Nicholas E. Mgaya amjibu JK

Umeridhishwa na majibu ya Mgaya dhidi ya JK?


  • Total voters
    65
tucta.JPG

tucta+(1).JPG

tucta+(2).JPG

tucta+(5).JPG
 
Kwa ufupi Mgaya CV kaisha pandisha, na yuko juu, na Mkulu hakujua kwamba kwa kumponda kwakutumia data feki kwa mrindimo wa mipasho ndo kaisha mpaisha jamaa, vijana wa leo wanasema hiyo ilikula kwa JK Yaani sasa hivi Mgaya yuko juu ile mbaya!

Kwa sasa hivi akirudi kwao Njombe anaweza gombea jimbo lolote napenda agombee kwa Anna Makinda.
 
Pole sana Mh Rais Kiwete, jamaa wa TUCTA wamekuvua nguo hadharani Msikitini....! Tanzania ya leo si ya mabwege tena! Huyu Mgaya na Mhadhiri wa Mzumbe kwa kweli Muungwana hata wasahau siku za hapa karibuni.
 
Tamko la TUCTA juu ya hotuba ya Mh. Rais...
Mheshimiwa mmoja bungeni alitoa mifano mingi sana kuwa nchi haiwezi kutawalika ikiwa kuna kundi dogo linafaidika katika nchi huku kundi kubwa linataabika. Nimeshitishwa kusoma taarifa hii kuwa Kikwete ametamka kwenye hotuba yake kuwa kima cha chini hakiwezi kuongezwa kufikia 315,000 hata katika kipindi cha miaka 8 ijayo. Maana yake kwa wafanyakzi ni kutomchagua Kikwete na CCM yake kwa sababu Kikwete amethibitisha kuwa mpaka mwaka 2018 bado wafanyakazi wataendelea kula vumbi. Hapa kweli watanzania tuliuvaa mkenge. Hatuna rais, CCM wanajali matumbo yao tu. Kuanzi wabunge hadi mawaziri na rais hawawajali watanzania.
 
Hapa ukweli unajulikana, Rais amevuliwa nguo. Huyu jamaa basi tu... alipataje kushawishi umma na kupata kura? maskini najutia kura yangu.
 
Nimesoma majibu ya TUCTA,kwa kweli yazidi kumdhalilisha Muungwa kwa kiwango cha kutisha
 
Wamejitahidi kucounter pamoja na kwamba kuna kawogawoga flani kwenye huu ufafanuzi,mfano kwa nini hawajanyambulisha hizo trilioni sita zilizokuwa zikisisitizwa na nkulu???????? anywayz ndiyo mambo ya dunia ya tatu!!!!!!!!!! All in all go TUCTA go!!!!!!!!!!!
 
Wamejitahidi kucounter pamoja na kwamba kuna kawogawoga flani kwenye huu ufafanuzi,mfano kwa nini hawajanyambulisha hizo trilioni sita zilizokuwa zikisisitizwa na nkulu???????? anywayz ndiyo mambo ya dunia ya tatu!!!!!!!!!! All in all go TUCTA go!!!!!!!!!!!

Hawana woga wana heshimu sheria.
Wamesema sheria inawakataza kutangaza wanachojadliana mpaka majadiliano yaishe.

Kwa hiyo subiri baada ya tar 8 watatoa mchanganuo
 
Naam,sasa ngoma inogile...Aibu iliyoje kwa mr prez.Kama kawaida,alilishwa kasa na hao wasaidizi wake.Wasaidizi my foot!
 
Duh....JK mkulu kachuuzwa vibaya sana na taarifa za kukusanya. Ndio maana Nyerere alikuwa akiwacharaza bakora Mawaziri wadanganyifu.
 
Aibu kubwa!
Ati huwezi lipa mshahara wa 315 000 hata kama ni miaka 8 ijayo? Ulidhani maisha bora kwa kila mtz yanaletwa kwa 80,000. Hii ni kauli ya kustaajabisha! Wakati wenzako wanasema YES WE CAAAAN!!! Wewe for Christ's sake unasema YES WE CAN'T. Hivi urais nini? Jambo dogo kama hilo linakushinda nini? Kuna wachumi wangapi Tanzania hii ambao ukiwaita wakafanya projection ya kile TUCTA wanataka ukaja na credible figures, Uka side na wafanyakazi wako ukaweka mkakati, ukaziba mianya, ukaongeza ufanisi mambo yaka unfold yenyewe!!!

Badala yake unakuja na kauli mfu kabisa! kabisa! In a simple plain language Mtanzania hana tumaini la kuyaona maisha bora labda mpaka baada ya miaka minane!
Mnafiki ni mtu anayesema halafu hatendi, Kauli mbiu ya mwaka huu yafaa uwaeleze watz unachomaanisha hasaaa! Maisha bora kwa kila Mtanzania 2019 tujue moja!!!
 
Ndiyo faida ya mtu anayepaswa kuwa kiongozi wa nchi kukurupuka na kupayuka hadharani, matokeo yake ni kuumbuka. Rais anawezaje kuhutubia kama vile amegombana na Mgaya kwenye mambo yao binafsi? Kwake yeye anadhani kila mtu anayeuanika uongozi wake ana agenda au ametumwa na wale wanaoutaka urais. Mediocre thinking!!
 
MgaYa angetulia tu!..Maana zile nyaraka alizotoa Rais wa TUCTA mbona zilitosha kuthibitisha Uzushi na Ubabe na Udhushi wa Mwenye Kaya?... Kujibu tuhuma ni sawa na kuendelea kumdhalilisha Mwenyekaya na wambea wake waliomdanganya......

TUCTA wametimiza haki yao ya msingi ya kutujuza watanzania kwamba siyo Waongo, Wazandiki nk. Kauli zao hazina jazba na zina dhamira ya kweli ya kumkomboa mfanyakazi w Tanzania. Tuwape moyo tusirudi nyuma
 
Aibu kubwa!
Ati huwezi lipa mshahara wa 315 000 hata kama ni miaka 8 ijayo? Ulidhani maisha bora kwa kila mtz yanaletwa kwa 80,000. Hii ni kauli ya kustaajabisha! Wakati wenzako wanasema YES WE CAAAAN!!! Wewe for Christ's sake unasema YES WE CAN'T. Hivi urais nini? Jambo dogo kama hilo linakushinda nini? Kuna wachumi wangapi Tanzania hii ambao ukiwaita wakafanya projection ya kile TUCTA wanataka ukaja na credible figures, Uka side na wafanyakazi wako ukaweka mkakati, ukaziba mianya, ukaongeza ufanisi mambo yaka unfold yenyewe!!!

Badala yake unakuja na kauli mfu kabisa! kabisa! In a simple plain language Mtanzania hana tumaini la kuyaona maisha bora labda mpaka baada ya miaka minane!
Mnafiki ni mtu anayesema halafu hatendi, Kauli mbiu ya mwaka huu yafaa uwaeleze watz unachomaanisha hasaaa! Maisha bora kwa kila Mtanzania 2019 tujue moja!!!
Kauli mbiu ni maisha bora kwa wabunge, mawaziri, rais, na mafisadi wengine.
 
Mie nimepapenda hapa jamani..."TUCTA imesikitishwa na kauli ya Mheshimiwa Rais kudai kuwa haitaji kura za Wafanyakazi wakati Wafanyakazi wanahamasishana kuchagua viongozi bora. Tueleweje? "
 
Back
Top Bottom