Niko dilema nishaurini

Niko dilema nishaurini

Huyo mwanamke huwezi kuishi naye la utavuruga mpango mzima wa maisha yako na huenda ukapunguza siku za kuishi anaonekana ni pasua kichwa kweli kweli. Kama kinachokupa tabu ni malezi ya mtoto, fanya utaratibu wa kimahakama umchukue mwanao atakua tu. Japo kisheria mtoto anatakiwa akae na mamaye hadi atimize miaka 7 lakini yapo mazingira ambayo mahakama huruhusu baba kumchumkua mtoto inapoonekana ustawi wa mtoto upo mashakani mikononi mwa mamaye. Hapa naona una kila hoja ya kuishawishi mahakama kukukabidhi mwanao.
 
Unataka ushauri upi? Kwanza una hakika huyo mtoto ni wako? Mbona hakukuambia tangu alipojua ni mja mzito? Kama ukishahakikisha mtoto ni wako unataka kumwoa mama wa mtoto wako kwa kuwa unampenda yeye au unampenda mtoto au ni kwa shinikizo la familia yake? Naona kama ndugu zake wanamgandamiza huyo mpenzi wako anafuata ushauri wao. Je una hakika ukimwoa hao ndugu hawataweza kuja kukuvurugia kwa ushauri wao mbaya?
Mkuu nina hakika ni mwanangu kwa vipimo vyangu vya macho kufanana na vipino vya ndugu na jamaa pamoja na mama yangu hakuna shaka yule ni mwanangu.
Hakuniambia kwa madai ya kuwa alikuwa ameshaona nataka kukimbia akawa ananiomba ela akidai ana shida kumbe alitaka aitoe kimya kimya na mimi sikumpa hiyo ela kwakuwa nilikuwa nishampotezea.
Akaamua kumwambia ndugu yake huyo ndugu yake akayafikisha kwa wakubwa.
Kusema kweli sikuwah kumpenda ila baada ya mtoto kuzaliwa I wanted to try ila hilo tukio walilofanya limenifanya nibadili mawazo.
Na hasa hata ukiongea naye yani anachukulia poa kinachomuuma ni kuwa sasa ana hali ngumu ya maisha huko aliko ila haoni kama walinikosea sana na saa nyingine inakuwa ananilaumu kwanini simrudishi dar. Sasa naona hajajifunzi ilifka november atakuwa katimiza mwaka.
 
Wanawake wengine wanatafuta hizi bahati hawapati....ungekuwa umtelekeza ingekuwaje?? Hata kama humpendi angalia kwanza welfare ya mwanao kwanza...
Mkuu ajabu ni kwamba ana dada yake flani ana watoto wawili kazaa na watu wawili tofauti na wametelekezwa hawamsaidii yeye ndiye anahangaika nao.
Lakini mimi niliyejitolea kumlea yeye na mtoto familia inaniona fala.
 
Huyo mwanamke huwezi kuishi naye la utavuruga mpango mzima wa maisha yako na huenda ukapunguza siku za kuishi anaonekana ni pasua kichwa kweli kweli. Kama kinachokupa tabu ni malezi ya mtoto, fanya utaratibu wa kimahakama umchukue mwanao atakua tu. Japo kisheria mtoto anatakiwa akae na mamaye hadi atimize miaka 7 lakini yapo mazingira ambayo mahakama huruhusu baba kumchumkua mtoto inapoonekana ustawi wa mtoto upo mashakani mikononi mwa mamaye. Hapa naona una kila hoja ya kuishawishi mahakama kukukabidhi mwanao.
Unalosema kweli mkuu, mimi lengo langu ilikuwa baadae nimfungulie biashara au aende asomee kitu kimsaidie maishani lakini niliwahi kujaribu ongea naye ikawa kama hayuko tayari kwa lolote.
Sikutaka tu nimuache hivi hivi kwakuwa nilizaa naye na sikuwa na mpango wa kumuoa nilitaka nimjengee msingi wa kujinasua lakini ndiyo wakavuruga.
 
Moyo wako.kama haupo tayri kuishi na mama mtu usijilazimishe na kwa tabia alizozionesha ndani ya muda mfup weny changamoto uyo si mke ila ni mwanamke
..fanya juu chini umpate mtoto
Then mama ake atajua afanyaje..tafuta mfanyakaz wa ndani maisha ya songea.babu...
Ilaa next TIME unapo HIT tumia njia za kuzuia mattz ya mkataba
All the best
 
Pole sana ndugu, kaa kwanza uyatafakari maana haya ni mambo makubwa. Unaeza mchukua mwanao na kumleta kwenu kwa maana wewe ni mtoto wa kiume, ulipo wewe ndo mwanao alipo. Kitamaduni mtoto wa kike akipata mtoto anakuwa si wa upande wa kwao ila anakuwa upande wa mume.
 
Anaendeshwa na dada yake na hii ni kutokana na kwamba hawamtambui jamaa. Lakini akishamuoa heshima inakuja na huyo mwanamke hatayumbishwa tena na dada yake.

Wanaume Huwa tunachukulia kiurahisi rahis suala la kumpa mtoto wa watu mimba . Tunapaswa kujua kila mzazi ana mindset ya maisha ya wanawe hivyo anapotokea mtu wa kumpa mimba mwanae miparakano lazima iwepo.

Muoe huyu mdada aseeh. Tena naona anakupenda sema ni kuendeshwa na dada na mama yake tu.
Mkuu hilo nalifahamu na nilikuwa tayari kumuhudumia kumsomesha au hata kumfungulia biashara lakini hakuwa interested.
Pia sikwenda kwao nikambeba tu, nilipewa idhini na mama yake baada ya shemeji yake kuwa anamsimanga na akataka mrudisha moshi.
 
Pole sana ndugu, kaa kwanza uyatafakari maana haya ni mambo makubwa. Unaeza mchukua mwanao na kumleta kwenu kwa maana wewe ni mtoto wa kiume, ulipo wewe ndo mwanao alipo. Kitamaduni mtoto wa kike akipata mtoto anakuwa si wa upande wa kwao ila anakuwa upande wa mume.
Mtoto naweza mchukua nikamwekea mtu wa kumlea maana sitaki alelewe na mama yangu nataka mwamangu niwe namuona kila siku.
Lakini mpaka naamua kumpangia ilikuwa sitaki kumnyanganya mtoto kwakuwa nilikuwa na perception kuwa anampenda mwanae sawa na mimi na ana haki ya kumlea mwanae kambeba mimba miezi 9.
Lakini sasa naona kama mambo si mambo
 
Mama alinikataza.nisiwe.na mazoea na wachaga
 
Hii ngumu kumeza ndugu mi hata sijui niseme nini Ila nakushauri piga goti omba Mungu atakuonyesha njia iliyo sahihi zaidi ili kusije kuwa na majuto baadae
 
Du ndugu pole kaka, ila nakupongeza sana ndugu yangu una moyo wa utu, tena utu haswa na umejiyaida mno mpaka hapa ulipofikia na una moyo aisee,kama ingekuwa ni mimi kwanza kitendo cha kuondoka nilipompangia na kubeba kila kitu pasipo kuniambia,na ukawa na moyo wa kumtafuta mpaka kwao na ukafika na kupigwa juu aisee pole ila tunatofautiana sana wanaume,kwanza kitendo cha kupigwa ukweni pasipo na makosa hilo pekee ni kosa la jinai aisee,mimi nigeleta kirikuu napakia kila kitu nilichonunua na sitaangalia nyuma mpaka waje waombe radhi kwa wazazi wangu/wanaume wa siku izi sijui ni nini shida aisee,kama hapo ikishindikana waende kwenye vyombo vya sheria ukajieleze huko usitishike aisee eeebo
 
Hivi watu wa Moshi ni kabila gani eti? Samahani lakini
Kuna wasafa walikuja manamba kufanya kazi ktk mashamba ya miwa TPC, kuna wangoni, wanyiramba, waluguru, wasandawe, wabaribaigi, wamasai, wanyaturu, wamakonde, wasambaa, wapare, wachaga, wagogo, wambulu vipi niendelee?
 
Back
Top Bottom