Mkuu kimsingi hakuna staili inayoitwa "combat karate"...ile wanayofundishwa jeshini ni baadhi tu ya mafunzo ya staili fulani. Yaweza kuwa shotokan au goju ryu pamoja na vitu vichache vya aikido au jiujitsu.
Pili hakuna sanaa ya mapigano ambayo ni bora zaidi ya nyingine. Msanii ndio huwa bora. Ni kama sanaa ya muziki. Haijalishi unaimba muziki gani, wewe kama msanii ndio waweza kusababisha muziki wako kupendwa au kuchukiwa.
Nitatoa mfano wa wasanii wa sanaa ya mapigano walio shawishi watu kujifunza baadhi ya sanaa zao:
Jackie Chan-Kungfu(Drunken & Snake)
Bruce Lee-Jeet Kune Do
Jet Lee-Wushu
Van Damme-Shotokan Karate
Tony Jaa-Muai Thai & Tae Kwon do
Scott Adkin(Boyka)-Kick Boxing&Tae kwon do
Shoku Sugi-Ninjitsu
Steven Seagal-Aikido
Donie Yen-Judo,Wushu & Wing chun
Hao ni baadhi tu. Leo hii kuna maelfu ya watu wanaojifunza hizo sanaa kwa ushawishi wa hao watu.
Kwa hiyo haijalishi utajifunza sanaa gani ila wakati wote kumbuka kuwa,'Sanaa haimfanyi mtu bali mtu ndiye huifanya Sanaa'.
Kila lakheri.