Kuna topic tayari inazungumzia ufisadi wa Sitta ambayo ilitetwa na GT. Pitia huko ndiyo utajua. Ufisadi siyo EPA, Richmond na Kagoda tu. Kama Spika anatumia UDS 8000 kwa mwezi kulipia nyumba, thamani za ndani Tshs 250 million then nafikiri utajaza mwenyewe.......!!!!!!!!!!!!!!
Lakini Tanzania Daima wameqoute waraka uliosambazwa,hata wememqoute mwenyewe kwamba amesema ni wa kipuuzi uzushi na chuki ,kwa hiyo mwanzisa thread hii analojambo anapo link majibu ya Spika na kushushuliwa kwa Gazeti. Spika siangeona imekuwa vizuri gazeti limeweka peupe waraka unaosambazwa .ni hiari yake kuudharau kama hauna ukweli ndani yake au kuusimamisha kwa kuutolea maelezo haitoshi tu kusema maadui zake wanamuwinda yeye ni kuueleza umma ukweli ni upi jamii inatabia yakuamini roumors apende asipende atakuwa na maadui wengi kwa sababu umekuwa mtindo wa CCM sasa hivi kuuana wenyewe kwa kutumia vyombo vya habari utakuta akina Mkapa akina Sitta na wengine na wengine,hatusomi tena habari za maendeleo ya nchi kila siku ni matatizo tuu hali hii inaudhi sana.
Kama ni msomaji mzuri wa magazeti utakuwa umegundua kwamba Tanzania Daima ndilo limekuwa likiandika sana habari chafu dhidi ya Spika, bila kujali chanzo cha habari hizo. Kutaka maoni yake ni kuhalalisha tu habari zao na ndivyo wanavyoelekezwa na hao mafisadi wanaowatuma. Nani asiyejua kwamba kuna watu wana kisasi na Spika?
Hivi hao waliotuhumu mbona hawakutuletea vielelezo? Tumewaamini kwa maneno yao tu, kwa nini na huyu tusimwamini kwa maneno yake tu? Sheria zetu zifauata principle ya commonweath-You are innocent until proved guilty. Let the accusers prove that Sitta is guilty kabla hatujamkondemn mzee wa watuJambo la msingi kwa mzee wetu huyu ni kueleza upande wa pili ambao anaamini kuwa ndio sahihi na akithibitisha kwa vielelezo.
hivi anatumia viagra au kuna mizizi ya kinyamwezi anaweza kweli kuwa nao wanawake kumi ,atupe hizo skills basi
Pitapitia thread utaona kuwa ufisadi wa Sitta pia ushajadiliwa humu. Unless unataka kusema GT ni mmoja wa wafanyakazi wa Tanzania Daima.
Kodi USD 8000 kwa mwezi, fenicha za Tshs 250 m?? need to say more????
hii ndio sababu ya yote hayo??Spika Sitta amekula akilazimisha kukiukwa kwa kanuni za bunge ili tu kuwapa nafasi wabunge wenzaki walio katika kambi moja kuisulubu serikali ili kuwaaminisha wananchi serikali ni ya hovyo bali yeye na wabunge hao ndiyo wana uchungu wa kweli na taifa hili.
Anatumia vyombo vya umma kufanya ufuska
Baada ya kuchoshwa na tuhuma nyingi zinazoelekezwa kwake kupitia magazetini, muda mfupi uliopita spika samwel sitta amesema tuhuma hizo zinapikwa na watu wasiompenda wakiyatumia magazeti ya tanzania daima na tazama. Huko nyuma tuliwahi kusikia kuwa wahariri wa gazeti la tanzania daima (absalom kibanda na charles mulinda) wamenunuliwa na mafisadi wakiongozwa na r.a. Ili kuwashambulia maadui zao, akiwemo spika sitta. Hawa wamekuwa pia wakilitumia pia jamvi hili la jf kupenyezaa upuuzi wao. Akizungumza kwa kujiamini spika ameonyesha kukerwa zaidi na tuhuma kwamba anapanga njama za kuchoma ofisi za bunge ili kuharibu ushahidi wa baadhi ya tuhuma. Sasa amemuomba waziri mkuu amuongezee ulinzi kwani anadhani watu hao ni hatari.