-

ILIPOISHIA
Inana aliangalia juu, akashusha macho na kuvuta pumzi kwa nguvu na kuzishusha taratibu.
“Dada Tunu,” Inana aliniita kwa Sauti ya uchungu huku machozi yakianza kutengeneza mifereji kwenye mboni za macho yake.

SASA ENDELEA...

Huo ndiyo ukweli Inana, inabidi tukabiliane na maisha kwa kutumia silaha hii,” niliendelea kumwambia mdogo wangu huku nikijiandaa kwa safari ya kurejea Dar.

Ilipofika saa moja na nusu asubuhi, niliagana rasmi na Inana nikimuahidi kumtafutia kazi maalum ya kujipatia kipato angalau kama kile cha kwangu kuliko kuendelea kuhangaika na vibarua kama alivyokuwa akifanya kwa wakati huo.
“Sawa dada, nitafurahi kama utafanya hivyo maana nimechoka kubangaiza na vibarua vya leo vipo kesho hamna,” alisema Inana wakati akinitoa nyumbani kuelekea kwenye stendi ya Chalinze.
Alinisindikiza hadi nilipopata baiskeli ya kukodi kuelekea stendi ya mabasi ya Chalinze. Inana akarudi nami nikapanda. Wakati baiskeli ikianza safari, niligeuka na kumuangalia Inana ambaye naye alikuwa akigeuka nyuma kuniangalia kila mara. Tulikutanaisha macho na kujikuta tukiachiana tabasamu.
Kwangu halikuwa tabasamu la furaha, bali lilimaanisha huzuni na maumivu makali ya ugumu wa maisha uliokuwa ukitukabili mimi na mdogo wangu.
Sikuacha kugeuka nyuma na kumuangalia hadi alipopotea kabisa kwenye upeo wa mboni za macho yangu ndipo nikaamua kuendelea na safari yangu. Nusu saa baadaye, tukawasili kwenye stendi ya mabasi ya Chalinze ambapo nilimlipa mwendesha baiskeli ujira wake nami kuendelea na ratiba zangu za safari.
Nilisimama kwa muda nikingojea basi la kuelekea Dar na muda mfupi baadaye lilifika basi la Morogoro liitwalo Hood. Nikapanda na kukaa kwenye siti iliyokuwa imebaki kwa nyuma kabisa. Safari ikaanza. Njia nzima nilikuwa nikitafakari ni jinsi gani nitaweza kutimiza ahadi ya kumtafutia kazi Inana. Nikawa namuomba Mungu kimoyomoyo. Nikamwambia hakuna wakati niliokuwa namhitaji kama kipindi hicho cha magumu nilichokuwa nakipitia. Niliendelea kusali moyoni kwa imani kubwa.
Safari ikaendelea, tulipofika Kibaha nilianza kuhisi usingizi mzito ukininyemelea, nikawa najikaza lakini sikuweza, hatimaye nililala. Katikati ya usingizi huo mtamu, nilijiwa na ndoto ambayo hakika ilinijaza nguvu na matumaini makubwa mno maishani mwangu.
Katika ile ndoto, mimi na mdogo wangu tulikuwa tunaishi maisha ya kitajiri na kifahari kupita kiasi. Kila kitu kilikuwa kimebadilika na kubaki historia tu. Tulikuwa na ukwasi wa hali ya juu uliotokana na kufanya kazi kwa bidii. Katika utajiri wetu, asilimia ishirini tuliitoa kwa watoto yatima ambao kila tukiwaangalia walitukumbusha maisha yetu ya zamani.
Ndoto yangu ikazidi kukolea, lakini nikiwa naendelea kuifaidi, ghafla niliamshwa na sauti nzito ya mwanaume akiniambia tumefika hivyo niamke. Nilifumbua macho. Niliangaza huku na kule ndipo kupitia dirisha la basi hilo nikakutana na maandishi yaliyosomeka ‘Ubungo Bus Terminal’. Tayari tulikuwa tumewasili Dar. Haraka nikajiandaa na basi liliposimama vyema nikashuka na kimzigo changu.
Nikaanza kutoka ndani ya stendi na kuelekea kwenye kituo cha mabasi ya kwenda Buguruni nilikokuwa nikiishi. Nikajikokota kwa uvivu uliotokana na usingizi hadi nikavuka upande wa pili wa barabara na kunyoosha hadi karibu na eneo la daraja ambapo nilisimama na kungojea mabasi ya Ubungo Posta ili nikashukie Buguruni-Malapa.
Basi lilifika nami nikapanda. Nilipokaa kwenye siti sikuwa na mazungumzo na mtu yeyote zaidi ya kuwa kimya na kuanza kutafakari kwa kina ile ndoto. Baada ya kuzama ndani ya mawazo nilijikuta nikifurahia moyoni. Lakini nilipoyafikiria maisha niliyomuacha nayo mdogo wangu Inana pamoja na ninavyoishi kwa tabu na shida kule Buguruni kwa shangazi, furaha yote iliyeyuka.
Yalikuwa ni maisha yaliyoumiza mno. Basi likaanza safari na baada ya dakika chache tukawasili Buguruni-Malapa. Nikapiga hatua hadi nyumbani. Sikumkuta shangazi lakini kwa kuwa mlango ulikuwa ni wa kuegesha tu, sikupata tabu sana. Nilifungua na kuingia.
Kutokana na uchovu niliokuwa nao, nilijilaza kwenye kile kigodoro changu kichafu ambapo nilijikuta nikipitiwa na usingizi tena. Nilipoanza kusinzia tu, shangazi aliingia na kuniamsha.
“Habari za siku?”

“Nzuri,” niliitikia huku nikifikicha macho yaliyokuwa na usingizi mzito.
“Bora umerudi, kuna kitu nataka nikujulishe kuhusu makazi tunayoishi hapa,” shangazi aliniambia kwa uso wa huzuni na kunifanya nihisi kitu kisicho cha kawaida.


Fuatilia katika Baadae...............

poa ndg
 
Niliua kwa Kukusudia-15-

ILIPOISHIA

Kutokana na uchovu niliokuwa nao, nilijilaza kwenye kile kigodoro changu kichafu ambapo nilijikuta nikipitiwa na usingizi tena.


Nilipoanza kusinzia tu, shangazi aliingia na kuniamsha.

"Habari za siku?"
"Nzuri," niliitikia huku nikifikicha macho yaliyokuwa na usingizi mzito.
"Bora umerudi, kuna kitu nataka nikujulishe kuhusu makazi tunayoishi hapa..."

SASA ENDELEA...


Shangazi alitulia kidog kisha kukohoa. Akanitazama usoni kwa macho ya mkazo kidogo. Wasiwasi ukazidi kuniingia moyoni. Hata hivyo, nilijikaza na kuwa tayari kupokea jambo lolote nitakaloambiwa na shangazi kwa wakati huo.

"Sisi tunaoishi eneo hili," Shangazi akaendelea nami nikajiweka sawa mahali nilipokuwa nimejilaza. Nikakaa kitako na kujiegemeza ukutani na kuanza kumsikiliza kwa umakini mkubwa shangazi.
"Tunaishi kwa kulipia vibanda hivi, sasa kwa kuwa tuko wawili hapa mimi na wewe, na madamu sasa umeshaanza kujipatia riziki, ni vyema sasa kama tutaanza kushirikiana katika ulipaji wa kodi ya pango hili," Shangazi alihitimisha mazungumzo yake na kuniangalia usoni huku akisikilizia kama nilikuwa na chochote cha kuzungumza juu ya hilo.
"Sawa shangazi, nimekusikia," nilimjibu kwa sauti ya upole na yenye utulivu wa hali ya juu mno.
"Nashukuru kama utakuwa umenielewa," alijibu shangazi.

"Nimekuelewa vizuri sana, vipi habari za hapa nyumbani jamani, maana hata hatujasalimiana kwa undani zaidi ya wewe kuleta mada ya kodi ya pango," nilijikuta nikitamka maneno hayo kwa ujasiri mkubwa ambao sikujua ulitokana na nini.
"Kama nilivyosema hapo awali, hapa nyumbani ni salama kabisa kama ulivyopaacha."
"Kama ni hivyo, ni jambo jema la kumshukukuru Mungu wa Mbinguni."
"Vipi wewe na safari yako, ulifika salama?"
"Nilifika salama kabisa."

"Inana anaendeleaje kwa sasa huko kijijini?"
"Anaendelea vizuri tu."
"Inaonekana kwa sasa ni binti mkubwa sana, maana sijamuona kwa muda mrefu sasa."
"Aah, mbona ni mama mkubwa sasa," nilimjibu Shangazi na wote tukaangua kicheko kilichoashiria furaha kubwa baina yetu.

Baada ya mazungumzo ya kuchangamshana, shangazi akatoka nje na kuniacha peke yangu kwenye kigodoro changu. Nikaendelea kukaa huku maswali mengi yakipita ubongoni mwangu kwa kasi.
Nikawa najiuliza mambo mengi sana kuhusu kauli ya shangazi. Lakini nikajipa moyo kuwa nitaweza kugharamia kodi ya pango kutokana na kipato changu cha kibarua cha hotelini. Nikaendelea kuwaza ndipo katika hali ya kuwaza na kuwazua, nikajikuta nikipata wazo ambalo hakika sikujua lilitoka wapi kwa wakati huo.
Nikawaza kuwa hata kama nitasaidizana na shangazi katika kulipia kodi ya pango la kibanda hicho, sitachukua muda mrefu kabla sijapanga chumba changu mwenyewe.
Wazo hilo likaendelea kuchukua nafasi kubwa sana kichwani mwangu. Nikakubaliana na wazo hilo kuwa nikusanye pesa kwa juhudi zote, ili niweze kupata kiasi cha kukodisha chumba na kuyaanza maisha yangu pamoja na mdogo wangu Inana.
Baadaye, nilitoka nje ambapo tayari ilishafika jioni kabisa. Nikaa kwa nje huku nikiendelea kuwaza.
Usiku ulipotimu, nilikuwa wa kwanza kuingia ndani na kujilaza tena kwenye kigodoro. Shangazi alikuja kuniamsha baada ya kuivisha na kuniomba tujumuike sote kwenye chakula cha pamoja.

Sikuwa na hiyana, nikajikokota kwa uvivu hadi mahali alipokuwa ametenga chakula. Tukaanza kula huku tukisimulizana mambo mbalimbali na kuambatanisha mazungumzo hayo kwa vicheko vya furaha.
Tulipomaliza kula, niliondoa vyombo vyote na kuvikusanyia kwenye chombo kimoja kikubwa na kuanza kuviosha. Baada ya kumaliza zoezi hilo, nikavipanga mahali pake nami nikaelekea kulala. Nikaanza kuusakama usingizi japo kwa taabu sana. Ukawa unakuja kwa mang'amung'amu tu. Mara nyingi nilikuwa nikishituka na kuketi kitako kutokana na mawazo.
Hadi kunapambazuka, sikuwa nimesinzia hata kidogo. Nikaamka na kumsabahi shangazi ambaye hadi wakati huo alikuwa bado akiusindikiza usngizi wa mwisho wenye kibaridi cha asubuhi.
Nikajiandaa ili niende kazini kwani siku za kupumzika zilikuwa zimekwisha. Baada ya kumaliza kuoga, nilivaa na kutoka kuelekea kwenye kituo cha mabasi ya kuelekea Mwananyamala. Nilipowasili kituoni, nikiwa naendelea kusubiri basi ghafla nilikumbuka kitu ambacho kiliniondolea kabisa raha ya siku hiyo.


Je, kijana huyo alikumbuka kitu gani? Usikose kufuatilia
 
Niliua kwa Kukusudia-16-


ILIPOISHIA:
Nikajiandaa ili niende kazini kwani siku za kupumzika zilikuwa zimekwisha. Baada ya kumaliza kuoga, nilivaa na kutoka kuelekea kwenye kituo cha mabasi ya kwenda Mwananyamala. Nilipowasili kituoni, nikiwa naendelea kusubiri basi, ghafla nilikumbuka kitu ambacho kiliniondolea kabisa raha ya siku hiyo.
SASA ENDELEA…


NILIKUMBUKA yale mazungumzo ya shangazi. Nilikosa raha kabisa. Lakini nikajipa moyo na kuamua kupambana na kila hali ya ugumu wa maisha itakayojitokeza mbele yangu. Kwa mbali nilianza kukichukia sana kifo, kwani bila hicho wazazi wangu wangekuwa hai. Mimi na mdogo wangu Inana tungekuwa tunaendelea na masomo.

‘Lakini ngoja nijikaze, kwani sina budi kupambana na maisha, imeshakuwa hivyo sasa sina jinsi lakini mwisho wa siku ni lazima nifanikiwe, siko tayari kufa nikiwa maskini', nilijikuta nikiwaza maneno hayo mazito na makali.
Niliendelea kungojea usafiri, muda mfupi lilikuja basi la UDA lililokuwa likielekea Mwananyamala. Nikajipakia na kuketi kiti cha nyuma kabisa nikiwa peke yangu. Kama kawaida sikupata muda wa kufurahia jambo lolote, nikaendelea na mawazo yangu.
Basi lilifika Mwananyamala-Kwakopa majira ya saa mbili na dakika 45, nikashuka na kumpatia kondakta pesa yake. Nilijikokota hadi hotelini kwenye kibarua changu. Nilikuta baadhi ya wafanyakazi wameshaanza kuwasili. Tulisabahiana kwa furaha kutokana na kukaa muda mrefu bila kuonana. Kila mtu alikuwa mwenye furaha.
Nikaenda kujiandaa ili nivalie nguo za kazi. Nikiwa nakaribia kabisa na mlango wa chumba cha kubadilishia nguo, nilisikia sauti ya mtu ikiniita kwa nyuma. Nikageuka na kuangalia kwa haraka. Alikuwa ni mfanyakazi mwenzangu, Sauda.
"Ah, Sauda habari za asubuhi?"
"Salama Tunu, hujambo?"
"Salama kabisa, sijui wewe?"
"Salama tu," nilimjibu huku nikitaka kuendelea na safari ya kuingia ndani ili nibadilishe nguo.
Nilipopiga hatua ya kwanza, Sauda aliniita tena na kunifanya nirudi na kumsogelea kwa karibu kwani nilihisi alikuwa na jambo alitaka kunieleza.

"Samahani Tunu."
"Bila samahani Sauda, nakusikiliza."
"Bosi anakuita."
"Bosi yupi, meneja au mkurugenzi?"
"Mkurugenzi."
"Yuko ofisini?"
"Ndiyo," Sauda alinijibu huku akigeuka na kuniacha nikitafakari nilichoitiwa asubuhi ile na yule Mwarabu.

Baada ya kuwaza kwa muda, nikajipa moyo na kuamua kwenda ofisini kumsikiliza yule Mwarabu ambaye kwa wakati huo nilikuwa nimeshamjua kwa jina kutokana na kusikia baadhi ya wafanyakazi akiwemo meneja. Alikuwa akiitwa Elihakimu.
Nikaingia ofisini kwa heshima na woga kwa mbali. Kule ofisini, nilikuta akivuta sigara huku akiwa amesimama na kushika simu mkononi. Kwenye kiti cha wageni kulikuwa na kijana mmoja ambaye naye alikuwa Mwarabu pia, kwa mbali walifanana japo si kwa sana.
"Ooh, karibu sana Tunu, habari za siku?"
"Salama, shikamoo."

"Marahaba, hujambo kabisa Tunu?" alinisabahi kwa uchangamfu wa hali ya juu sana Elihakimu.
Baada ya kumsalimia, nikamgeukia yule mgeni aliyekuwa kimya kabisa naye akiendelea kuvuta sigara.
"Shikamoo."
"Marahaba binti, hujambo?"
"Salama kabisa."

"Kaa hapo Tunu," akaniambia Elihakimu na kunionesha moja ya viti vilivyokuwemo ofisini humo.
Akaendelea kuvuta sigara na kutoa moshi mwingi sana kupitia tundu za pua na mdomoni. Akavuta hadi kilipobaki kipisi alikiminya kwenye kile kifaa kilichokuwa juu ya meza cha kuzimia sigara.
Akaketi na kutuangalia kwa zamu mimi na yule mgeni mwigine Mwarabu.
"Tunu," alininiita na kunikazia macho.

"Bee."
"Huyu ni mdogo wangu."
"Sawa."
"Anaitwa Ashraf."
"Nimefurahi kumuona," nilimjibu ambapo maneno yangu yalimfanya yule Mwarabu mgeni aniangalie kwa furaha ya wazi.

Bosi aliendelea na utambulisho ambapo alieleza hadi jinsi nilivyofahamiana naye.
Mazungumzo yakaendelea. Wakati bosi anaendelea na kuratibu kikao hicho, mlango ulifunguliwa. Akatokeza yule mhudumu wa mapokezi akiwa ameshika sinia lililokuwa na vikombe na birika la kahawa na baadhi ya vitafunwa. Akavitenga mezani kisha kuanza kumnawisha yule mgeni, baadaye bosi. Alikupokuja kwa upande wangu. Nilikataa kwa kisingizio kuwa nilikuwa nimeshiba.

Bosi na yule mgeni walinisisitizia kwa hamasa kubwa. Nikajikuta nimekubali na kunawa. Yule mhudumu akatumiminia kahawa na kutuwekea sawa vitafunwa. Akatukaribisha. Alipoondoka tu, bosi Elihakimu alinigeukia.
"Tunu."
"Abee, bosi."
"Huyu mdogo wangu ana shida ambayo naamini utaweza kumsaidia, najua huwezi kuniangusha
.

Je, ni shida gani hiyo? Usikose kufuatilia baadae leo jioni....
"
 
Back
Top Bottom