Nilifikiri anatania ....anakuja kweli!

Nilifikiri anatania ....anakuja kweli!

MAKULUGA

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2011
Posts
8,098
Reaction score
10,937
Salaam!
Miezi kadhaa iliyopita nilkuwa safari katika Wilaya moja mpya !Bahati mbaya sana kijijij tulipofikia [ambayo ni makao makuu ya wilaya hiyo]Kupata chakula nyakati za jioni ni shida! na hapo ndipo mchezo ulipoanzia!
Baada ya kupata nyumba ya kulala tuliamua kwenda kutafita chakula! Njiani tulikutana na dada mmoja wa makamo,tulimwomba atuelekeze sehaemu tunapoweza kupata mlo...alionesha kushtuka kama kweli kwa mida hiyo tungepata chakula! Hata hivyo alituonesha !
Kama alivotarajia dada yule hatukupata chakula!...tuliamua kununua maji na kwenda kulala!Njiani tulikutana tena na yule dada akitikea dukani kwake ....tukamwelezakuwa hatukufanikiwa!Alitafakari kidogo na kutuambia 'twendeni nikaandalie chakula nyumbani kwangu' kwa namana ya wasifu wake wa nje ulivvyo na mazingira ya kijijini ilitosha kutuaminisha kuwa yule dada ni muungwana ,hivyo kukataa ilikuwa ni ngumu!
Tuliandaliwa chakula kitamu cha usiku.
Katiak maongezi yetu nilifahamu kuwa licha ya kuwa ni nesi pia ni mfanyabiashara wa nguo! na huzifuata Kampala Ugand ....nilimhoji kama anafahamu DAR akasema hajawahi,......nikampa changamoto kuwa ni vema akahamu mji mkuu wa nchi yake na angalie kama anaweza kunufaika na bidhaa rundo kutika Dubai na China Kariakoo ,aliahidi kuwa kuna siku angekuja!
Nilipeenda mara ya pili nilimtembelea ofisini kwake ....wakati ananiaga alinifanyia kitu cha ajabu.......alisimama akanibusu na kuniambia pamoja kuwa [mimi] nipo kilomita zaidi ya elfu moja [kutoka kwao] ila siku moja atanifuata kwani ametokea kunipenda ajabu!
Leo asubuhi nimepokea simu kuwayupo njiani anakuja DAR !
Nimpokee saa 4!a
Nimeshindwa cha kufanya hata kuuliza anafikia wapi [tayari aliniambia hana ndugu wala rafiki Dar (isipokuwa mimi labda)
SIJAJUA NITAMHANDLE VIPI NA SIWEZI MWAMBIA MKE WANGU GHAFLA NAMNA HII
NIFANYEJE
 
Umueleze hali halisi tu kuwa we uko vipi atakuelewa, na utajua jinsi gani ya kumhandle time atakayokua dsm
 
Pole sana kaka kwa hayo yaliyokukuta. Siku hizi wanawake wana bidii sana kutafuta wanaume angalau wapate chochote. Nakushauri kama ifuatavyo;
Andaa guest house then akifika na ukishampokea mpeleke akalale then mambo mengine mwambie kesho. Itakapofika kesho we huonekani na simu yako tayari unakuwa umeizima kabisa ila kumbuka kulipia gharama ya chumba kwa siku mbili na msosi wa siku moja tu, mengineyo atajiongeza mwenyewe.
Vinginevyo, ukijiona una huruma sana kwa huyo mwanamke basi ndoa yako itakuwa mashakani ingawa inategemea pia ulionyesha nini kwake wakati mnaonana kwa mara ya kwanza na wakati ambao mmekuwa mkiwasiliana.
 
Acha mambo ya kitoto pokea mgeni,kama una chumba kimoja lala kwa jirani mpishe,si lazima kufanya ngono, ingawa huko ndiyo naona mnaelekea.
 
unakumbuka shuka kumekucha,hukumjulisha toka mwanzo kwamba umeoa sahizi ndo unahaha mtafutie mahali pa kulala na muelee hali halisi.
 
Choonde zinaa mbaya, na hii ni kwaresma!!

Kuwa mkarimu kwake kama alivyokukarimu, tenda wema nenda usingoje shukrani kaka!!

Ukiweza mshirikishe waifu wako anaweza akawa kinga ya dhambi inayokunyemelea!!

Please mpige shetani teke teke teke kuuuleh!!
 
Salaam!
Miezi kadhaa iliyopita nilkuwa safari katika Wilaya moja mpya !Bahati mbaya sana kijijij tulipofikia [ambayo ni makao makuu ya wilaya hiyo]Kupata chakula nyakati za jioni ni shida! na hapo ndipo mchezo ulipoanzia!
Baada ya kupata nyumba ya kulala tuliamua kwenda kutafita chakula! Njiani tulikutana na dada mmoja wa makamo,tulimwomba atuelekeze sehaemu tunapoweza kupata mlo...alionesha kushtuka kama kweli kwa mida hiyo tungepata chakula! Hata hivyo alituonesha !
Kama alivotarajia dada yule hatukupata chakula!...tuliamua kununua maji na kwenda kulala!Njiani tulikutana tena na yule dada akitikea dukani kwake ....tukamwelezakuwa hatukufanikiwa!Alitafakari kidogo na kutuambia 'twendeni nikaandalie chakula nyumbani kwangu' kwa namana ya wasifu wake wa nje ulivvyo na mazingira ya kijijini ilitosha kutuaminisha kuwa yule dada ni muungwana ,hivyo kukataa ilikuwa ni ngumu!
Tuliandaliwa chakula kitamu cha usiku.
Katiak maongezi yetu nilifahamu kuwa licha ya kuwa ni nesi pia ni mfanyabiashara wa nguo! na huzifuata Kampala Ugand ....nilimhoji kama anafahamu DAR akasema hajawahi,......nikampa changamoto kuwa ni vema akahamu mji mkuu wa nchi yake na angalie kama anaweza kunufaika na bidhaa rundo kutika Dubai na China Kariakoo ,aliahidi kuwa kuna siku angekuja!
Nilipeenda mara ya pili nilimtembelea ofisini kwake ....wakati ananiaga alinifanyia kitu cha ajabu.......alisimama akanibusu na kuniambia pamoja kuwa [mimi] nipo kilomita zaidi ya elfu moja [kutoka kwao] ila siku moja atanifuata kwani ametokea kunipenda ajabu!
Leo asubuhi nimepokea simu kuwayupo njiani anakuja DAR !
Nimpokee saa 4!a
Nimeshindwa cha kufanya hata kuuliza anafikia wapi [tayari aliniambia hana ndugu wala rafiki Dar (isipokuwa mimi labda)
SIJAJUA NITAMHANDLE VIPI NA SIWEZI MWAMBIA MKE WANGU GHAFLA NAMNA HII
NIFANYEJE

Uwe mbwane uwe!!! Chininiii...!
Muleke munanso waso.
 
Mkome kushobokea kila demu na kuwa waongo waongo; mtakuja kutokea mpaka MAJINI mufee na mdhuru familia zenu. Hapo lazima umuhudumie kama alivyokuhudumia wewe Mbulu hakuna lingineeee...
 
Hujamalizia hadithi yako sasa inakuwa ngumu kuchangia, alipokupiga busu na kukwambia anakupenda ulimwambiaje, ulikubali? Uliwahi kumwambia kama una mke Dar au ulijifanya upo singo, Umewahi kuonesha kuwa mko wapenzi kwa namna fulani? Alipowapikia chakula uliishia kula chakula cha nafaka au na kile kingine ulikula?
 
acha mambo ya kitoto pokea mgeni,kama una chumba kimoja lala kwa jirani mpishe,si lazima kufanya ngono, ingawa huko ndiyo naona mnaelekea.
ninavyumba vya kutosha ila ...hatuelekei labda yeye!
 
duh!kazi ipo. .we alivokuambia anakupenda kwanini hukumwambia kuwa una mke? huyo ana mahali pa kufikia ndo maana kakujulisha kuwa anakuja wakat kashapanda gari.
 
Nakushauri zima tu simu yako mapemaaaa.achana nae kidogo kidogo hujaza kibaba kila aianzae safari ajue ataimalizaje fullstop
 
Hilo unalo. Mpokee na Kariakoo umpeleke kwakuwa ni wewe mwenyewe ulimwambie aje Dar. Ila ikimbie zinaa
 
hujamalizia hadithi yako sasa inakuwa ngumu kuchangia, alipokupiga busu na kukwambia anakupenda ulimwambiaje, ulikubali? Uliwahi kumwambia kama una mke dar au ulijifanya upo singo, umewahi kuonesha kuwa mko wapenzi kwa namna fulani? Alipowapikia chakula uliishia kula chakula cha nafaka au na kile kingine ulikula?
nilpigwa na butwaa na sikusemakitu ndio nilikuwa naingia kwenye gari!
Anajua coz nilimwambia nina mke .
Hapana tulikula ndizi na maharage basi
 
Back
Top Bottom