Kuna mchina mmoja nilimuona You-tube na yeye alikuwa mkatoliki kama wewe. Akasoma Quran lakini akawa na wasiwasi kama uislamu ni dini ya kweli. Basi aliamua kufanya maombi maalumu akamuomba Mwenyezi Mungu, amuongoze na amuonyeshe ukweli ni upi?
Basi akachukua Biblia na Quran, kisha akamuomba Mwenyezi Mungu kuwa amuonyeshe kama Biblia ndio ya kweli kwa kumuonyesha Aya za Biblia zinazosema hiyo ndio kweli. Kwa maana alimuomba Mwenyezi Mungu kuwa atafunga macho na kisha atafungua Biblia randomly akiwa amefunga macho hivyo hivyo na akamuomba Mungu hiyo paragraph atakayoisoma iwe inasema kuwa hii ndio UKWELI ili aufuate.
Na kwamba pia atafungua Quran kama alivyofanya kwa Biblia yani atafunga macho kisha afungue page randomly huku akiwa amefunga macho na hiyo page au Aya atakayokutana nayo iwe inasema HII NDIO UKWELI ili aufuate. Huyu kijana alimwambia Mwenyezi Mungu kuwa ikiwa Biblia itamwambia kuwa ndio kweli basi ataifuata, na ikiwa Quran itamwambia kuwa ni kweli basi ataifuata. Kwa hivyo alimuomba Mwenyezi Mungu amuonyeshe ukweli kupitia vitabu hivi.
Alifungua Biblia kwa mara tatu akiwa amefunga macho na kila alipofungua ukurasa alifungua macho ili asome aone kama atapata Aya inayosema HII NDIO KWELI lakini haikutokea hivyo. Kisha akachukua Quran nayo akafunga macho akafungua randomly kisha akafungua macho ili kusoma akakuta Aya inasema HII NDIO KWELI, kisha akarudia tena kwa Quran na ikaja Aya nyengine tena inasema hii NI KWELI na aifuate. Huyu kijana alisilimu, na alionyeshwa ukweli huu na Mwenyezi Mungu Mwenyewe.
Sasa na wewe fanya hivyo, usiwasikilize watu wewe muombe Mungu atakuonyesha UKWELI na uufuate huo UKWELI. Ngoja nakutumia ile clip uingalie.
Namuomba Mwenyezi Mungu atuongoze wote katika njia iliyo ya KWELI
View: https://youtu.be/BtNDfpzhyzU?si=lKkC1ifHH74Rm8w4