Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 43,037
- 34,741
- Thread starter
- #41
Niliua kwa Kukusudia -9-
ILIPOISHIA :
"Unaitwa nani vile?"
"Tunu, kwani vipi?"
"Nilitaka tufahamiane, mimi naitwa
Hemed."
"Nashukuru kukufahamu," nilimjibu
huku nikianza kupiga hatua kuendelea na
safari yangu.
"Kuna jambo moja nataka nikuulize."
"Jambo gani tena?" Nikamuuliza kwa
sauti ya juu na ukali kidogo kutokana na
uchovu pamoja na mawazo niliyokuwa
nayo. ENDELEA SASA…
Ukali wangu ulimfanya yule kijana kunyamaza kidogo. Akakosa neno la kuongeza, nami nikaendelea na safari yangu.
Nikatembea hatua chache kabla ya kufika eneo la kupandia mabasi ya Ubungo ambapo baadaye nilitakiwa nikapande tena mabasi ya Buguruni.
Nilipofika kwenye kituo hicho, nikaungana na abiria wenzangu waliokuwa wakisubiri mabasi. Nikajitenga pembeni kidogo.
Muda mfupi baadaye, yalifika mabasi mawili ya kuelekea Ubungo. Nikapanda mojawapo na kuketi kiti cha nyuma kabisa ambapo niliendelea kuwa mkimya sana.
Mawazo yaliendelea kuisumbua akili yangu. Nikaendelea kumkumbuka sana mdogo wangu. Inana.
Niliendelea kuzama kwenye lindi la mawazo hadi niliposhtuliwa na sauti ya kondakta aliyekuwa akiomba nauli yake baada ya basi hilo kuwasili kituo cha Ubungo.
"Oyaa wewe sista, nipe changu bwana."
"Sawa jamani," nilimjibu yule kondakta huku nikimkabidhi nauli yake.
"Hayo ndiyo mambo," alisema yule kondakta lakini sikumjali zaidi ya kushuka na kuelekea kwenye kituo cha kusubiria mabasi ya kuelekea Buguruni.
Kutokana na wingi wa watu kituoni hapo, abiria wengi walikuwa wakigombania mabasi. Nami nikaungana nao nikiwa na mkoba wangu begani. Niliuangalia kwa uangalifu wa hali ya juu mno.
Baada ya pilikapilika ya kugombania mabasi, nilibahatika kupata basi moja na kukaa kwenye kiti ambapo niliendelea kuwa kimya huku msongo wa mawazo ukizidi kuniandama.
Nilifika nyumbani jioni sana kutokana na foleni ndefu iliyokuwepo kwa siku hiyo. Nilikuwa nimechoka kweli.
"Naona mwenzangu sasa mambo yameanza kukuendea sawa," shangazi aliniuliza baada ya kusalimiana na kujuliana hali tangu tuachane nyakati za asubuhi.
"Afadhali kidogo, Mungu ameanza kuonesha mwanga," nilimjibu lakini kwa sauti iliyoashira uchovu mno.
"Umeanza kazi?"
"Ndiyo shangazi."
Baada ya kubadilishana mawazo na shangazi, niliingia chumbani ambapo nilitandika jamvi langu la kulalia lililokuwa limechakaa kupindukia.
Sijui ni saa ngapi nilipitiwa na usingizi, nilishituka ikiwa tayari ni asubuhi.
Nilimsabahi shangazi aliyekuwa tayari anajiandaa kwa biashara zake za mama ntilie.
Haraka sana nikaingia bafuni. Nikaoga pamoja na kusukutua mswaki kabla ya kujiandaa kwa safari ya kurejea kazini ili niwahi majukumu ya usafi nitakayopangiwa kwa siku hiyo.
"Haya kwaheri shangazi."
"Haya basi, baadaye," shangazi alinijibu lakini kwa sauti iliyojaa utulivu mno.
Nikawahi hadi kituo cha mabasi ya Ubungo. Nikawasili na kuunganisha hadi Mwananyamala, eneo langu jipya la kazi.
Niliendelea na kazi za usafi hotelini hapo kwa siku kadhaa bila kuona dalili yoyote ya kubadilishiwa nafasi nyingine ya kazi. Hata hivyo sikukata tamaa hata kidogo. Nikaendelea kujipa matumaini huku Mungu akiendelea kuwa nguzo na tegemeo langu kuu.
Kawaida wafanyakazi wote wa hotelini hapo walikuwa na desturi ya kubadilishana siku ya kupumzika kwa siku nne mfululizo baada ya kuingia kazini kwa muda wa majuma mawili mfululizo.
Siku moja nilipokuwa naingia kazini asubuhi, nilimkuta yule Mwarabu amesimama pembeni mwa lango kuu la kuingilia hotelini hapo.
Tofauti na siku nyingine nilizokuwa nimemzoea kwa ukarimu wake, siku hiyo hakuwa mwenye furaha kabisa. Wajihi wake ulionekana kugubikwa kwa mawazo tele.
"Salama, za kwako," aliniitikia kwa sauti ya chini baada ya kumsabahi.
Nilipompita nikiwa naelekea eneo la kubadilishia nguo kabla ya kuanza kazi, nilisikia akiniita.
"Naamu," niliitikia kwa uoga kidogo.
"Njoo. Unaendeleaje na kazi," aliniuliza akiwa amenikazia sana macho.
"Vizuri tu bosi," nilimjibu kwa utulivu.
"Mbona kama…"
"Hebu njoo ofisini kwangu," aliniambia huku akipiga hatua kuelekea ofisini ambapo nami nilimfuata.
Je, nini kitafuata? Fuatilia Kesho Usiku.
ILIPOISHIA :
"Unaitwa nani vile?"
"Tunu, kwani vipi?"
"Nilitaka tufahamiane, mimi naitwa
Hemed."
"Nashukuru kukufahamu," nilimjibu
huku nikianza kupiga hatua kuendelea na
safari yangu.
"Kuna jambo moja nataka nikuulize."
"Jambo gani tena?" Nikamuuliza kwa
sauti ya juu na ukali kidogo kutokana na
uchovu pamoja na mawazo niliyokuwa
nayo. ENDELEA SASA…
Ukali wangu ulimfanya yule kijana kunyamaza kidogo. Akakosa neno la kuongeza, nami nikaendelea na safari yangu.
Nikatembea hatua chache kabla ya kufika eneo la kupandia mabasi ya Ubungo ambapo baadaye nilitakiwa nikapande tena mabasi ya Buguruni.
Nilipofika kwenye kituo hicho, nikaungana na abiria wenzangu waliokuwa wakisubiri mabasi. Nikajitenga pembeni kidogo.
Muda mfupi baadaye, yalifika mabasi mawili ya kuelekea Ubungo. Nikapanda mojawapo na kuketi kiti cha nyuma kabisa ambapo niliendelea kuwa mkimya sana.
Mawazo yaliendelea kuisumbua akili yangu. Nikaendelea kumkumbuka sana mdogo wangu. Inana.
Niliendelea kuzama kwenye lindi la mawazo hadi niliposhtuliwa na sauti ya kondakta aliyekuwa akiomba nauli yake baada ya basi hilo kuwasili kituo cha Ubungo.
"Oyaa wewe sista, nipe changu bwana."
"Sawa jamani," nilimjibu yule kondakta huku nikimkabidhi nauli yake.
"Hayo ndiyo mambo," alisema yule kondakta lakini sikumjali zaidi ya kushuka na kuelekea kwenye kituo cha kusubiria mabasi ya kuelekea Buguruni.
Kutokana na wingi wa watu kituoni hapo, abiria wengi walikuwa wakigombania mabasi. Nami nikaungana nao nikiwa na mkoba wangu begani. Niliuangalia kwa uangalifu wa hali ya juu mno.
Baada ya pilikapilika ya kugombania mabasi, nilibahatika kupata basi moja na kukaa kwenye kiti ambapo niliendelea kuwa kimya huku msongo wa mawazo ukizidi kuniandama.
Nilifika nyumbani jioni sana kutokana na foleni ndefu iliyokuwepo kwa siku hiyo. Nilikuwa nimechoka kweli.
"Naona mwenzangu sasa mambo yameanza kukuendea sawa," shangazi aliniuliza baada ya kusalimiana na kujuliana hali tangu tuachane nyakati za asubuhi.
"Afadhali kidogo, Mungu ameanza kuonesha mwanga," nilimjibu lakini kwa sauti iliyoashira uchovu mno.
"Umeanza kazi?"
"Ndiyo shangazi."
Baada ya kubadilishana mawazo na shangazi, niliingia chumbani ambapo nilitandika jamvi langu la kulalia lililokuwa limechakaa kupindukia.
Sijui ni saa ngapi nilipitiwa na usingizi, nilishituka ikiwa tayari ni asubuhi.
Nilimsabahi shangazi aliyekuwa tayari anajiandaa kwa biashara zake za mama ntilie.
Haraka sana nikaingia bafuni. Nikaoga pamoja na kusukutua mswaki kabla ya kujiandaa kwa safari ya kurejea kazini ili niwahi majukumu ya usafi nitakayopangiwa kwa siku hiyo.
"Haya kwaheri shangazi."
"Haya basi, baadaye," shangazi alinijibu lakini kwa sauti iliyojaa utulivu mno.
Nikawahi hadi kituo cha mabasi ya Ubungo. Nikawasili na kuunganisha hadi Mwananyamala, eneo langu jipya la kazi.
Niliendelea na kazi za usafi hotelini hapo kwa siku kadhaa bila kuona dalili yoyote ya kubadilishiwa nafasi nyingine ya kazi. Hata hivyo sikukata tamaa hata kidogo. Nikaendelea kujipa matumaini huku Mungu akiendelea kuwa nguzo na tegemeo langu kuu.
Kawaida wafanyakazi wote wa hotelini hapo walikuwa na desturi ya kubadilishana siku ya kupumzika kwa siku nne mfululizo baada ya kuingia kazini kwa muda wa majuma mawili mfululizo.
Siku moja nilipokuwa naingia kazini asubuhi, nilimkuta yule Mwarabu amesimama pembeni mwa lango kuu la kuingilia hotelini hapo.
Tofauti na siku nyingine nilizokuwa nimemzoea kwa ukarimu wake, siku hiyo hakuwa mwenye furaha kabisa. Wajihi wake ulionekana kugubikwa kwa mawazo tele.
"Salama, za kwako," aliniitikia kwa sauti ya chini baada ya kumsabahi.
Nilipompita nikiwa naelekea eneo la kubadilishia nguo kabla ya kuanza kazi, nilisikia akiniita.
"Naamu," niliitikia kwa uoga kidogo.
"Njoo. Unaendeleaje na kazi," aliniuliza akiwa amenikazia sana macho.
"Vizuri tu bosi," nilimjibu kwa utulivu.
"Mbona kama…"
"Hebu njoo ofisini kwangu," aliniambia huku akipiga hatua kuelekea ofisini ambapo nami nilimfuata.
Je, nini kitafuata? Fuatilia Kesho Usiku.