Katika hali isiyo ya kawaida huko Zanzibar watu wengi wamefurika na wamehudhuria mhadhara ya kupinga muungano uliofanyika viwanja vya Lumuba mjini Zanzibar na hivyo kupelekea mpaka Polisi nao kushiriki katika uchukuaji picha za video katika mhadhara huo.
Kwa kweli Wazenji wamevunja ukimya na kuiweka SMZ katk hali ngumu ya mchakato wa katiba mpya licha ya kuwa kuna polisi wengi waliopelekwa kutoka Tanganyika kwa hofu ya kutokea fujo.
Naikumbuka picha hii ni kutoka moja ya mikutano ya CUF mwaka 2000 wewe unaileta hapa ?
Nani sasa alikuwa anahesabu mikono ya wasioutaka? Halafu mbona wamenyoosha mikono miwili miwili, haiwezi ikawa dalili ya kuwa wasioutaka ni wachache?Leo Lumumba hali ilikuwa hivi jee Muungano mnautaka au hamuutaki? hilo ndio jibu la wa Zanzibari hapo wasioutaka wanyooshe mikono .
a maana karume alikuwa hujui kusoma au ?
naunga mkono kutengana na wazanzibari... wamechakachuliwa sana na CCM kwenye chaguzi tatu zilizopita, wakikaa kimya basi ni mabwege
walau wao wanapinga hii kitu wazi wazi
sie tumekuwa waoga kama panya vile
CHADEMA toeni tamko kuhusu hili
swali la kizushi
hati za muungano kwa nini zinafichwa?
kwa niin sherehe za muungano hazifanywi zanzibar?
Bado wanaukubali Muungano. Wanajadili chini ya Picha ya Rais wa Jamhuri ya Muungano. Muungano wa Tanz Bara na Zanzibar ukishavunjika unaofuatia ni ule wa Pemba na Unguja kwa sababu Zanzibar ni muungano wa Pemba na Unguja na ndio maana kule kuna Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar(SMZ) na hakuna Serikali ya Pemba.
Wanaitaka nchi "yao" ya Zanzibar; Wanataka kurudia "utukufu wa Zanzibar" kwa kuwa hapa walipo sasa hawaoni manufaa "yoyote" kwa Zanzibar. Wanasema wanaitaka nchi yao waliyonyang'anywa na Wadanganyika (ati Watanganyika). Wanataka warudishiwe nchi yao waliyonyang'anywa na Nyerere na watu wa bara.
Ni Zanzibar ipi hiyo wanayoitaka?
Ni ipi hasa wanayoitaka? Ni ipi hasa Zanzibar "proper". Isije kuwa ni kama nchi ya ahadi ambayo iko katika fikra za watu tu lakini haijawahi kuwepo; yaani ile nchi imiminikayo maziwa na asali na kwamba watu wa bara na dunia nzima wanataka kuwanyang'anya Wazanzibari.
- Zanzibar ya historia ya kale (Zenj - nchi ya weusi?) ambayo ni zaidi ya visiwa vya Unguja na Pemba bali na mwambao wa Afrika ya Mashariki
- Zanzibar ya Sultani(ambaye naye utawala wake ulizidi mipaka ya Unguja na Pemba)
- Zanzibar ya Sultani chini ya Mwingereza
- Zanzibar ya baada ya Uhuru na Sultani akiwa bado ni Mkuu wa Nchi na serikali ya Mseto
- Zanzibar ya Mapinduzi kabla ya Muungano
- Zanzibar "mpya" ambayo haijawahi kuwepo yaani ya baada ya muungano
Na labda hapa itabidi tulijibu swali pia kuwa Mzanzibari ni nani hasa?
Tunataka Zanzibar ya Wazanzibari ambyao itajiamulia Mambo yake na Haitachaguliwa mamluki kutoka DodomaWanaitaka nchi "yao" ya Zanzibar; Wanataka kurudia "utukufu wa Zanzibar" kwa kuwa hapa walipo sasa hawaoni manufaa "yoyote" kwa Zanzibar. Wanasema wanaitaka nchi yao waliyonyang'anywa na Wadanganyika (ati Watanganyika). Wanataka warudishiwe nchi yao waliyonyang'anywa na Nyerere na watu wa bara.
Ni Zanzibar ipi hiyo wanayoitaka?
Ni ipi hasa wanayoitaka? Ni ipi hasa Zanzibar "proper". Isije kuwa ni kama nchi ya ahadi ambayo iko katika fikra za watu tu lakini haijawahi kuwepo; yaani ile nchi imiminikayo maziwa na asali na kwamba watu wa bara na dunia nzima wanataka kuwanyang'anya Wazanzibari.
- Zanzibar ya historia ya kale (Zenj - nchi ya weusi?) ambayo ni zaidi ya visiwa vya Unguja na Pemba bali na mwambao wa Afrika ya Mashariki
- Zanzibar ya Sultani(ambaye naye utawala wake ulizidi mipaka ya Unguja na Pemba)
- Zanzibar ya Sultani chini ya Mwingereza
- Zanzibar ya baada ya Uhuru na Sultani akiwa bado ni Mkuu wa Nchi na serikali ya Mseto
- Zanzibar ya Mapinduzi kabla ya Muungano
- Zanzibar "mpya" ambayo haijawahi kuwepo yaani ya baada ya muungano
Na labda hapa itabidi tulijibu swali pia kuwa Mzanzibari ni nani hasa?
Hiyo kaidai OmanTunataka Zanzibar ya Wazanzibari ambyao itajiamulia Mambo yake na Haitachaguliwa mamluki kutoka Dodoma