Nilikufa halafu badaye nikafufuka...

Nilikufa halafu badaye nikafufuka...

2005 njia zilikuwa Safi kabisa, tena Chambiri alikuwa amelima kujiandaa na uchaguzi, kulikuwa na lami mpaka Sirari, halafu kulikuwa hamna Landover ni michomoko tu, hata ukitembea kwa mguu toka Tarime hadi Nyabirongo, kiongera, matamankwe, au korotambe huwezi kutumia masaa hayo.
Barabara ya lami mpaka 2015 kwa tarime ukiachana na ile ya sirari, ile ya tarime mugumu mpaka leo haijawekwa lami zaidi ya kipande kutoka mjini mpaka mogabiri (ilianza kuwekwa mwaka jana.) Kisha kutoka mogabiri unaikuta tena nyamwana nayo ni kipande cha 1 km ambayo imekuja mpaka jirani na barabara ya nyamongo (wanapaita kipimio) kwenye kona. Hiyo lami ya mwaka 2005 wewe umeitoa wapi ukaiweka tarime nzima? Ni kweli 2005 kulikuwa na michomoko, lakini niambie mchomoko gani ulikuwa unaenda kuanzia bwirege kule. Hii njia ya kwa Gachuma kuelekea nyamongo mpaka leo haina usafiri zaidi ya raia kukodi bodaboda au kusubiri basi la jioni la kwenda nyamongo ndipo wapate usafiri.
 
Sasa mbona humaliziiii?
Au umefariki tena? baadae uje utuambia umefufuka mara ya tatu.
R.I.P in advance.
 
sijasomwa kilicho andikwa ila nitoe comment kwanza
ivi bangi inaruhusiwa lini ili muwe mnatumia kihalali maana hizi mnatumia kinyume na sheria inawapa tabu sana

naenda kusoma sasa maada husika
Bangi itakua unavuta ww usie jielewa
 
  • Thanks
Reactions: amu
Umenifurahisha kwenye karanga tu iwe kweli iwe uongo utajua mwenyewe .Nipe bei ya kilo moja ya karanga hapo Tarime sijui Musoma na aina gani inapendwa hapo .Niingie mzigoni.
 
Ok acha nimalizie, baada ya kuwa nafanya kazi ya kuchunga bila malipo kumbe nyumbani wakuwa wanapeleleza Mimi nilipo! Walisikia nipo Kijiji jirani na siku moja ilikuwa mida ya saa 3 asubuhi alikuja baba mpaka kwenye huo mji. Akawaita wenyeji akaanza kuwalagai kuwa wanidanganye ili anikamate nirudi home. Aisee niliitwa huku nikihojiwa vimaswali vya kitoto Kama fulani yupo nikasema ndiyo. Akaniambia njoo nikwambie Sasa, ila Mimi nilikuwa nichezwa na machare kuwa lazima atakuwa ni mshua kaja kunitafuta

Basi kweli bana nikamuona akiwa akachuchuma mahali ili nisimuone, aisee nilikimbia kama vile nimeona mnyama mkali baba alibaki anasikitika kuwa huyu mtoto ana matatizo gani!? Nilikimbia karibia vijiji 4 hivi mpaka ilipofika jioni ndipo nikaanza kutafuta sehem ya kulala. Basi cku hiyo nikalala kwa Wajaruo dah! Duh Wajaruo siyo watu kabsaaa. Nilikula vrz ila badaye nilikuja kujuta na kutamani nirudi home. Kwa vile Mimi toka utotoni nilikuwa na jeuri, hivyo ule mji wa pale ujaruoni sikukubaliana nao kutokana na Kwanza walikuwa n kabila tofauti na langu na pili walionesha kutokunijali ukilinganisha na pote nikipopita.

Sasa nikaamua kuanza kurudi safari ya kurudi home huki, aisee uchawi upo kabla sijafika nilianza kuhisi Kama sioni vile basi nikapata wasi wasi nikaka njiani kabsa mpaka akaja baba mmoja alipo niona nimelala njiani akaanza kufoka kuwa nahatarisha maisha kwani ningeweza ata kugongwa na baiskel. Basi nikamueleza akanielewa nikasema na kijijini kwetu make nilihisi kuna kitu. Tukaenda nikiwa nimechoka kabsa mpaka tukafika home mida ya saa 9 mchana. Tuliwakuta ndugu zangu wakimenya mihogo baada ya kuniona walishangaa sana huku mama wa kambo akaanza kulia kwani hali yangu ilikuwa siyo shwari.

Basi bana yule mzee akaeleza aliponikuta na Mimi nikiwa naongea kwa sauti ya unyongeee. Mpaka nilipokata roho. Nilikaa nikiwa marehemu kama siku 3 ila cku ya mazishi walikuja walimu wa shule niliyokuwa nasoma kabla sijaacha pa1 na wanafunzi wenzangu. Ndipo mwalimu Oganda alipo kuja kuona marehe mara ya mwisho, aliponiona nikamkonyeza aiseee yule mwalimu alishituka na kusema kuwa sijafa ila kuna mchezo. Basi bana walihairisha mazishi na kukaa kikao cha dharura. Waliafikia kuleta mtaalam na mtalaam kweli kesho yake aliwasili kutoka huko Magu mkoani Mwanza. Alifika akaagiza aletewe mgomba akaletewa make tulikuwa tunalima ndizi kwa wingi.

Basi ule mgomba ulikatwa huku akiongea maneno fulani hivi huku watu wote wakishangaa miujiza baada ya kukata vipande 3 nilitoka ndani ya sanda na kusimama. Ndipo nikaanza kulia huku nikijutia udhurulaji. Nilikaa home mpaka mwaka 2005 ulipoisha nikaingia mwaka 2006 bila ya kuendelea na shule ilipofika mwaka 2006 mwezi wa 8. Nilipelekwa shule nikaanza tena darasa 3. Aisee nilisoma kwa bidii mpaka saivi nipo chuo ila ningejuaga kuwa kutatokea tatizo la ajira niingeendelea na harakati za maisha.

NB: Hii story ni ya kweli na siyo ya kutunga. Imeisha hivyo
 
Umenifurahisha kwenye karanga tu iwe kweli iwe uongo utajua mwenyewe .Nipe bei ya kilo moja ya karanga hapo Tarime sijui Musoma na aina gani inapendwa hapo .Niingie mzigoni.
Mkuu Tarime nilihama toka 2010 saiv sipo huko ila kipindi hicho kilo ilikuaga 600 Kama sikosei
 
  • Thanks
Reactions: EEX
Jaribu siku moja kutembea kutoka pale kilipo kituo cha basi Gachuma, mpaka daraja la mto Mara kisha uje na masahihisho ya kauli yako kwamba hata akitembea kwa miguu. Au hata kutoka kwa gachuma mpaka kimusi ndani huko au muriba.

Unaweza kukosoa kuwa mtoa mada ni muongo, na wewe ukaonekana muongo zaidi.
Mbona unatoa mfano ambao ni irrelevant, yeye amesema alitoka Tar mjini na sio huko unakokusema, kwanza kutoka kwa Gachuma kwenda Kirumi sio Tarime.
 
Barabara ya lami mpaka 2015 kwa tarime ukiachana na ile ya sirari, ile ya tarime mugumu mpaka leo haijawekwa lami zaidi ya kipande kutoka mjini mpaka mogabiri (ilianza kuwekwa mwaka jana.) Kisha kutoka mogabiri unaikuta tena nyamwana nayo ni kipande cha 1 km ambayo imekuja mpaka jirani na barabara ya nyamongo (wanapaita kipimio) kwenye kona. Hiyo lami ya mwaka 2005 wewe umeitoa wapi ukaiweka tarime nzima? Ni kweli 2005 kulikuwa na michomoko, lakini niambie mchomoko gani ulikuwa unaenda kuanzia bwirege kule. Hii njia ya kwa Gachuma kuelekea nyamongo mpaka leo haina usafiri zaidi ya raia kukodi bodaboda au kusubiri basi la jioni la kwenda nyamongo ndipo wapate usafiri.
Lami nimesema nikutoka Tarime hadi Sirari, na maelezo yake uelekeo ulikuwa huo, uwe unaelewa Mada.
 
Mbona unatoa mfano ambao ni irrelevant, yeye amesema alitoka Tar mjini na sio huko unakokusema, kwanza kutoka kwa Gachuma kwenda Kirumi sio Tarime.
Ila zamani ilikuaga ni Tarime. Ila nashangaa mtu anayesema kuwa 2005 kulikuwa hakuna Land Rover
 
Lami nimesema nikutoka Tarime hadi Sirari, na maelezo yake uelekeo ulikuwa huo, uwe unaelewa Mada.
Hpn soma vzr utajua ckuwa na uelekeo huo. Sirari nilifika mwaka jana toka nizaliwe japo na penyewe nilienda kikazi
 
Hpn soma vzr utajua ckuwa na uelekeo huo. Sirari nilifika mwaka jana toka nizaliwe japo na penyewe nilienda kikazi
Msati, barabara ya kojfa, mto Mori ni uelekeo wa Sirari.
 
Back
Top Bottom