Huku mitaani naishi na wznz, hawa ni watu wa kawaida na wanaendesha maisha yao bila wasi wasi, wao muungano ni sehemu ya neema kwani wakienda bahari wanaleta pweza, wakirudi znz wamebeba viazi, watoto wanakwenda shule wanatibiwa n.k. kundi hili hawaoni Znz ya pepo yenye mito ya maziwa na asali bali Znz ya juhudi zao na fursa ya muungano.
Kuna kundi la wale waliosoma vitabu na kuamini kuwa Znz ya enzi hizo ilikuwa ni bora sana, znz ya sultani kwani tende, halua na mchele vilipatikana bure kutoka uarabuni. Kundi hili linaungwa mkono na wafanyabiashara kutoka uarabuni wanaotaka kurejesha usultan kwani nao wanatamani zama za usulatan wao a.k.a znz yao.
Wapeleke mswaada wa kura ya maoni ili warudishe nchi ya neema, nchi ya kusadikika, yenye mito ya asali, na mabwawa ya maziwa.
Mkuu ndipo hoja ilipo, wanaweza kufanya bila matusi, kashfa na dharau wakifahamu kuwa muungano umekuwa na faida, kama hakuna haja ni vema kuachana kwa amani. Na suala la kura ya maoni lipo ndani ya uwezo wao na si internet,=Nonda;1889565]!
Bora jamaa warudishiwe sovereignty yao
Hakika kati ya wau waliohoji sana muungano nipo.Hoja yangu ilikuwa ni muungano uangaliwe upya kwani malalamiko yalikuwa pande zote,kama haiwezekani basi uvunjwe kwa amani. Unakumbuka G55 ya jenerali na Njelu kasaka?sasa kuna vijana wa utandawazi, wa internet na twitter, wametembea ,wanaona mambo, wanasoma...kizazi kipya kina madai yake na si vyema kupuuzwa....wimbi la mageuzi limeshika kasi hata kama tutajaribu kulizuia litakuwa ni suala la muda tu.
.sasa kama wazanzibari wanaufananisha muungano na uvamizi au kutawaliwa basi hakuna lugha itakayowapoza mpaka watakapopata wanachokitaka
Shirikisho lishughulikie mambo gani? mbona hakuna anayetuambia yapi yawe ya shirikisho? na watachangia nini?Ni wazi wao wanataka ama shirikisho na sio unitary union au wanataka Zanzibar ya asali na maziwa kama unavyoiita.
!Nafikiri mpira wameturushia sisi kaka viranja
Ndiyo maana watu wamekataa mswada ulioletwa bila muungano kujadiliwaMimi sifahamu kwa nini serikali inakataa mjadala wa wazi juu ya muungano na muundo wake? Muungano huu haujawahi kufanyiwa review, sisi tunauimarisha tu bila ya kujua wananchi wetu wanauonaje, faida na hasara zake.
Haswaa ilipaswa iwe hivyo, lakini wazanzibar wameshatoa hukumu hata kabla ya mjadala, sasa mjadala utasaidia nini, wao wanasema wameonewa bila kutaja hata chembe ya jema. Hili ndilo linatia hasira tukijua kuwa rasimali za bara na hata upendeleo maalumu umefanyika lakini fadhila zake ni matusi.Mimi nazungumzia mjadala wa kitaifa,Watu walio na Muungano fuctional, ambao wanaona faida yake hawalalamiki wala kupiga mayowe bana?
Mkuu ndipo hoja ilipo, wanaweza kufanya bila matusi, kashfa na dharau wakifahamu kuwa muungano umekuwa na faida, kama hakuna haja ni vema kuachana kwa amani. Na suala la kura ya maoni lipo ndani ya uwezo wao na si internet,
kinachowashinda nini?
Hakika kati ya wau waliohoji sana muungano nipo.Hoja yangu ilikuwa ni muungano uangaliwe upya kwani malalamiko yalikuwa pande zote,kama haiwezekani basi uvunjwe kwa amani. Unakumbuka G55 ya jenerali na Njelu kasaka?
.
Ndiyo maana tunawashauri wapeleke mswada BLW ili kuanzisha mchakato wa kuvunja muungano, hilo hawataki wanataka serikali ya Tanganyika ili iwepo serikali ya shirikisho. Wanajua kuna faida lakini element za unafiki ndizo zinawachanganya.
Shirikisho lishughulikie mambo gani? mbona hakuna anayetuambia yapi yawe ya shirikisho? na watachangia nini?
!
Mpira wanao wao,kwasababu Tanganyika hawahitaji kura ya maoni, wapo tayari kwa lolote, na kura ya maoni labda iwe Ilala dhidi ya Znz kuleta usawa.
Ndiyo maana watu wamekataa mswada ulioletwa bila muungano kujadiliwa
Haswaa ilipaswa iwe hivyo, lakini wazanzibar wameshatoa hukumu hata kabla ya mjadala, sasa mjadala utasaidia nini, wao wanasema wameonewa bila kutaja hata chembe ya jema. Hili ndilo linatia hasira tukijua kuwa rasimali za bara na hata upendeleo maalumu umefanyika lakini fadhila zake ni matusi.
Hii mada inanigusa kama mwananchi,namshukuru mungu, nimeishi sehemu nyingi sana duniani. Nimeishi na wznz kwao na hapa bara, ninajua malalamiko ya pande zote na faida zitokanazo.
Tatizo kwa wznz, wengi wanaimba nyimbo, hawajui tungo zake zina maana gani, Hawawezi kujibu maswali rahisi kwasababu wamekaririshwa ujio wa nchi ya ahadi, yenye matunda ya dhahabu, visima vya maziwa, mito ya asali,hewa ya jasmini na sinia za biriani barabarani.
Wamekariri toka kwenye hekaya na ngano za watunzi tofauti na leo hawajui mapinduzi ni halali au haramu.
Znz wafikishe mswada wa kujitenga baada ya pasaka ikiwezekana ili warejea kwao tayari kula matunda ya misaada na visa ya Oman.!!!(ref. mzalendo.)
Mzizimkavu nje ya muungano kuna "Sisi Wapemba wao waungunja" hakuna Zanzibar...Muungano ndo unafanya kuwepo na Zanzibar...
Hapo Zamani kulikuwa kuna Chama kinaitwa ZANZIBAR AND PEMBA PEOPLE'S PARTY (ZPPP). hivi kwani Pemba siyo sehemu ya Zanzibar?, kwa nini hicho chama hakikuitwa ZANZIBAR PEOPLE'S PARTY?.
Dah, napata taabu kidogo kujadili, nahisi kama nimeingia mzalendo.net.
Anyway, hivi jina lina uhusiano gani kiuchumi,kisiasa au kiutamaduni. Kwamfano Tanganyika ikibadili jina na kuwa Tanga then so what.
Burma wanajiita jina jipya inawasaidiaje. Hata sasa hivi Tanzania ni Tanganyika kwasababu Zanzibar haijiiti Tanzania ikiwa ni pamoja na ninyi wachangiaji.
Tafadhali kama huna hoja za kufikirisha, rejea mzalendo.net kwasababu JF inakuwa level ya juu kidogo. Usishushe hadhi ya mjadala kwa hoja rojo rojo. Please
Serikali tatu zishughulikie nini? ni mambo gani unadhani seriakali ya shirikisho inapaswa kuyashughulikia, fafanua kwasababu neno tatu halijatusaidia kukuelewa.
My take: Post zilizopita nimewahi kusema wazanzibar wanataka Tanganyika irudi ili wajenge hoja kuwa tuwe na shirikisho tofauti na unafiki wa kusema eti wanataka Tangnayika kwani ndiyo inawashikilia. Sasa wanakuja na siri tuliyoijua mapema.
Tanganyika haihitaji maoni, mzigo wa muungano upo kwa Wznz, kuamua kunyoa au kusuka.
Serikali tatu hapana hadi watakaposema mambo gani yawe ya seriakali tatu kwanza.
Serikali tatu ni kubebesha mzigo bara kwasababu wao watachangia nini kwa bajeti ya bilioni 500.
Serikali tatu maana yake kuwasaidia kwa yale wanayonufaika ndani ya muungano.
Kura ya maoni ndiyo itaamua hatma ya nchi ya matunda, asali na maziwa Zanzibar.
Makaimati, dhambi ya ubaguzi haitaishia hapo...baada ya kujitenga hamtaishia hapo,mtakuja na sisi wapemba na wao waunguja! Then Mimi wa kusini Unguja,mimi wa mji mkongwe na mwishoni utakua umesimama mwenyewe!...sijasema muungano uendelee kuwepo na sijasema pia uvunjike!...
Mtoto akililia wembe mpatie acheze nao halafu umkate,gari kama engine inasumbua dawa ni kuishusha chini na ku overhaul pia unaweza
kununua engine mpya ukaweka mambo yakasonga mbele vizuri zaidi nasi Muungano wetu napendekeza uvunjwe halafu tuzungumze upya kila nchi ikiwa huru zaidi naamini baada ya hapo tutahashimiana.
Yaani zanzibar ya ki-oic na ile ya kimahakama ya kadhi.......................
Wanaitaka nchi "yao" ya Zanzibar; Wanataka kurudia "utukufu wa Zanzibar" kwa kuwa hapa walipo sasa hawaoni manufaa "yoyote" kwa Zanzibar. Wanasema wanaitaka nchi yao waliyonyang'anywa na Wadanganyika (ati Watanganyika). Wanataka warudishiwe nchi yao waliyonyang'anywa na Nyerere na watu wa bara.
Ni Zanzibar ipi hiyo wanayoitaka?
- Zanzibar ya historia ya kale (Zenj - nchi ya weusi?) ambayo ni zaidi ya visiwa vya Unguja na Pemba bali na mwambao wa Afrika ya Mashariki
- Zanzibar ya Sultani(ambaye naye utawala wake ulizidi mipaka ya Unguja na Pemba)
- Zanzibar ya Sultani chini ya Mwingereza
- Zanzibar ya baada ya Uhuru na Sultani akiwa bado ni Mkuu wa Nchi na serikali ya Mseto
- Zanzibar ya Mapinduzi kabla ya Muungano
- Zanzibar "mpya" ambayo haijawahi kuwepo yaani ya baada ya muungano
Ni ipi hasa wanayoitaka? Ni ipi hasa Zanzibar "proper". Isije kuwa ni kama nchi ya ahadi ambayo iko katika fikra za watu tu lakini haijawahi kuwepo; yaani ile nchi imiminikayo maziwa na asali na kwamba watu wa bara na dunia nzima wanataka kuwanyang'anya Wazanzibari. Na labda hapa itabidi tulijibu swali pia kuwa Mzanzibari ni nani hasa?
Kwa hiyo? kwa nini msifanye maandamano mbaki na nchi yenu mfe njaaHayo mtajua wenyewe wala haituhusu, sisi tunataka Zanzibar yetu ambayo tutaweza kujiamulia mambo yetu.
Mahkama za Kadhi zipo Zanzibar toka dahari na imo ndani ya Katiba yetu.
OIC ni fitna zenu maana hata Msumbiji ni member.
Huo uhasidi na uchoyo wenu kwa Zanzibar ndio iliotufikisha hapa tulipo.
"If I could tow that island out into the middle of Indian Ocean, Id' do it." - JK Nyerere.
Wasiongee ongee tu wafanye kwa vitendo tangu wameanza kulalamika ni lini tulisikia kundi fulani limeanzisha hoja hii ili kushinikiza viongozi wao waombe huo uhuru?wazenj wanataka nchi yenye uhuru zaidi, wanataka mipaka yao itambulike rasmi, wanataka maendeleo yao bila kupitia upande wa pili