chai ya rangi
Senior Member
- Mar 7, 2026
- 130
- 403
Hii ni story yangu na nitatoa na mifano ya vitu nilivyowahi kufanya. Watu wengi hawakujua, lakini kuna matukio kadhaa yaliyotokea nikiwa mtoto ambayo hayakuwa ya kawaida kabisa. Haikuwa mara moja ilikuwa vitu ambavyo vilitokea mbele ya watu wengine pia.
Mfano wa kwanza ulikuwa mvua.
Kuna siku anga lilikuwa wazi kabisa. Hakukuwa na dalili ya mvua hata kidogo. Nilisimama nje nikaangalia juu halafu nikasema tu mvua inyeshe. Baada ya muda mfupi, mawingu yakaanza kukusanyika polepole, upepo ukabadilika, halafu mvua ikanesa. Watu walishangaa lakini hawakujua nini kilitokea dakika chache kabla.
Mfano wa pili ulitokea nyumbani.
Kuna siku taa ya chumbani ilikuwa imeharibika kabisa, haikuwaka hata kidogo. Watu walijaribu kuigusa mara kadhaa bila mafanikio. Nilishika tu swichi nikasema iwake, na ghafla taa ikawaka kama kawaida.
Watu walikaa kimya kwa muda.
Mfano wa tatu ulitokea nilipokuwa nje nacheza.
Kulikuwa na kitu kidogo nilichokuwa nacho mkononi kama sarafu. Niliitupa juu halafu kwa sekunde chache ilikaa hewani bila kuanguka mara moja. Ilikuwa kama imesimama kidogo hewani kabla haijarudi chini. Watu wawili waliokuwa karibu waliona hilo.
Walishangaa sana.
Mfano wa nne ndio uliwashangaza zaidi watu wazima.
Kulikuwa na glasi iliyoanguka na kuvunjika vipande vipande. Nilivikusanya vile vipande nikaviweka pamoja, nikavishika kwa mikono yangu kwa sekunde chache… halafu vile vipande vilikaa pamoja tena kama havikuvunjika kabisa.
Watu waliokuwa pale hawakuongea kwa muda.
Na mfano wa tano ndio ulionifanya nijue uwezo huo ulikuwa wa kweli.
Nikikia na uwezo wa kufungua madirisha au milango kwa kuiangalia tu kwa macho na kuifikiria ikiwa inafunguka au kufunga nayo inafanya hivyohivyo kama nilivyoifikiria akilini.
Baada ya hapo, mambo hayo yalianza kupungua polepole kadri nilivyokuwa nakua.
Mpaka sasa ni nadra naona kama yamepotea.
Lakini ukweli ni kuwa…
nilipokua mdogo miujiza ilikuwa inatokea mbele yangu, na wakati mwingine mikononi mwangu kabisa.
Mfano wa kwanza ulikuwa mvua.
Kuna siku anga lilikuwa wazi kabisa. Hakukuwa na dalili ya mvua hata kidogo. Nilisimama nje nikaangalia juu halafu nikasema tu mvua inyeshe. Baada ya muda mfupi, mawingu yakaanza kukusanyika polepole, upepo ukabadilika, halafu mvua ikanesa. Watu walishangaa lakini hawakujua nini kilitokea dakika chache kabla.
Mfano wa pili ulitokea nyumbani.
Kuna siku taa ya chumbani ilikuwa imeharibika kabisa, haikuwaka hata kidogo. Watu walijaribu kuigusa mara kadhaa bila mafanikio. Nilishika tu swichi nikasema iwake, na ghafla taa ikawaka kama kawaida.
Watu walikaa kimya kwa muda.
Mfano wa tatu ulitokea nilipokuwa nje nacheza.
Kulikuwa na kitu kidogo nilichokuwa nacho mkononi kama sarafu. Niliitupa juu halafu kwa sekunde chache ilikaa hewani bila kuanguka mara moja. Ilikuwa kama imesimama kidogo hewani kabla haijarudi chini. Watu wawili waliokuwa karibu waliona hilo.
Walishangaa sana.
Mfano wa nne ndio uliwashangaza zaidi watu wazima.
Kulikuwa na glasi iliyoanguka na kuvunjika vipande vipande. Nilivikusanya vile vipande nikaviweka pamoja, nikavishika kwa mikono yangu kwa sekunde chache… halafu vile vipande vilikaa pamoja tena kama havikuvunjika kabisa.
Watu waliokuwa pale hawakuongea kwa muda.
Na mfano wa tano ndio ulionifanya nijue uwezo huo ulikuwa wa kweli.
Nikikia na uwezo wa kufungua madirisha au milango kwa kuiangalia tu kwa macho na kuifikiria ikiwa inafunguka au kufunga nayo inafanya hivyohivyo kama nilivyoifikiria akilini.
Baada ya hapo, mambo hayo yalianza kupungua polepole kadri nilivyokuwa nakua.
Mpaka sasa ni nadra naona kama yamepotea.
Lakini ukweli ni kuwa…
nilipokua mdogo miujiza ilikuwa inatokea mbele yangu, na wakati mwingine mikononi mwangu kabisa.