Nilichojifunza Dar es Salaam mpaka sasa

Nilichojifunza Dar es Salaam mpaka sasa

Dar kutamu asikudanganye mtu hakuna mambo ya ukabila wala udini labda kwa waajiriwa is kitaa kikubwa unajishugulisha hamna ishu za kuchorana hata uokoye makopo huku ukifanikiwa kujenga unamaliza kazi unaweza kuweka hata Banda la chips nje kwako ukakamata pesa hata 50k per day mikoani jau ushamba mzigo mikoa yote Ina kasoro ukabila na udini ndo maana napenda dar japo sip kwetu

Mpango mzima viwanja mi kuishi mkoa ambao hauna bahari ni sumu na siwajai kuishi labda mwanza maana kuna ziwa napenda tu

Mchanganyiko mkubwa wa watu hamna inferiority complex kikubwa upambane ila huko mikoani washamba kithenge

Dar ni jiji lenye waisilamu wengi kuliko dini zingine, ndio maana hata mauwaji sio mengi kihivyo.
 
Mimi ni wa mkoani, lakini nitazungumzia kipengele cha mauwaji. hapo kwenye mauwaji nitakukatalia. Kama wewe ni mfuatiliaji wa news basi utakua umeshajua ni kanda zipi watu wake wanauwana kwa wingi!! Hapo dar itoe kabisa, ckatai kwamba hakuna mauwaji, laa hasha, yapo lakinii co mengi kama mikoani.

Njombe
Geita
Iringa
Mikoa ya Kaskazini
Tarime, ingawa muda cjasikia mauwaji.
Toa njombe eka musoma
 
Niliishi Dar miezi sita bila sehemu ya kulala
Nilikuwa nafanya kazi usiku na mchana
Mchana kwenye taasisi moja ya serikali, malipo ilikuwa ni kwa masaa, usiku kiwandani mikocheni. Siku ambazo sikuwa na kazi usiku nilikuwa nakesha bar) club
Siku ambazo sikuwa na kazi mchana nilikuwa nalala beach. Na tulikuwa wengi tu
Uliishi kwa hesabu Kali sana
 
Ila watu wa Dar wanaishi maisha poa sana. Yaani hakuna kufuatana fuatana, au kuchunguzana!

Unaweza ukaishi nyumba ya kupanga hata miaka 20! Halafu hakuna atakaye kuuliza ni kwa nini unaishi nyumba ya kupanga.

Siyo huku Mikoani tuliko aisee! Tena ujiroge ununue ka gari used, halafu bado uwe unaishi nyumba ya kupanga! Utasimangwa wewe na majirani/watu wako wa karibu, mpaka utakauza hako kagari na kwenda kununua kiwanja.

Hata mwanza mkuu, labda wachache. Jiji lenye mzunguko mkubwa wa pesa, all the time watu wake wapo bize hawatakua na time na wewe. Mfano (Dar and Mwanza)Lakinii mikoani mhh ukijamba mji mzima watajua flani amejamba.
 
Ukishindwa kuishi Dar itakuwia vigumu sana kuishi majiji mengine ulimwenguni!!!Dar bado kuna upenyo wa kudaka vifursa, Mjini kila kitu kinauzwa mpk mavi weka kwny package nzuri tu biashara (mbolea ) we mwenyewe ukilemaa mjini utauzwa vile vile! Kaa kijanja.
 
Dar ni jiji la fursa ni sehemu pekee ambayo kila mtu ana nafasi sawa ya kufanikiwa kwa sababu ya mzunguko mkubwa wa pesa uliopo hapo.
Hamna mambo ya kufatiliana eti sijui kulogana kizembezembe. Cha muhimu we fata lililokuleta utaniambia
 
Bongo nyoso ukipita kwa bar unaona watu wanapiga Mitungi mpka kuchee + dadaz warembo hakuna Mfano afu wakati huo we mfukoni una buku 2 tu na hapo ndio umetoka mishe zako za siku nzima

Asikwambie mtu Dar bila deals hutoboi kwa mshahara pekee
Andika kiswahili fasaha, Acha ujinga na upuuzi kuiga watu wa Kenya

Jitu zima na mandevu yako Unaandika kiswahili ambacho hakitumiki kimuundo

Eti"Ukipita kwa bar"

Kwa bar sio kiswahili fasaha

Mnaiga mambo ya mombosa huko, Mnaiga mpaka kuinamishwa
 
Habari wana JF poleni na majukumu ya kazi......Naomba niende moja kwa moja kwa point yangu hapo juu ya kuhusu hili Jiji letu la Bongo dar
Kwanza kabisa nianze na wakazi wa hili Jiji wengi wanashinda njaa pia
Familia nyingi hazilelewi kama Sisi tunaotokaa huko mikoani

Wengi wa waajiriwa na kipato chao hakikidhi mahitaji yao hivyo kufanya waishi maisha ya kukataa hata ndgu na kujikuta wako busy pindi wanapowatembelea.

Wengi hawana hofu ya Mungu kiasi Ni rahisi kukuta Mauwaji, Ugomvi, Ukahaba, Ujambazi na wivi kwa vijana ambao ndio panya road tishio katika baadhi ya mitaa.

Wengi wa vijana wanaokuja toka mikoani hawana pakulala na hata pia wale Machinga wa baadhi ya masoko makubwa huwa wanalala hapo hapo kwa biashara zao.

Nimalize na hili la unaweza kuwa kwenye Hali Nzuri tu ya kiuchumi na mara ghafla ukajikuta huna kitu kabisaaa hii ndio Dar haina mchezo.
Hakuna mtu siku hizi anatoka mkoani kuja Dar,aje kufuata nini hasa ikiwa mikoani sasa kuna barabara nzuri,umeme Vijijini, huduma za afya na fursa kama zote?

Tukija huko labda tufuate huduma za kibingwa na kugeuza..
 
Point yako ni ipi sasa ?
Ulitaka ukae kwa ndugu ili iweje?
Kama dar hupaelewi si urudi tu kijijini?
Mwenye jukumu la kubadili hali uliyonayo ni wewe mwenyewe

Grow and change for a better future of you
Usilalamike ety ndugu hawakupi chakula mara cjui dar ngumu mara ooooh dar wahuni sana
sasa hayo ww yanakuhusu nini mkuu
 
Hakuna mtu siku hizi anatoka mkoani kuja Dar,aje kufuata nini hasa ikiwa mikoani sasa kuna barabara nzuri,umeme Vijijini, huduma za afya na fursa kama zote?

Tukija huko labda tufuate huduma za kibingwa na kugeuza..
Inawezekana ni kweli kwa kiasi fulani ila bado watu wanaoenda Dar na kubakia mazima bado ni wengi sana. Kumbuka kila leo basi zinaingia Dar na kila sampuli ya abiria
 
Kuna ambao wanatengeneza pesa na ambao wapo kwenye msoto na wengine wenye maadili mabovu hizo specimen ulizotaja zote zipo wanasema kuishi DSM ni form six tosha, all the best kwenye utafutaji wako.
Halafu ukiwasikiliza watu wa mikoani utafikiri haya ya msoto,maadili mabovu huko mkoani hakuna.
 
Watu wa dar ni wabinafsi ,wakatili ,hawana ushirikiano ,hawaongeleshani ,ni wachoyo hatari ,Wana njaa hatari ....

Maisha ya dsm ni magumu hatari ,imagine mtu kapanga chumba kimoja ,humo ndani analala yeye ,mke wake ,watoto watatu Tena jinsia tofauti ...bado ndoo za maji +gesi +vyombo+sufuria +madumu +feni + ..... chumba kina makolokolo Kama stooo ....

Usione hawapendi kukalibisha wageni ukafikili wanapenda ohooooo ni mazingira magumu tu ..!!
 
Back
Top Bottom