Ni vibaya binti kumnunulia baba yake boxer?

Ni vibaya binti kumnunulia baba yake boxer?

ameline

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2013
Posts
2,292
Reaction score
1,152
Wana MMU naombeni msaada wa ushauri..
Kabla sijaoewa nilikua na tabia ya kuwanunulia wazazi wangu zawad mbalimbali..mfano nikimnunulia mama vitenge au makatalogi yaliyotoka baba nae humnunulia mashati, suruali, viatu, mikanda n.k nikinunua underware za mama na nguo nyingine za ndani bas na baba namnunulia vilevile boxerz, pants,vest n.k na huzipeleka kwa pamoja..walikua wameshazoea na kuzifurahia zawad..na nilifanya hivi kwa muda mrefu tu na nlikua sina ubaguz wa mzaz yeyote.wote wanapata.
baada ya kuchumbiwa pia sikuacha hata mchumba wangu aliona wakat nanunua zawad.hizo na wakat mwingine tunachagua wote nae akimnunulia.mama yake.

Baada ya.kuolewa sasa..siku moja nikanunua kama kawaida makadet na mashati pamoja na nguo za mama na wakwe zangu kama zawadi nikamwita mdogo wangu aje dukani kuchukua za wazaz wangu awapelekee.sasa rafiki yangu nliekua nae akanambia unafanya nini? unamnunulia babako nguo mpaka leo? wewe mke wa mtu acha mke wake (mama yangu) amnunulie! hutakiwi kumnunulia tena! mnunulie mama tu! mh na.maneno mengi tu aliongea yaliyonikatisha tamaa mpaka ikabidi nisitishe zawad hizo mpaka leo sijawahi tena kuwanunulia sio baba wala mama kwani naogopa kumpa mama bila baba kwani nilishazoea kuwapa wote.

Nauliza jamani;: kuna ubaya wowote kwa binti alieolewa kumnunulia baba yake zawadi kama nguo na nguo za ndani n.k?
sina amani najisikia vibaya kwani wazaz wangu wataona nimewatelekeza tangu niolewe hakuna zawadi tena..naombeni mnisaidie wale wenye uzoefu na haya mambo jamani.
 
ameline huo unaitwa upendo hukosei na unafanya kitu kikubwa sana, unawapenda wazazi wako na hiyo ni tabia njema. Hakuna tatizo lolote kwani wababa wangapi wanawanunulia binti zao pad?
 
Last edited by a moderator:
mamy ngoja waje mimi bado sijaingia ila naona mama yangu mpak aleo huwa anamnunulia baba yanke nguo lakini siyo za ndani
 
mmh!
baba mzazi unamnunulia boxer?
kwa huu usukuma wangu na malezi niliyokulia kwa kweli siwezi
 
hapana sio vizuri asee suala la bocer muachie mkewe(mama yako) ila zingime kama mashati,vest hizo ruksa kabisa
 
mmh!
baba mzazi unamnunulia boxer?
kwa huu usukuma wangu na malezi niliyokulia kwa kweli siwezi

mwenzio hata mimi sijakulia uzunguni..nimekulia uchagani ..mazoea tu ndugu
 
Kwani zawadi ni boxer peke yake hadi uhisi wazazi wako watajisikia vibaya kwamba huwanunulii zawadi

alivonishauri huyo dada mtu mzima ambae naweza kumwita mamdogo ni kwamba sistahili kumnunulia baba zawad yeyote kwani mim ni mke wa mtu napaswa kumnunulia mama tu na.mume wangu..ila sijamaanisha boxer tu
 
Mmmh boxer kwa mdingi?? Duu hata kwa kaka yangu siwezi!!nunua zawadi zingne bana siy lazima nguo za ndani
 
ameline huo unaitwa upendo hukosei na unafanya kitu kikubwa sana, unawapenda wazazi wako na hiyo ni tabia njema. Hakuna tatizo lolote kwani wababa wangapi wanawanunulia binti zao pad?

ila sasa mimi nimeolewa ndugu..baba pads alitununulia sana wakati.tunasoma tena sekondari..ile nliambiwa hain shida hata nlivofanya vile kabla sijaolewa..tatizo ni sasa nishaolewa eti baba hastahili zawadi.zangu.tena?
 
Last edited by a moderator:
Kwani zawadi ni boxer "NGUO" peke yake hadi uhisi wazazi wako watajisikia vibaya kwamba huwanunulii zawadi

Kwani zawadi ni "NGUO" peke yake hadi uhisi wazazi wako watajisikia vibaya kwamba huwanunulii zawadi
 
mmh!
baba mzazi unamnunulia boxer?
kwa huu usukuma wangu na malezi niliyokulia kwa kweli siwezi
Mmh!sio wasukuma tu hata mie naona ajabu kumnunulia baba yangu boxer!pamoja na kwamba nimekulia mazingira ya mjini!sijawahi kufanya hivyo hadi sasa nimeshazeeka. Wala kufikiria kumnunulia baba boxer maishani sijawahi!
Au labda kwa kuwa nina kaka wengi!
 
Back
Top Bottom