Ni zipi Faida za kwenda JKT?

Ni zipi Faida za kwenda JKT?

Hamna kitu, kama zaidi ni kung'atwa na chawa tu na kuzoea mazingira machafu sana. Uzinzi njenje, upende usipende hasa kwa mabinti. Labda wakati Israel alipoanzisha lilikuwa na maana. Lakini mazingira niliyopita wakati wangu duhhh. Zoezi langu la Karate lilikuwa bora kuliko hiyo JKT.
Kwa maandishi yako unaonyesha hujawahi pita mafunzo ya JKT,askari muda wote anatakiwa kuwa msafi kuanzia mwili,mavazi mpaka unapolala, ndiyo maana kuna parade. Kuhusu uzinzi,zaidi kwa wasichana,napenda kukujulisha kwamba ni mabint wapenda dezo ndio walikua wanajirahisisha kwa maafande,mabint wachapa kazi na wanao jiheshimu tulikua tunakomaa nao kwa kila jambo. So siyo unakalia kusikiliza stori za uwongo!
 
Wanatumia mamilioni JKT halafu vijana wakitoka hapo serikali inasema haina pesa za kuwakopesha kwenda vyuo vikuu.
 
umepotea miaka 3 chuo kikuu hujaajiriwa alafu ukapoteze miaka 3 tena jkt usiajiriwe ukitoka hapo una miaka 30 huna ulichochuma lazima utakuwa jambazi tu.
 
Ukibet kuna kuliwa na muhindi au wewe kumla muhindi.
Ndio sawa na kwenda jkt(kujitolea), unasaini mkataba wa miaka 2 na sharti kubwa ni kwamba jkt haiajiri.
Ukibahatika kupata ajira unashukuru Mungu na ukikosa unarudi kwenu.

Kwa wale wanaokwenda kama kozi ya compulsory (mujibu wa sheria) naona wengi wao wanapata double loss, wanaumia for nothing, definitely hakuna wanachopata na kuongeza hasara serikalini. Anapiga kozi miezi 3 then anaenda chuo anakosa mkopo, anapotaka kurudi jeshini ili apate ajira anaambiwa haruhusiwi kupiga kozi ya jeshi zaidi ya mara moja, hapo atadanganywa asubiri utaratibu unaandaliwa ujue ndo imetoka hiyo, na aliyepata mkopo akimaliza chuo hana nafasi tena ya ajira akitaka kuingia haruhusiwi kwakua kashapitia jkt, kuna yule aliyefeli form 6 na kashamaliza jkt, hana nafasi ya kuingia jkt na hana kazi lakini amepata mafunzo ya kivita na matumizi ya silaha
shauri yenu nawaambia mtakuja kujilaumu sana mlioanzisha huo utaratibu)

Yote kwa yote hakuna mtu anapenda kwenda kuteseka ila kuna wakati inabidi tu kwa sababu ya umasikini wetu.
 
Nakiri kwamba faida ya JKT hii mpya kwa wabunge hata mimi sioni. Kwa nielewavyo JKT ni Sehemu ambapo vijana hujifunza
  • Nidhamu
  • Uvumilivu
  • Ukakamavu
  • Umoja
  • Uzalendo/utaifa
  • Kujitegemea
  • Heshima kwa watu bila kujali tabaka la kiuchumi
Hizo Faida za JKT ulizozitaja hatuzioni Kwa viongozi Wetu na wengine wanaongoza taasisi mbalimbali. JKT haikuwa na impact kabisa kwao. Wabinafsi, si wazalendo, mafisadi n. K.
 
hapo juu umelist vizuri faida za kijana aliye pitia JKT anatakiwa kuwa,hizi issues za ufisadi na kukosa uzalendo kwa baadhi ya watu waliopita JKT isiwe kigezo cha kuhukumu maelfu ya Watanzania waliopita mafunzo hayo kwamba kwamba siyo wazalendo,ni kupoteza muda na rasilimali za nchi. Kwa maoni yangu JKT ni muhimu zaidi sasa kama sehemu ya kuwaunganisha vijana wa Tanzania ambao wametenganishwa ktk matabaka elimu,shule za kata na academy. Ningependa hata itengenezwe programu maalum kwa watumishi wa serikali,taasisi na mashirika ya umma ambao hawakupitia mafunzo haya,wapelekwe huko sasa! Inaweza ikawa ni programu ya miezi mitatu kwa intake.
Haki haki Haki. Haki ikitolewa ktk sekta Zote uzalendo, kuheshimiana kunakuwepo automatically.hizo fedha za JKT zijenge hospitali tu. Wekeni JKT halafu Haki iwepo mtaani. JKT Hii ni sawa na kuoga kwenye mchanga bila viatu.
 
Nimejaribu mno kujaribu kuelewa faida za watu waende kujiunga JKT SIJAZIONA. Na nimejaribu sana kuona faida za wabunge nao kujiunga na mafunzo ya JKT sijaona!

Wanasema eti wanafundishwa uzalendo? Seriously? Uzalendo unafundishwa JKT kwa miezi hiyo michache?

Binafsi naona hasara kwa Taifa:

Kwanza pesa za walipa kodi zinazotumika, Pili JKT ni PIKNIKI tu fulani kwani nionavyo mimi haina tofauti na watoto wa shule ya msingi na skauti.

Sanasana kuna hatari ya kuandaa majambazi kwa kupitia hayo mafunzo! Watu watakuwa majasiri while hawana ajira so watajikuta wana skillz za kufanyia ujambazi na kwa wabunge wanachopata ni cheap publicity tu as if wamefanya la maana saana; ni ujinga mtupu....
The boss the boss the boss the boss
 
Faida au hasara ni suala la muda bc what is true today may be wrong tomorrow. Tatizo lililopo tumekariri Yale ya miaka ya 60 Kama kufukuza mwenge. Mambo mengine yamegeuka imani na hayo kuabudiwa.
 
Nothing other than Loyalt and patriotism which are very important for maintanace of peace we have..
 
Back
Top Bottom