Niko njiapanda ya kuchagua dini sahihi

Niko njiapanda ya kuchagua dini sahihi

Habari wana jf leo ninaswala gumu linanitatiza naitaji maoni yenu.

Kama binadamu wengine namuamini mungu.

Ila napata wakati mugumu kuchagua dini ya kuabudia. Nikisema hivyo namaanisha mini ni mtu ambaye napenda kujifunza sana.

Na kijifunza kwanga kumefanya nibadili jinsi ninavyo itizama dini yangu iliyonelea (ukristo)

Nimekulia katika familia inayo abudua kupitia roman Catholic ila miaka mitano nyuma baada ya kujifunza na kuelewa vitu fulani mimi kama binadamu ninahaki ya kuchagua wapi nikaabudu ivyo nikaamua kubadili na kuwa katika makanisa ya kilokole.

Now nimwaka wa pili sasa huwa najiuliza kama uamuzi niliofanya ni sahihi make najikuta naitaji kubadili tena na safari hii naonelea zaidi kuwa mwisilam (dini ninayoipenda zaidi).

Kinacho nisukuma kufanya hivi sio nafata mkumbo hapana ila kunavitu vingi uwa vinanipa mwaswali na hayo maswali yakikosa majibu basi huwa naitaji kubadilisha msimamo wangu.

Nitaepuka kuweka maswali hayo hapa ili nisianzishe mjadala wa kinidi.

Kiukweli kabisa niko njia panda na ukizingatia naelewa pia sio rahisi kumwamini mungu kwa kuto shiriki katika dini yoyote maana utakosa malezi ya kidini japo wengine ufikili kuingia kwenye dini ni kama kujiingiza kwenye jela yako mwenyewe.

Ntashukulu kwa maoni yako mwana jf.
Dini is the biggest scam acha a nazo.
 
Quran 75:16
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
Quran 75:17
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
Quran 75:18
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.

Quran ni Maneno ya Mungu kuja Kwa mtume Muhammad

Aliyekuwa anayachukua hayo Maneno kutoka Kwa Mungu kwenda Kwa Mtume Muhammad ni malaika Jibril

Malaika Jibril alikuwa anaubeba ujumbe kama ulivyo kutoka Kwa Mungu kuenda Kwa Mtume Muhammad

Hivyo basi hayo ni maelekezo ambayo Jibril yeye ameyatoa Kwa Mungu na hapo anayafikisha Kwa mtume Muhammad

Wewe shida yako Nini hapo?
Mzee umesoma vizuri umezielewa hizo Aya?
 
Wanaouksanya na kuusomesha ni wakina nani?
Wanaousoma ili mtume aufuatilize ni wakina nani?
 
Ala kumbe!

Kwa maana hiyo Zen Buddhism na Tamaduni(culture) ni sawa.

Culture =total way of life

Kila jamii ina utamaduni zake na hata baadhi ya dini misingi yake ni chimbuko la tamaduni fulani.

Kuna:;
Italy
Israel
Arabs
Hindi
China
Russia
England
Japani
Mongolia
Africa nk...


Mleta mada nodetz unataka uondoke na utamaduni wa Jamii ipi
Utamaduni unao nisogeza karib zaid na mung
 
Ila mkuu dini hazipo ili kujibu maswali ya watu wala sidhani kama itakuwa ni sahihi kwa mtu kusema anatafuta dini sahihi kwa kuangalia dini yenye kuweza kujibu maswali.
Mtu kusema anatafuta dini sahihi ni kusema anatafuta utamaduni sahihi, sijui bwana!!
 
Waislamu siku hizi mnakuja kihivi, kujifanya Mkristo eti umechanganyikiwa, endelea huko kwenye uislamu kuabudu huyo Mohammad ambaye alikuwa anagegeda katoto Aisha kakiwa na umri wa miaka tisa
 
Swali lako halipo sawa kitaalamu ila nimekuelewa

So wakati Mtume yupo Quran ilikuwa Ina sura zake na Aya zake
So, kama ilikuwepo mpangilio wake halisi ni upi?
Na kwanini binadamu wakipangulue na kupanga kitabu cha Mungu Kwa utashi wao?

Swali la bonus, Quran imeandikwa lini?
 
Waislamu siku hizi mnakuja kihivi, kujifanya Mkristo eti umechanganyikiwa, endelea huko kwenye uislamu kuabudu huyo Mohammad ambaye alikuwa anagegeda katoto Aisha kakiwa na umri wa miaka tisa
Duuh
 
Mtu kusema anatafuta dini sahihi ni kusema anatafuta utamaduni sahihi, sijui bwana!!
Ila mkuu haya maisha yetu yalivyo ni athari ya kuanzia kwa wazazi,shuleni,jamii husika na imani zetu/dini ndio zimetujenga kuwa hivi tulivyo. Hivyo dini ni kitu kimoja wapo tu ambacho kinatuaminisha mambo na kutufanya tuwe na aina fulani fulani za mitazamo, ila ni jambo ambalo hata wazazi, waalimu mashuleni na jamii pia hutujenga tabia na aina ya mitizamo.
 
Karibu katika uislam lakini ukae ukijua dhima kubwa ya kuwa muislam ni kuitafuta akhera yako (wengine wanaita mbinguni) kwahiyo utamiss vitu kama vile

1. Ushuhuda
2. Miujiza
3. Unabii na manabii wa duniani
4. Maombezi kwa ajili ya kupata utajiri
5. Maombezi ya kuponya magonjwa na miujiza ya kuponya vilema

Kiufupi utajinyenyekeza kwa Mwenyezi Mungu kwa ajili ya kupata pepo yake na sio starehe za dunia
 
Karibu katika uislam lakini ukae ukijua dhima kubwa ya kuwa muislam ni kuitafuta akhera yako (wengine wanaita mbinguni) kwahiyo utamiss vitu kama vile

1. Ushuhuda
2. Miujiza
3. Unabii na manabii wa duniani
4. Maombezi kwa ajili ya kupata utajiri
5. Maombezi ya kuponya magonjwa na miujiza ya kuponya vilema

Kiufupi utajinyenyekeza kwa Mwenyezi Mungu kwa ajili ya kupata pepo yake na sio starehe za dunia
Asante
 
Utamaduni unao nisogeza karib zaid na mung
Hauhitaji dini ili kuwa karibu na nguvu kuu, bali uwepo wako tu ni sehemu ya hiyo nguvu... Kanuni kuu ni "upendo", upendo kwa viumbe vyote vilivyo hai na visivyo hai. Ukiishi hivi ni unatimiza mapenzi ya MUNGU.

Ila kama unajihisi mpweke na unahitaji ufuasi (sense of belonging)
basi inatakiwa uwe karibu zaidi na chimbuko lako /utamaduni (huko ndiko una-chemistry nako nzuri kuliko huko kungine).

Tangu na tangu(millennia) watangulizi wako walikua wanawasiliana na huyo Mungu kwa namna yao. Na walilindwa Na ndio sababu hadi hii leo kizazi chao kipo(upo)...

Na kama unaona tamaduni zenu ni potofu na zimepitwa na wakati, kwa mujibu wa wapinzani wako kiutamaduni, basi unaweza ukachagua tamaduni nyingine yeyote Ile... kwasababu hakuna iliyo ya ukweli na hakuna iliyo ya uongo...

Jibu/nguvu ni moja tu ila njia tofauti(tamaduni), njia nyingine ni nyepesi, zingine za wastani ila nyingine ni ngumu zaidi kulingana na asili silka hulka ya jamii husika.

Ndio maana nikakwambia hata huko ulikokua mwanzo kuzuri pia (kuna nguvu ya ushawishi na nguvu ya wafuasi wenye maarifa mbalimbali.
 
Asante
Hauhitaji dini ili kuwa karibu na nguvu kuu, bali uwepo wako tu ni sehemu ya hiyo nguvu... Kanuni kuu ni "upendo", upendo kwa viumbe vyote vilivyo hai na visivyo hai. Ukiishi hivi ni unatimiza mapenzi ya MUNGU.

Ila kama unajihisi mpweke na unahitaji ufuasi (sense of belonging)
basi inatakiwa uwe karibu zaidi na chimbuko lako /utamaduni (huko ndiko una-chemistry nako nzuri kuliko huko kungine).

Tangu na tangu(millennia) watangulizi wako walikua wanawasiliana na huyo Mungu kwa namna yao. Na walilindwa Na ndio sababu hadi hii leo kizazi chao kipo(upo)...

Na kama unaona tamaduni zenu ni potofu na zimepitwa na wakati, kwa mujibu wa wapinzani wako kiutamaduni, basi unaweza ukachagua tamaduni nyingine yeyote Ile... kwasababu hakuna iliyo ya ukweli na hakuna iliyo ya uongo...

Jibu/nguvu ni moja tu ila njia tofauti(tamaduni), njia nyingine ni nyepesi, zingine za wastani ila nyingine ni ngumu zaidi kulingana na asili silka hulka ya jamii husika.

Ndio maana nikakwambia hata huko ulikokua mwanzo kuzuri pia (kuna nguvu ya ushawishi na nguvu ya wafuasi wenye maarifa mbalimbali.
Asant mkuu na kama nimekuelewa vizuri unamaanisha hatuitaji mwongozo wa kufuata ila tunaitaji tuu kuwa na upendo ?
 
Soma Biblia kwanza, angalau vitabu 6 vya kwanza. Vitabu Viwili vya Manabii(Isaya, Yeremia), Injili 2(Mathayo + Yohana) na Vitabu vitatu vya Paulo.

Kisha uendelee kusali, utapata tu mwalimu mzuri.
 
Back
Top Bottom