Nilichojifunza Dar es Salaam mpaka sasa

Nilichojifunza Dar es Salaam mpaka sasa

Bongo ni kawaida unaweza ukawa unatubu zako ghetto huelewi waya mkali hujaiona siku kwa mlo hata mmoja, wakati huo mtaa wa jirani kuna wahuni wanavunja glass, bangi nyingi, vifua wazi na babecue wakiwa wameegesha ndinga zao za hatari uwani wakiburudishwa na milupo pisi kali. Yani kama mtoni vile. Wanatumia hela tu hata week nzima.
Mjini deals Mzee ukitegemea mshahara hutoboi
 
Yupo mwanangu flani yupo Dar soko la Mtongani (kazi zake za sokoni) jana kanipigia nimtumie pesa akatibu mwanae mgonjwa na anasisitiza nitume pesa aokoe maisha ya "malaika". Hapo haangalii mimi nakomaa huku bush kazi yangu kuteremsha mikungu ya ndizi kutoka milimani afu leo mtu wa Dar ndo ananiomba hela eti ya matibabu
 
Bongo ni kawaida unaweza ukawa unatubu zako ghetto huelewi waya mkali hujaiona siku kwa mlo hata mmoja, wakati huo mtaa wa jirani kuna wahuni wanavunja glass, bangi nyingi, vifua wazi na babecue wakiwa wameegesha ndinga zao za hatari uwani 😂😂😂 wakiburudishwa na milupo pisi kali. Yani kama mtoni vile. Wanatumia hela tu hata week nzima.
Tena vinywaji vyao ni kama hivi 👇

294349130_1089686175284023_8177485204204854384_n.jpg
 
Yupo mwanangu flani yupo Dar soko la Mtongani (kazi zake za sokoni) jana kanipigia nimtumie pesa akatibu mwanae mgonjwa na anasisitiza nitume pesa aokoe maisha ya "malaika". Hapo haangalii mimi nakomaa huku bush kazi yangu kuteremsha mikungu ya ndizi kutoka milimani afu leo mtu wa Dar ndo ananiomba hela eti ya matibabu
Bongo nyoso ukipita kwa bar unaona watu wanapiga Mitungi mpka kuchee + dadaz warembo hakuna Mfano afu wakati huo we mfukoni una buku 2 tu na hapo ndio umetoka mishe zako za siku nzima

Asikwambie mtu Dar bila deals hutoboi kwa mshahara pekee
 
Habari wana JF poleni na majukumu ya kazi......Naomba niende moja kwa moja kwa point yangu hapo juu ya kuhusu hili Jiji letu la Bongo dar
Kwanza kabisa nianze na wakazi wa hili Jiji wengi wanashinda njaa pia
Familia nyingi hazilelewi kama Sisi tunaotokaa huko mikoani

Wengi wa waajiriwa na kipato chao hakikidhi mahitaji yao hivyo kufanya waishi maisha ya kukataa hata ndgu na kujikuta wako busy pindi wanapowatembelea.

Wengi hawana hofu ya Mungu kiasi Ni rahisi kukuta Mauwaji, Ugomvi, Ukahaba, Ujambazi na wivi kwa vijana ambao ndio panya road tishio katika baadhi ya mitaa.

Wengi wa vijana wanaokuja toka mikoani hawana pakulala na hata pia wale Machinga wa baadhi ya masoko makubwa huwa wanalala hapo hapo kwa biashara zao.

Nimalize na hili la unaweza kuwa kwenye Hali Nzuri tu ya kiuchumi na mara ghafla ukajikuta huna kitu kabisaaa hii ndio Dar haina mchezo.

Mimi ni wa mkoani, lakini nitazungumzia kipengele cha mauwaji. hapo kwenye mauwaji nitakukatalia. Kama wewe ni mfuatiliaji wa news basi utakua umeshajua ni kanda zipi watu wake wanauwana kwa wingi!! Hapo dar itoe kabisa, ckatai kwamba hakuna mauwaji, laa hasha, yapo lakinii co mengi kama mikoani.

Njombe
Geita
Iringa
Mikoa ya Kaskazini
Tarime, ingawa muda cjasikia mauwaji.
 
Niliishi Dar miezi sita bila sehemu ya kulala
Nilikuwa nafanya kazi usiku na mchana
Mchana kwenye taasisi moja ya serikali, malipo ilikuwa ni kwa masaa, usiku kiwandani mikocheni. Siku ambazo sikuwa na kazi usiku nilikuwa nakesha bar) club
Siku ambazo sikuwa na kazi mchana nilikuwa nalala beach. Na tulikuwa wengi tu
 
Dar kutamu asikudanganye mtu hakuna mambo ya ukabila wala udini labda kwa waajiriwa is kitaa kikubwa unajishugulisha hamna ishu za kuchorana hata uokoye makopo huku ukifanikiwa kujenga unamaliza kazi unaweza kuweka hata Banda la chips nje kwako ukakamata pesa hata 50k per day mikoani jau ushamba mzigo mikoa yote Ina kasoro ukabila na udini ndo maana napenda dar japo sip kwetu

Mpango mzima viwanja mi kuishi mkoa ambao hauna bahari ni sumu na siwajai kuishi labda mwanza maana kuna ziwa napenda tu

Mchanganyiko mkubwa wa watu hamna inferiority complex kikubwa upambane ila huko mikoani washamba kithenge
 
Ila watu wa Dar wanaishi maisha poa sana. Yaani hakuna kufuatana fuatana, au kuchunguzana!

Unaweza ukaishi nyumba ya kupanga hata miaka 20! Halafu hakuna atakaye kuuliza ni kwa nini unaishi nyumba ya kupanga.

Siyo huku Mikoani tuliko aisee! Tena ujiroge ununue ka gari used, halafu bado uwe unaishi nyumba ya kupanga! Utasimangwa wewe na majirani/watu wako wa karibu, mpaka utakauza hako kagari na kwenda kununua kiwanja.
 
Niliishi Dar miezi sita bila sehemu ya kulala
Nilikuwa nafanya kazi usiku na mchana
Mchana kwenye taasisi moja ya serikali, malipo ilikuwa ni kwa masaa, usiku kiwandani mikocheni. Siku ambazo sikuwa na kazi usiku nilikuwa nakesha bar) club
Siku ambazo sikuwa na kazi mchana nilikuwa nalala beach. Na tulikuwa wengi tu
Kawaida sana Mkuu bora hata we ulikua unaenda hata club
 
Ila watu wa Dar wanaishi maisha poa sana. Yaani hakuna kufuatana fuatana, au kuchunguzana!

Unaweza ukaishi nyumba ya kupanga hata miaka 20! Halafu hakuna atakaye kuuliza ni kwa nini unaishi nyumba ya kupanga.

Siyo huku Mikoani tuliko aisee! Tena ujiroge ununue ka gari used, halafu bado uwe unaishi nyumba ya kupanga! Utasimangwa na majirani/watu wako wa karibu, mpaka utakauza gako kagari na kwenda kununua kiwanja.
Umeona eeeh
 
Bongo ni kawaida unaweza ukawa unatubu zako ghetto huelewi waya mkali hujaiona siku kwa mlo hata mmoja, wakati huo mtaa wa jirani kuna wahuni wanavunja glass, bangi nyingi, vifua wazi na babecue wakiwa wameegesha ndinga zao za hatari uwani wakiburudishwa na milupo pisi kali. Yani kama mtoni vile. Wanatumia hela tu hata week nzima.
Nimecheka sana
 
Back
Top Bottom