Niko njia panda, ushauri tafadhali

Niko njia panda, ushauri tafadhali

Ifike wakati muwe mbaacha ujinga basi mnatudhalilisha sana WANAUME,hapo mpaka umeambiwe umekalia kaa la moto ndipo uinuke???
 
Ipo hivi nilioa single mother mwaka jana mwezi October,anaishi Mwanza na mimi nipo mkoa jirani,mwezi January akaomba aende Mwanza kuona maendeleo ya biashara zake(ana duka la nguo)
Muda wote alishanihakikishia kwamba hana mawasiliano na baba wa mtoto wake,na mtoto anaishi na bibi yake hivyo mawasiliano na pesa ya matumizi yapo kwa bibi yake,
Aliporudi kutoka Mwanza(alikaa wiki moja)nikakagua simu yake na kukuta kama siku tatu mfululizo walikuwa wakiongea na mzazi mwenzake.
Kuongea na mzazi mwenzake kwangu siyo tatizo maana siwezi kujua waliishije mpaka kuzaa pamoja.Ila kilinichonistua ameenda huko ndipo wakawasiliana karibia kila siku, na nilipomuuliza mbona ulisema hamuwasiliana ina maana ulinidanganya? Akasema "alipiga kujua hali ya mtoto wake"
Mimi mtu mzima nikaona huyu hatutafika mbali,bora nimpunguze kabla sijaingia gharama na kupoteza muda.
Nilimuacha kistaarabu sana mpaka leo hajui kama tumeshaachana au laa,kwa sasa siwezi kuoa mwanamke aliyewahi kuolewa au kuzaa na mtu mwingine bora nitafute tu gurunyembe ambalo halijawahi kuolewa wala kuzaa lije liniharibikie mwenyewe.
 
pole...sana kwa kifupi wewe ni rimbukeni wa mapenzi...
ukiona mfupa umemshinda fisi ujue hakuna mnyama yeyote porini atakae uweza.

ebu wewe mwenyewe jiulize mwanaume mwenzako kamshindwa hadi amemuacha..
wewe unajidai kidume kumfuata mwanamke alieshindwa na mwanaume mwenzako...utamuweza wapi huyo...?

tumia akili kufikilia....
Huuu msemo wa waha huwa una ukweli ndani yake mwanamke aliyeshindwa na mwanaume mwenzio wewe utamuweza.
 
Tulisha waambia, ukitaka kuoa single mother hakikisha baba mtoto wake amekufa na akuonyeshe kaburi lake.
 
Ipo hivi nilioa single mother mwaka jana mwezi October,anaishi Mwanza na mimi nipo mkoa jirani,mwezi January akaomba aende Mwanza kuona maendeleo ya biashara zake(ana duka la nguo)
Muda wote alishanihakikishia kwamba hana mawasiliano na baba wa mtoto wake,na mtoto anaishi na bibi yake hivyo mawasiliano na pesa ya matumizi yapo kwa bibi yake,
Aliporudi kutoka Mwanza(alikaa wiki moja)nikakagua simu yake na kukuta kama siku tatu mfululizo walikuwa wakiongea na mzazi mwenzake.
Kuongea na mzazi mwenzake kwangu siyo tatizo maana siwezi kujua waliishije mpaka kuzaa pamoja.Ila kilinichonistua ameenda huko ndipo wakawasiliana karibia kila siku, na nilipomuuliza mbona ulisema hamuwasiliana ina maana ulinidanganya? Akasema "alipiga kujua hali ya mtoto wake"
Mimi mtu mzima nikaona huyu hatutafika mbali,bora nimpunguze kabla sijaingia gharama na kupoteza muda.
Nilimuacha kistaarabu sana mpaka leo hajui kama tumeshaachana au laa,kwa sasa siwezi kuoa mwanamke aliyewahi kuolewa au kuzaa na mtu mwingine bora nitafute tu gurunyembe ambalo halijawahi kuolewa wala kuzaa lije liniharibikie mwenyewe.
Shukran mkuu kwa ushauri
 
Kilichopendwa hapo ni uwezo wako wa kugharamia tu,hakuna mapenzi ya kweli hapo
 
Niko kwenye mahusiano na single mother yapata miezi mitatu Sasa, na lengo lilikuwa nimuoe. Huyu mwenzang naona kidogo hajatulia maana nilifuma SMS kwenye simu yake akiwa bado anaendelea kuwasiliana na mpenzi wake wa zamani nikauliza akapoa kidogo na kunambia kuwa jamaa amemtafuta kwa lengo la kumjulia hali. Ana mtoto mmoja mpaka sasa na umri wake ni miaka 20 hivi.

Wiki moja iliyopita sikuweza kuwasiliana nae ndani ya kama siku 5,maana kila nikituma SMS na ata nikimpgia simpati hewani nikashindwa kumuelewa kabisa. Siku ya jumatano alinipigia simu na kunijuza kuwa yuko Moshi kwa dada yake ikabid nimuulze ni kwa nini kaondoka bila kunipa taarifa lakin jibu lilikuwa "nimeondoka ghafla pia nilishindwa kuja kukuaga sababu nilikuw busy,naomba unisamehe" kiukwel iliniuma sana nikaona sina thamani kwake kwa lolote lile. Lakini ikabidi nimsamehe tu baada ya kuzungumza naye.

Tangu niko nae amekuw ni mtu wa kutaka pesa tu kila wakati na jana kanipigia simu nimtumie elfu 80, nikauliza ni kwa ajili ya nini anasema matumizi,nikaona isiwe kesi hiyo pesa ntamtumia jioni. Imefika muda wa saa 10 Alasiri jana nikamjuza kuwa niko nje kidog ya mji na huduma za fedha uku ni ngumu kidogo hivyo anivumilie mpaka leo asubuh ndipo nimtumie. Lakini akajibu kwa jazba"najua hunipendi najipendekeza kwako ndo maana unashindwa nitatulia shida zangu kwa wakati" Wakuu nahisi kichwa kinaanza kuuma kwa mbali nikaona hii sehemu nilipo si sahihi hata kidogo,nikatoa laini ile hewani nikaweka laini mpya hivyo mawasiliano yakaishia jana jioni.

Asubuh kaja rafiki yangu ananijuza kuwa yule binti amempigia na kumuuliza kwa nin sipatikani ama niko na mtu mwingine na tangu yeye kaondoka labda kuna mtu alishawahi kuja kwangu na mambo mengi.

Sasa niko njiapanda nimtafute ama niachane nae,msaada tafadhali
Wewe ni mpumbavu, endelea kukaa na upumbavu wako
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom