Mkuu Huko nilikwisha toka siku nyingi sana kwenye kuamini invisible God......... Nilipitia exactly hatua kama unazopitia wewe kwa sasa hadi nilipokuja kubaini PASI NA SHAKA YA ZIADA kwamba HAKUNA MUNGU zaidi ya Hadithi tu za kisadikika
Keep digging.......
Ahaaa, kwa hiyo Mkuu, ulimwengu ulitokea ghafla ghafla tu (kibahati bahati), na vitu vikajipanga vyenyewe (kwa ustadi) kibahati bahati tu?
Fikiria mfano wako (binadamu):
1. Mdomo umetokea kibahati bahati ukakaa mahali hapo ulipo, na pamefaa/endana kabisa na kazi yake—haikutokea mdomo ukajiweka begani, tumboni, au katikati ya miguu—na mdomo una meno, ulimi, na ukaunganishwa na mfumo kamili wa usagaji chakula. Na mfumo huo ukabeba viungo mbalimbali vyenye sifa/muundo maalumu unaopelekea ufanisi wa kazi mfumo huo.
2. Mfumo wa usagaji chakula ukaunganishwa kikamilifu na njia ya kupumua na kuzungusha virutubishi mwilini, kwa usahihi wa ajabu (imetokea kibahati bahati tu?).
3. Viungo vya uzazi vipo katikati ya miguu, sehemu inayovilinda, na sio kichwani mfano pale penye mdomo au macho au utosini. Na kila jinsia ina mpangilio wake wa kipekee na adaptations zinazowezesha uzazi kufanikishwa.
4. Mfumo wa seli na sehemu zake zote, ikiwemo DNA (ndani ya chromosomes)—ambayo imehifadhiwa sana (highly conserved) na hubeba taarifa muhimu zinazofafanua sifa na muundo wa binadamu (traits).
Ikawa ktk uzazi, idadi za chromosomes (46) kwa kila jinsia zinagawanyika kuwa nusu, na zinaungana na nusu za jinsia ya pili kuwa 46 kamili?
Hivi vyote, vinavyofanya kazi kwa usahihi na kwa kushirikiana, vingewezaje kutokea tu kwa bahati bahati pasi na kuwepo aliyevitengeneza na akaamua kuvipanga ktk huo mpangilio wa ajabu usioleta mushkeli ktk ufanyaji wa kazi wa vitu/viungo/mifumo hiyo kwa ujumla?
Mkuu, Vipi nyumbani kwako au chumbani kwako, imewahi kutokea vitu vikajipanga vyenyewe kibahati bahati? Asiwepo aliyevipanga?
Au sofa likajitengeneza lenyewe pasi na kuwepo mtengenezaji (fundi), rangi ya nyumba ikatokea yenyewe kwenye kuta za nyumba yako pasi na kuwepo mtengenezaji wala mpakaji?