kiss ov love
JF-Expert Member
- Jan 21, 2025
- 9,363
- 16,092
Kuna kijana alikuja kupata huduma ofisini kwetu akawa amechukua namba yangu yeye ana ofisi yake huko town anauza viatu vya kike.
Mwanzoni alikuwa mpole tukawa tunawasiliana vizuri tu, kwa vile ana ofisi yake nikajua atanipa ushauri mzuri wa biashara na kujiajiri hivyo nikawa nimemuamini, na kumchukulia kama kaka au rafiki wa kiume.
Ikatokea siku akanialika kwake nikitoka kazini, kwakuwa siyo mbali na ofisini kwetu nilivyotoka nikaenda, tukakaa tukapiga story tukala chakula, baada ya hapo nashangaa mtu mara anisogelee atake kunishika, akaninyanyua kanipeleka chumbani weee hapa nilibadilika nikawa mbogo, maana mimi sikujia hayo mambo iweje atake kunibaka bila ridhaa yangu kisa nimekuja kwake ndiyo aone kuwa nimekubali kila kitu.
Tulivutana sana hiyo siku nakumbuka, mimi hadi nimefura kwa hasira ndiyo kumlazimisha akanipeleka home maana ana usafiri wake, tangu hiyo siku nimetoka sijapokea simu yake wala kujibu meseji zake, nimemuona ni mwanaume wa hovyo sana tangu lini mapenzi yakalazimishwa? Mwache mwanamke akupe kwa kuridhia mwenyewe.
Mwanzoni alikuwa mpole tukawa tunawasiliana vizuri tu, kwa vile ana ofisi yake nikajua atanipa ushauri mzuri wa biashara na kujiajiri hivyo nikawa nimemuamini, na kumchukulia kama kaka au rafiki wa kiume.
Ikatokea siku akanialika kwake nikitoka kazini, kwakuwa siyo mbali na ofisini kwetu nilivyotoka nikaenda, tukakaa tukapiga story tukala chakula, baada ya hapo nashangaa mtu mara anisogelee atake kunishika, akaninyanyua kanipeleka chumbani weee hapa nilibadilika nikawa mbogo, maana mimi sikujia hayo mambo iweje atake kunibaka bila ridhaa yangu kisa nimekuja kwake ndiyo aone kuwa nimekubali kila kitu.
Tulivutana sana hiyo siku nakumbuka, mimi hadi nimefura kwa hasira ndiyo kumlazimisha akanipeleka home maana ana usafiri wake, tangu hiyo siku nimetoka sijapokea simu yake wala kujibu meseji zake, nimemuona ni mwanaume wa hovyo sana tangu lini mapenzi yakalazimishwa? Mwache mwanamke akupe kwa kuridhia mwenyewe.