Tunakoelekea, ni Mungu tu aepushie mbali! Haitafahamika ikiwa watanzania tutakuwa tunaishi kwenye nchi yetu wenyewe ama ni ugenini! Mungu saidia
Na ikitokea kura zinapigwa kesho, wenye kumpa kura kwa sasa ni hao walamba asali tu!
Ni vigumu sana kukubaliana na ukweli huu!
Na bahati mbaya kabisa hata wale wanaomfanyia utafiti mama kwa kiasi gani anakubalika kwa wananchi, wapo tu maofsini wamelewa asali!
Na hata wakienda kufanya utafiti, bado watamletea majibu ya kuongopa ili tu waendelee kulewa asali kama kawaida yao!
Ndugu zangu! Si mkulima wala asiyemkulima anayenufaika na upandaji wa mazao kwa sasa!
Jambo hili limemchukiza kila mtu, siyo mkulima wala mlaji! Wote wanahasira nalo! Baba makini na mwenye uchungu na watoto wake, hakurupuki, akisikia watoto wake kulalamikia jambo fulani, hufuatilia kuona ukweli wa jambo hilo!
Nalimuelewa vema Dkt Bashiru kwenye hoja yake kuhusu bei juu ya mazao, na kwamba serikali ifanye ubunifu wa kukabiliana na hali hii mbaya, na akatoa mfano hai kusema, Ikiwa wananchi wamebuni mbinu zao za kukabiliana na hali hii kwa kupanga upya ratiba ya Milo, iweje serikali ikose ubunifu na mbinu mbadala wa kutatua jambo hili?
Hivi mnajua tsh 5000 haitoshi kula mtu mmoja? Na ndiyo maana kwa kulijuahilo, yeye mwenyewe amewaongezea wanafunzi wa vyuo kufika bajeti ya kujikimu kwa siku, kufikia tsh 10,000 ya kula!
Kwa mantiki hiyo hiyo, pesa ya kula kwa mtu mmoja kwa siku inafikia kiwango hichohicho kwa kila raia na sio kwa wanafunzi wa vyuo pekee, Je ukiangalia katika uhalisia, hicho ndicho kipato kweli cha mtanzania? Kwa haraka haraka ni hakuna!
Sasa wananchi wananchi wanaishije ikiwa hawana uwezo wa kipato cha Tsh 10,000 kwa siku? CCM mmelaka mkiwa mmelewa asali ili hali wananchi wanashinda njaa?
Kwa nini ukweli huitwa uchochezi kwa watu wasiojua machungu ya wananchi kwa wanayoyapitia?
Kwa hali kama hiyo? Ni mpuuzi nani wa kutoa kura yake Ili aendelee kuishi kama digidigi mbugani
Nimeongelea moja tu ambapo wananchi wengi wameweka hasira zao ili kulipiza 2025
Mitaani kumekuwa na vichaa wengi sana wa kiume, na ukiuliza ni vipi imekuwa hivyo! Watu wanaeleza tu kuwa imetokea mtu ameshindwa kuitunza familia yake, maisha yamekuwa ni magumu na hatimaye mtu anaanza tu kuongea mwenyewe njiani kisha kuokota makopo na uchizi tayari unamvamia
Hakuna kipindi chochote kile katika nchi hii ambapo watu wanasafa kuliko hata mbwa wakitafuta malisho
10000 kwa sasa ni sawa na una buku 2000 haitoshi kwa lolote!
Hivi tuambizane ukweli, ni mtu nani jasiri wa kutoa kura yake kurudia mateso kama haya?
Ombi kwa vituo vya afya! Anzeni mapema sasa kupima watoto ikiwa hawana utapia mlo, hali ni mbaya
Na kwa nini mnadhani ni vibaya kuusema ukweli ili kuchukua hatua?
Na ikitokea kura zinapigwa kesho, wenye kumpa kura kwa sasa ni hao walamba asali tu!
Ni vigumu sana kukubaliana na ukweli huu!
Na bahati mbaya kabisa hata wale wanaomfanyia utafiti mama kwa kiasi gani anakubalika kwa wananchi, wapo tu maofsini wamelewa asali!
Na hata wakienda kufanya utafiti, bado watamletea majibu ya kuongopa ili tu waendelee kulewa asali kama kawaida yao!
Ndugu zangu! Si mkulima wala asiyemkulima anayenufaika na upandaji wa mazao kwa sasa!
Jambo hili limemchukiza kila mtu, siyo mkulima wala mlaji! Wote wanahasira nalo! Baba makini na mwenye uchungu na watoto wake, hakurupuki, akisikia watoto wake kulalamikia jambo fulani, hufuatilia kuona ukweli wa jambo hilo!
Nalimuelewa vema Dkt Bashiru kwenye hoja yake kuhusu bei juu ya mazao, na kwamba serikali ifanye ubunifu wa kukabiliana na hali hii mbaya, na akatoa mfano hai kusema, Ikiwa wananchi wamebuni mbinu zao za kukabiliana na hali hii kwa kupanga upya ratiba ya Milo, iweje serikali ikose ubunifu na mbinu mbadala wa kutatua jambo hili?
Hivi mnajua tsh 5000 haitoshi kula mtu mmoja? Na ndiyo maana kwa kulijuahilo, yeye mwenyewe amewaongezea wanafunzi wa vyuo kufika bajeti ya kujikimu kwa siku, kufikia tsh 10,000 ya kula!
Kwa mantiki hiyo hiyo, pesa ya kula kwa mtu mmoja kwa siku inafikia kiwango hichohicho kwa kila raia na sio kwa wanafunzi wa vyuo pekee, Je ukiangalia katika uhalisia, hicho ndicho kipato kweli cha mtanzania? Kwa haraka haraka ni hakuna!
Sasa wananchi wananchi wanaishije ikiwa hawana uwezo wa kipato cha Tsh 10,000 kwa siku? CCM mmelaka mkiwa mmelewa asali ili hali wananchi wanashinda njaa?
Kwa nini ukweli huitwa uchochezi kwa watu wasiojua machungu ya wananchi kwa wanayoyapitia?
Kwa hali kama hiyo? Ni mpuuzi nani wa kutoa kura yake Ili aendelee kuishi kama digidigi mbugani
Nimeongelea moja tu ambapo wananchi wengi wameweka hasira zao ili kulipiza 2025
Mitaani kumekuwa na vichaa wengi sana wa kiume, na ukiuliza ni vipi imekuwa hivyo! Watu wanaeleza tu kuwa imetokea mtu ameshindwa kuitunza familia yake, maisha yamekuwa ni magumu na hatimaye mtu anaanza tu kuongea mwenyewe njiani kisha kuokota makopo na uchizi tayari unamvamia
Hakuna kipindi chochote kile katika nchi hii ambapo watu wanasafa kuliko hata mbwa wakitafuta malisho
10000 kwa sasa ni sawa na una buku 2000 haitoshi kwa lolote!
Hivi tuambizane ukweli, ni mtu nani jasiri wa kutoa kura yake kurudia mateso kama haya?
Ombi kwa vituo vya afya! Anzeni mapema sasa kupima watoto ikiwa hawana utapia mlo, hali ni mbaya
Na kwa nini mnadhani ni vibaya kuusema ukweli ili kuchukua hatua?