Niko njia panda, ushauri tafadhali

Niko njia panda, ushauri tafadhali

Pole sana mkuu. Ila kufanya mahusiano na Single mama nisawa na kujivika bomu lililosetiwa muda.
Kama umependa na unahisi upo tayari kuumizwa endelea na mipango yako ya kumuoa.
Pia kwa umri wake, bado sana kuexperience maisha yalivyo.
 
Ukweli ni mchungu lakini kuoa single mother ni kukosa ushauri kutoka Kwa wazazi/walezi wako.ukiwa nae ktk mahusiano anacholenga yeye ni namna atakavyokutumia wewe kumuendeleza mwanae ....kimasomo,mavazi na malazi. Upendo wao mkubwa huwa Kwa mwanae na ni rahisi Sana kubadili maamuzi pale unapochelewesha huduma.
Nilikua na single Maza mmoja alinisumbua Sana ila nyuma ya pazia bado jamaa aliemzalisha walikua na mawasiliano ya karibu.wana mengi yaliyojificha ila ukitaka kuharibu uelekeo wa maisha na maono yako basi uoe SINGLE MOTHER.
 
Mkuu ijapo kila mtu huwa bize kwenye kazi katika nyakati tofauti, lakini inapofika kwenye kupenda utajibu tu hata Kama ni kwa kifupi kumjulisha mwenzako ni muda gani utakuwa free, Ukiona unayefikiria anakupenda hapendi kuutumia muda unaopata hata Kama ni kidogo pamoja na ww, basi ujue hapo hamna kitu zaidi ya kwamba she is there for another mission not love
 
Niko kwenye mahusiano na single mother yapata miezi mitatu Sasa, na lengo lilikuwa nimuoe. Huyu mwenzang naona kidogo hajatulia maana nilifuma SMS kwenye simu yake akiwa bado anaendelea kuwasiliana na mpenzi wake wa zamani nikauliza akapoa kidogo na kunambia kuwa jamaa amemtafuta kwa lengo la kumjulia hali. Ana mtoto mmoja mpaka sasa na umri wake ni miaka 20 hivi.

Wiki moja iliyopita sikuweza kuwasiliana nae ndani ya kama siku 5,maana kila nikituma SMS na ata nikimpgia simpati hewani nikashindwa kumuelewa kabisa. Siku ya jumatano alinipigia simu na kunijuza kuwa yuko Moshi kwa dada yake ikabid nimuulze ni kwa nini kaondoka bila kunipa taarifa lakin jibu lilikuwa "nimeondok ghafla pia nilishindwa kuja kukuaga sababu nilikuw busy,naomba unisamehe" kiukwel iliniuma sana nikaona sina thamani kwake kwa lolote lile. Lakini ikabidi nimsamehe tu baada ya kuzungumza nae.

Tangu niko nae amekuw ni mtu wa kutaka pesa tu kila wakati na jana kanipigia simu nimtumie elfu 80, nikauliza ni kwa ajili ya nini anasema matumizi,nikaona isiwe kesi hiyo pesa ntamtumia jioni. Imefika muda wa saa 10 Alasiri jana nikamjuza kuwa niko nje kidog ya mji na huduma za fedha uku ni ngumu kidogo hivyo anivumilie mpaka leo asubuh ndipo nimtumie. Lakini akajibu kwa jazba"najua hunipendi najipendekeza kwako ndo maana unashindwa nitatulia shida zangu kwa wakati" Wakuu nahisi kichwa kinaanza kuuma kwa mbali nikaona hii sehemu nilipo si sahihi hata kidogo,nikatoa laini ile hewani nikaweka laini mpya hivyo mawasiliano yakaishia jana jioni.

Asubuh kaja rafiki yangu ananijuza kuwa yule binti amempigia na kumuuliza kwa nin sipatikani ama niko na mtu mwingine na tangu yeye kaondoka labda kuna mtu alishawahi kuja kwangu na mambo mengi.

Sasa niko njiapanda nimtafute ama niachane nae,msaada tafadhali.
We jamaa bhana, hakuna mwanamke hapo, shtuka piga chini fanya mambo mengine
 
Hivi unawezaje kuumizwa moyo na singo maza?
Nafkiri umeipuuza ile kanuni yetu no 1 inayosema singo maza haolewi
 
Dawa hapo ni kumuacha tu kabla hajazid kukuumiza inaonesha unampenda sana
 
sheria namba 1 usioe singo maza
sheria namba 2 usioe singo maza
sheria namba 3 usioe singo maza

kama unaona wanawake wameisha basi muoe tu ila usije hapa tena kufungua uzi.
 
hakuna mwanamke alieolewa na kuzaa akaachana na mzazi mwenzie moja kwa moja! mawasiliano juu ya mtoto hayaishi na wanaweza kurudiana wakati wowote au wasirudiane!! hapo huna chako unachunwa tu, mbona wanawake wengi mtandaoni fb huko na mitaani! tafuta ambae hajazaa!!
 
pole...sana kwa kifupi wewe ni rimbukeni wa mapenzi...
ukiona mfupa umemshinda fisi ujue hakuna mnyama yeyote porini atakae uweza.

ebu wewe mwenyewe jiulize mwanaume mwenzako kamshindwa hadi amemuacha..
wewe unajidai kidume kumfuata mwanamke alieshindwa na mwanaume mwenzako...utamuweza wapi huyo...?

tumia akili kufikilia....
Ukisema hivo unakosea mkuu,hakuwa kwenye ndoa bali alizalishwa tu mtoto na huyo mtu wake akamkimbia aliporejea ndipo naona mawasiliano bado yanaendelea
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom