Nilimfumania, sasa ananitishia kuniua

Nilimfumania, sasa ananitishia kuniua

Fanya juu chini huyu fyatu akamatwe akajibu kesi ya kutishia kuua. Inawezekana kapewa binti na kodi ya nyumba kafutiwa ili ampunguzie mama mzigo wa kumchunga binti yake. Tulia utapata wa kwako, ukimkosa ni pm tulianzishe.
 
Pole sana,ila wanaume kugusa gusa panapo maua ni kawaida sana...aliyeimba ukitaka wa kwako peke yako muumbe mwenyewe hakukosea
 
Lkn kma ndio ww hapo kweny picha hio profile kaaaaa amakwel Mungu bac mm ningezawadiwa kma ww mbona wangesema umenipa rimbwata
 
Yaani miezi tisa ushamwita mchumba na kumtambulisha kwa wazazi?!
Hapo lazima jamaa alikuingia kwa gia ya kukuoa fasta nawe ukaingia mkenge.

Chukua hilo kama funzo na achana nae huyo hakufai kabisa
Ulitaka akae miaka mingapi ndio awe mchumba?Nyie ndio mnawakalishaga wadada miaka na miaka wakitokea wenye nia wanawaolewa wachumba zenu.
Mnaweza kutana hata ndani ya mwezi na mkaoana
 
Mpuuzi huyo, tundika meseji alizokuandikia akikutishia maisha kwenye mitandao pamoja na jina lake. Ukizembea atakuua kweli, wanaume wengine ni machizi kabisa.
 
Sitaki kuamini huu ujinga,baadhi ya wanaume tunatia aibu sana!unajiuliza mtu kishakufumania,badala ukae ujipange hata jinsi ya kuitoa hiyo aibu machoni pa aliyekufumania(of cause hatakuamini tena na huenda asikusamehe)but uso umeumbwa na aibu kuna leo na kesho,wewe unatoka kumgongea gate eti wewe sio chaguo langu yule ndiye kisha wiki mara unarudi kuomba msamaha na vitisho,hata huyo mwanamke anakushangaa na kuzidi kukudharau ulivyo dhaifu hata kama angefikiria kukusamehe anakuona ulivyo humfai.na wanaume wa hivi ndio wale nyumba ikivamiwa na majambazi yeye anapanda juu darini na kuanza kutoa maelekezo kwa familia yake kwamba jificheni uvunguni.hakuna mwanamke anataka kuolewa na poyoyo la hivi.
 
Jamani huyo mwanaume wako si mzima inawezekana kati ya wale wanne yeye ndio mmoja wapo.Haiingii akilini mtu ufumaniwe halafu wewe tena utake kuua.
Ila na wamama sisi tuna tabia mbaya sana sasa huyo mama mwenye nyumba anabariki kabisa mwanae kubanduliwa humo humo ndani ilihali anajua mkaka ana mchumba mbali na hilo yeye ndio anakuwa mlinzi wao aiseeee kweli ni shidaaa

Adui wa mwanamke ni mwanamke mwenzake
 
Kuna watu ukiachana nao katika mahusiano wanakuwaga kama wehu.
Yaani mtu umemuacha kwa amani ila utajuta mana anakukosesha raha.
Na ukishaona mtu yupo hivo na aliondoka kwa mbwembwe jua alipoenda yamemshinda hivo anataka kukurudia.
Chamsingi simama imara huyo hamaanishi anakutisha tu ili uogope umrudie ila ukikomaa ataona humpapatikii hivo atakuacha.
 
Niibox nikupe pole kwakweli amekukosea mno
 
Huyo hapana kabisaa, fanya yako utaumia bure, huko anakutisha tu uingie mkenge akulipue
 
Haya mama tafuta huyo wa peke yako......
Ushaambiwa mwanaume ni kama baba ntilie, mwiko mmoja vyungu vingi.

Jambo la msingi ungemuuliza tu " Honey mwiko umeuosha? "
Kama ndio nae uutumie zako na maisha yangeendelea.

Haya tafuta wa peke yako uone kama halija kuchwea
UKIMWI je?
 
Jamani huyo mwanaume wako si mzima inawezekana kati ya wale wanne yeye ndio mmoja wapo.Haiingii akilini mtu ufumaniwe halafu wewe tena utake kuua.
Ila na wamama sisi tuna tabia mbaya sana sasa huyo mama mwenye nyumba anabariki kabisa mwanae kubanduliwa humo humo ndani ilihali anajua mkaka ana mchumba mbali na hilo yeye ndio anakuwa mlinzi wao aiseeee kweli ni shidaaa
Inasikitisha sana ndo mama zetu sasa sijui sisi watoto tutakuwaje analinda kabisa
 
Back
Top Bottom