Nilikuwa nakutega tu!!

Nilikuwa nakutega tu!!

Leo katika pita pita zangu nikakutana na mdada mmoja mtaani. Huyu dada tumeshawahi kutana mara nyingi, mi najua anafanya kazi gani ila ya alikuwa hajui kazi yangu. Nikamweleza kuwa nina maongezi naye, akanipa namba yake ili nimtafute jioni. Ilipofika jioni nikamtafuta tukaenda pub moja tukaagiza vinywaji na nyama choma. Tukiendelea kunywa akaniuliza nafanya kazi gani? Nikamwambia mi muuzaji wa duka la mhindi. Si akaanza kujishaua, oooh... Unajua kuna mtu nataka nimuwahi aliahidi kunipa hela leo..!., na sababu zingine kibao! Aakiwa anaendelea kujishaua kuna jamaa anayenifahamu akatukuta pale. Katika kunisalimia akataja Dr. Nyalotsi vipi? Kusikia hivyo nikaona mdada kabadirika, akaagiza na kinywaji kingine na kuniuliza, mbona hukunambia kuwa wewe ni dr? Nikamjibu nilitaka nijue kama utavutiwa na mimi kwanza.. Bahati nzuri na simu yangu ikaita kuna jamaa yangu alikuwa zamu, alihitaji nimsaidie. Lakini bado najiuliza, kukiwa hakuna uhakika wa hela hupendwi? Ina maana ni money for service? Duh, kazi tunayo..!

Ndio maana mimi nimeamua kujikalia zangu parokiani na Husninyo wangu tukiwahudumia kondoo...lol!
CC: Himidini Mentor Heaven on Earth !
 
Last edited by a moderator:
Leo katika pita pita zangu nikakutana na mdada mmoja mtaani. Huyu dada tumeshawahi kutana mara nyingi, mi najua anafanya kazi gani ila ya alikuwa hajui kazi yangu. Nikamweleza kuwa nina maongezi naye, akanipa namba yake ili nimtafute jioni. Ilipofika jioni nikamtafuta tukaenda pub moja tukaagiza vinywaji na nyama choma. Tukiendelea kunywa akaniuliza nafanya kazi gani? Nikamwambia mi muuzaji wa duka la mhindi. Si akaanza kujishaua, oooh... Unajua kuna mtu nataka nimuwahi aliahidi kunipa hela leo..!., na sababu zingine kibao! Aakiwa anaendelea kujishaua kuna jamaa anayenifahamu akatukuta pale. Katika kunisalimia akataja Dr. Nyalotsi vipi? Kusikia hivyo nikaona mdada kabadirika, akaagiza na kinywaji kingine na kuniuliza, mbona hukunambia kuwa wewe ni dr? Nikamjibu nilitaka nijue kama utavutiwa na mimi kwanza.. Bahati nzuri na simu yangu ikaita kuna jamaa yangu alikuwa zamu, alihitaji nimsaidie. Lakini bado najiuliza, kukiwa hakuna uhakika wa hela hupendwi? Ina maana ni money for service? Duh, kazi tunayo..!

At least umemjua ni mtu wa aina gani na kichwani mwake anawaza nini! Hapo sasa kazi ni kwako, maana dunia ni yako na chaguo ni lako!
 
Kudadadeki!
Ukiwa na hela unakula hata visivyoliwa!

Siku hizi nikiulizwa kazi na binti namuambia nauza karanga

Hii kadhia nilishakumbana nayo sana tu
Laiti wangekuwa wanajua.............!!!!!!!!!
 
At least umemjua ni mtu wa aina gani na kichwani mwake anawaza nini! Hapo sasa kazi ni kwako, maana dunia ni yako na chaguo ni lako!

Mkuu habari ya asubuhi?
Jamaa amemuona nyoka kwenye rangi yake hasa

Chaguo ni lake

CC: Mjuni Lwambo !
 
Last edited by a moderator:
Na hivi madaktari wengi hawajipendi (rough rough) muonekano wako ulimlazimisha akuulize wafanya kazi gani.
Ingukuwa smart (simaanishi kichwani) asingekuuliza angekuuliza kwa vitendo na kudeduce kuwa unazo au za kuunga na gundi ya mnyaa.

Wenye "akili" siku hizi hawaulizi hata kama unaonekana muuza "tingisha"
Wanajua wanachokitafuta

Mzima lakini?
 
Leo katika pita pita zangu nikakutana na mdada mmoja mtaani. Huyu dada tumeshawahi kutana mara nyingi, mi najua anafanya kazi gani ila ya alikuwa hajui kazi yangu. Nikamweleza kuwa nina maongezi naye, akanipa namba yake ili nimtafute jioni. Ilipofika jioni nikamtafuta tukaenda pub moja tukaagiza vinywaji na nyama choma. Tukiendelea kunywa akaniuliza nafanya kazi gani? Nikamwambia mi muuzaji wa duka la mhindi. Si akaanza kujishaua, oooh... Unajua kuna mtu nataka nimuwahi aliahidi kunipa hela leo..!., na sababu zingine kibao! Aakiwa anaendelea kujishaua kuna jamaa anayenifahamu akatukuta pale. Katika kunisalimia akataja Dr. Nyalotsi vipi? Kusikia hivyo nikaona mdada kabadirika, akaagiza na kinywaji kingine na kuniuliza, mbona hukunambia kuwa wewe ni dr? Nikamjibu nilitaka nijue kama utavutiwa na mimi kwanza.. Bahati nzuri na simu yangu ikaita kuna jamaa yangu alikuwa zamu, alihitaji nimsaidie. Lakini bado najiuliza, kukiwa hakuna uhakika wa hela hupendwi? Ina maana ni money for service? Duh, kazi tunayo..!

Mkuu huyo njaa tu. Maskini jeuri hana lolote. Hizo tactics hata mm....nazitumia sana na nimewashika wengi type hzo. Most na pretend kuwa interested nao alaf bdae napiga chini, nafukuza kama siwajui. Wako wanawake wengi wa kueleweka.....achana na product za uchwara. Lol
 
Na hivi madaktari wengi hawajipendi (rough rough) muonekano wako ulimlazimisha akuulize wafanya kazi gani.
Ingukuwa smart (simaanishi kichwani) asingekuuliza angekuuliza kwa vitendo na kudeduce kuwa unazo au za kuunga na gundi ya mnyaa.

Khaaa!!!

We Kaunga wewe. Shkamo dada.
 
Hahahah, marihaba umeamka uzuri?

Sijaamka nimekesha. Si unajua tena mie daktari jana nilikuwa zamu ya usiku.

Lakini mie siko rafu kivíile. Usije ukaupiga chini mwaliko wangu bure.
 
Sijaamka nimekesha. Si unajua tena mie daktari jana nilikuwa zamu ya usiku.

Lakini mie siko rafu kivíile. Usije ukaupiga chini mwaliko wangu bure.

Sio mchafu mchafu kama ..........?
Bwana natania tu, vya pombe ndio wanakuwaga wachafu.
Jamani kulikuwa na emergency ngapi? Nakumbuka enzi za mzee wangu, akiwa zamu alikuwa anafuatwa na dreva in case kuna operation au emergency. Siku hizi ikoje?
 
Siku hizi nikiulizwa kazi na binti namuambia nauza karanga

Hii kadhia nilishakumbana nayo sana tu
Laiti wangekuwa wanajua.............!!!!!!!!!

Ayaaaaa!!!
Kaka mleta mada alisema ni muuza duka kwa muhindi, ke alishaanza kuchopoka!
Sasa wewe karanga! Khaa! Usikute anachomoka ndani ya wavu!!!
 
Ayaaaaa!!!
Kaka mleta mada alisema ni muuza duka kwa muhindi, ke alishaanza kuchopoka!
Sasa wewe karanga! Khaa! Usikute anachomoka ndani ya wavu!!!

Mkuu wengi huzimika kama umeme wa Tanesco kila wakisikia hii habari
Ila nimeshajizoea maisha ya kukaa mwenyewe

Siwezi kuishi maisha ya kuigiza mie!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom