Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Kwani huyo CAG naye si Fisadi tu, mahesabu kibao ya serikali yanapotea na hatoi taarifa, huyo naye Fisadi tu

Mimi nadhani Zitto katoa mwanga .So yule mtoa mada tena alikuwa na posts kama 2 ama tatu .Inawezekana kaja na kazi maalumu .Pokeeni ushauri na tuone akija atasema nini .Ama kama yupo anasoma ajitokeze ajibu hoja za Zitto .
 
Hivi hii mada imeshikiliwa na watu wangapi? Muwekaji anabadilika kila mara halafu mada yenyewe sioni kama ina nguvu sana inaonekana kama inaweweseka kabisa.

Lakini wenye data zaidi ya hizi wekeni na pia imenifundisha kuwa Sitta SIYO FISADI wa kuhatarisha maisha ya Watanzania.
 
Mkuu Zitto heshima mbele lakini naomba kutofautiana na wewe katika masuala yafuatayo:

Maadili! maadili! maadili!.
Viongozi ni kioo cha jamii,wao kwa matendo yao wanapaswa kuwa mfano mzuri kwa wale wanaowaongoza. Kiongozi asiyeheshimu ndoa yake ataweza kweli kuheshimu ndoa ya mwenzake?, kiongozi wa namna hii anajenga misingi ya familia bora na taifa au anabomoa?

Katika challenge tunazokutana nazo katika nchi yetu, na balaa hili la Ukimwi hivi unaweza kusema Ngono nje ya ndoa siyo ishu kweli?, yaani kwamba maadam kiongozi hajaliibia Taifa lakini hata kama mwenendo wake unatishia mustakbali wa taifa kwa kulea tabia zinazokwaza mapambano dhidi ya ukimwi hiyo siyo ishu kweli?.

Tutakuwa tunajidanganya tukidhani tutaweza kuiweka jamii yetu katika msitari ulionyooka kama tunadhani tunaweza kupambana na matatizo tuliyonayo kinjenje tu bila ya kuangalia mtatizo ya kindnindani ambayo kila mmoja wetu anayo.Ishu ya kujiheshimu,kuheshimu mume/mke kuheshimu familia yako ni jambo la msingi sana.

Kwa nchi kama marekani ikidhibitika kwamba unakwenda nje ya ndoa hata kama wewe ni raisi huo ni msala mnene tena unaweza kuondoka hivihivi na kiti unakiacha hivi hivi.

Lazima tufikie hatua iwepo aibu ya yale tunayoyatenda, Kiongozi/au mtu kwenda nje ya ndoa ni jambo la aibu, na kwa kiongozi anayetakiwa kubeba mwenge wa kumulika njia ya wananchi kisiasa na kijamii inabidi aonyeshe njia bora.

Hivi tutapambana vipi na Balaa la ukimwi iwapo tunaona yale yanayokuza ukimwi siyo ishu?
 

Kuna jamaa aliileta hapa hii mada ikawa inafutwa na ndiyo maana nimeomba ibakie ili kuondoa hisia mbaya .Si umeona sasa Zitto kaja kasadia kuweka sawa mambo ? Kuna jamaa ana posts kama 2 tatu ndiye source wa hii habari .Mods wanajua vyema the name wanaweza kutusaidia .
 
Hii mada ni nzito na kanuni zangu nilizotumia na kuzisema wakati wa sakata la Amina na Zitto bado zinaukweli kama tukiamua kuzifuata.

a. Kama kiongozi yeyote anahusika na uhusiano wa kimapenzi na mtu yeyote ambaye si kinyume cha sheria kuwa nayo, basi jambo hilo ni la binafsi.

b. Kama kiongozi huyo katika mahusiano hayo anaenda nje ya ndoa yake basi suala hilo ni la yeye na mwenzi wake, wachungaji/mashehe, na wanafamilia. Sisi watu wa nje, mwiko kuligusia.

c. Kama kiongozi anahusika na suala la mapenzi ambalo ni kinyume na sheria kama kubaka, mapenzi na watoto wa shule, au kujihusisha na makosa ya Sheria ya Kujamiiana (vipengele maalum) ya 1998 na sheria ya nyingine zihusianazo na makosa ya kujamiiana basi mtu huyo siyo tu anajadilika bali hastahili kushikilia uongozi.

d. Kama kiongozi wa umma (mwanasiasa au vinginevyo) anahusika na mahusiano ya mapenzi ambayo yanahusisha ofisi yake, cheo chake, jina, na hadhi yake, basi mtu huyo siyo tu anajadilika bali anastahili kujiuzulu kulinda heshima ya ofisi hiyo.

Kanuni hizo nne, kwangu zinaniongoza ninapoangalia hoja zilizotolewa hapo juu.

Nitumie mfano halisi ambao bado uko mawazoni mwa watu. Gavana wa New York Bw. Spitzer amejiuzulu wadhifa huo kwa kosa la kujihusisha na huduma ya malaya na kulipia karibu shilingi milioni 90! Licha ya kuwa alikuwa ni makini katika kuwafunga wengine (akiwa Mwanasheria Mkuu wa NY) kwa makosa kama hayo, lakini kibano kilipogeuzwa alijikuta hana ujanja.

Hata hivyo, Gavana mpya naye alipoingia jambo la kwanza kukiri ni kuwa yeye na mke wake walikwenda nje za ndoa yao baada ya kuwa katika mchakato wa talaka miaka kadhaa huko nyuma, na aliamua kuwa mkweli kuwa wakati huo hawakutarajia kurudiana, lakini waliporudiana walisameheeana na wako pamoja leo hii.

Sasa turudi kwenye suala la Spika Sitta.

Kama madai dhidi yake kuwa amehusisha ofisi yake na fedha za Watanzania katika kuhudumia his sexual trysts siyo tu amedhalilisha ofisi ya spika bali anastahili kuwa impeached.

Kama madai ya kutumia ofisi, fedha, na mali za serikali ni ya kweli (na huyu aliyeleta hii taarifa ameniweka kwenye hali ya "nusura nimuamini") basi Spika Sitta kama vile Mbowe anastahili kuambiwa arudishe fedha hizo, aombe msamaha, na kusafisha nyumba yake.

Kwanini basi mada hii inazungumzika hapa JF?

Kwa sababu, linapokuja suala la ngono na mambo ya mapenzi:

- Tumemzungumza Kikwete hapa
- Tumemzungumza Mengi hapa
- Tumemzungumza Manji hapa
- Tumemzungumza Amina hapa
- Tumemzungumza Zitto hapa
- Tumemzungumza Slaa hapa
na wengine wengi...

Sasa kwanini Sitta asiwe sehemu ya mazungumzo hayo? Kama madai haya ni ya uongo, ni ya kupuuza tu kwani hata mtu akitaka kutafuta ushahidi hawezi kuupata kama vile yule jamaa aliyekuja na madai kuwa Mbowe kabaka watoto wa shule na anakesi kibao mahakamani tangia miaka ya tisini, lakini alipoulizwa ataje mahakama na kesi hizo akakimbia! huyu aliyeleta suala la Sitta tukimuuliza hata majina sitashangaa.

NB:

Pamoja na maneno yangu mengi hapo juu nitoe angalizi moja. Niliripoti karibu mwezi mmoja uliopita kuhusu Agenda 21. Ninaamini (na ninazo sababu za kuamini) kuwa aliyeleta mada hii awali ni mtu wa agenda hiyo, na lengo ni kuhakikisha wanajibu mashambulizi hasa baada ya Spika Sitta kumzidi ujanja Lowassa (imeelezewa jinsi gani kwenye klhnews taarifa ya "Jinsi Lowassa alivyozidiwa kete".

Hivyo, sehemu hii ni sehemu ya mapambano yale yale na kwa vile JF imekuwa kama msumeno, tunaposhabikia wengine kuwakuta tusije shtuka siku moja na sisi tuko upande wake wa makali!

M. M.
 
.

b. Kama kiongozi huyo katika mahusiano hayo anaenda nje ya ndoa yake basi suala hilo ni la yeye na mwenzi wake, wachungaji/mashehe, na wanafamilia. Sisi watu wa nje, mwiko kuligusia.

japo sijui ni vigezo gani umetumia
kuweka standard hizi!

pia kutuhimiza kuwa ni mwiko kuligusia sijui unaupata wapi ujasiri wa namna hii.

let me put it like this:
Matendo kama haya ya kutembea na wake/waume za watu ni tishio kwa ustawi wa jamii,ni matendo yanayojenga chuki na kubomoa misingi ya ngazi ya awali ya Taifa ya familia kwa hiyo ni haki sisi kama jamii kuyakemea na kumkemea yeyote yule ambaye yupo within our reach.

Ni matendo yanayotishia jamii kutokana na kuwa kichocheo cha ukimwi!,hapa huwezi kuiambia jamii ikae hivi hivi,wakati unaona wale makamanda wanaoongoza mapambano wanaanza kuact kinyume!

Ndiyo sote tuna udhaifu, lakini udhaifu wetu usiwe sababu hata ya kutokemea yale yanayokwenda kinyume cha maadili ambayo kimsingi inabidi tuyafuate
 
.



japo sijui ni vigezo gani umetumia
kuweka standard hizi!

pia kutuhimiza kuwa ni mwiko kuligusia sijui unaupata wapi ujasiri wa namna hii.

Ni mwiko kwa sababu, hakuna mtu mwenye haki ya kumuambia mtu aliyeoa au kuolewa kuwa "tunakutaka ulale na mkeo/mumeo tu"! Ni wao waliokuwa kiapo cha ndoa na ni wao wataishi na matokeo ya kukivunja kiapo hicho. Sasa jukumu la jamii ni kuwasaidia kuishi katika ndoa hiyo vizuri, ndipo suala la wachungaji, n.k linapokuja.

Na linapokuja suala la watoto na mambo ya Ukimwi, hali halisi inaonesha kuwa si wote wenye ukimwi ni watu wa ndoa!
 
hakuna mtu mwenye haki ya kumwambia mtu alale au asilale na Mke/mme wake mwenyewe , lakini mtu mwenye kuibiwa mke/mme ana haki ya kumwambia mwenye kuiba aache kusarandia vya wenzie,hapo ndipo jukumu la jamii linapokuja, kukemea tendo zima linalosababisha huzuni kubwa na ukosefu wa harmony katika jamii na pengine kuweza kupeleka hat uvunjivu wa familia yenyewe.
Na linapokuja suala la watoto na mambo ya Ukimwi, hali halisi inaonesha kuwa si wote wenye ukimwi ni watu wa ndoa!
ni kweli siyo wote wenye ukimwi ni watu wa ndoa, lakini je hiyo pekee yafaa kutufanya tukae kimya hata kama ni dhahiri tendo linalotendwa linachochea ustawi wa tatizo?.tena tendo lenyewe liwe linafanywa na mtu ambaye kwa cheo chake ingebidi afahamu urefu wa kina cha tatizo na hivyo kuwa mfano wa namna ya kupambana na tatizo?.

Hii ni issue kubwa siyo ndogo hata kidogo.
bila values katika family hakuwezi kuwa na values katika taifa.
 
hakuna mtu mwenye haki ya kumwambia mtu alale au asilale na Mke/mme wake mwenyewe , lakini mtu mwenye kuibiwa mke/mme ana haki ya kumwambia mwenye kuiba aache kusarandia

Yaani mtu anamuiba mtu mwingine na unakuita huko kusarandia? Mtu akimtongoza mume/mke wa mtu na mtu huyo akaingia laini, huwezi kuita kuiba! Mtu ambaye anajua amefunga ndoa, na ana familia anapokubali vishawishi vya nje, na akaacha ndoa yake, mtu huyo ana sababu zake. Hakuibwa. Ila kama kuna mtu kweli anaingia kwenye nyumba ya mtu na kumuiba mke/mume wa mtu huyo mtu anastahili kutiwa pingu kwani anachofanya ni kile nilichokielezea kwenye mojawapo ya vifungu vya kanuni zangu.

vya wenzie,hapo ndipo jukumu la jamii linapokuja, kukemea tendo zima linalosababisha huzuni kubwa na ukosefu wa harmony katika jamii na pengine kuweza kupeleka hat uvunjivu wa familia yenyewe.

Hilo nakubaliana na wewe kabisa, lakini wenye jukumu la kwanza la kutunza na kulinda ndoa zao siyo jamii ni wana ndoa wenyewe! sisi wengine hata tupige matarumbeta mtu akiamua "kupata" nje ataruka ukuta (no pun intended)



Matatizo ya ndoa hayaishi kwa kukemewa (historia inaoonesha hivyo) yanatokana na maadili mazuri ambayo msingi wake ni kumcha Mungu, maadili ambayo hupandikizwa tangu utoto na humwagiliwa kama miche katika maisha ya watu. Hata hivyo mwanadamu ni kiumbe huru na licha ya hayo yote akiamua kwenda nje ya ndoa au kufanya kitu kinyume na maadili ya ndoa ni yeye anawajibika kwa hilo.


Hii ni issue kubwa siyo ndogo hata kidogo.
bila values katika family hakuwezi kuwa na values katika taifa.

Sipingi hilo, na tuko mstari mmoja. Ninachosema, huwezi kuwalazimisha watu wazima na akili zao kuwa na maadili katika familia kama wameamua kutokuwa nayo utawafunga!?
 
Mzee Mwanakijiji,

Sawa hatuwezi kukufuatilia na maamuzi yako kama umemchoka mkeo na unataka visura wengine and what not--technically we can, na tutachonga tu kama kawaida yetu...

Lakini wananchi tuna-exclusive right to question matendo ya kiongozi! Ukiwa kama kiongozi, tuna right ya ku-question your ethical standards, na hilo la ndoa kwa mzee Sitta fits this scenario like a glove. Tutakuwaje na imani nawe kama unaweza kuiweka ndoa yako rehani? kama hawawezi kuacha uroda, waache kuwania uongozi!
 
Mzee Mwanakijiji,

Sawa hatuwezi kukufuatilia na maamuzi yako kama umemchoka mkeo na unataka visura wengine and what not--technically we can, na tutachonga tu kama kawaida yetu...

mnakaribishwa, niko kwenye basikweli yangu nani atanitaka! miye mrs anaitwa bi. "L.A. Ptop"..

 
Mwanakijiji, nilipoandika
Sawa hatuwezi kukufuatilia na maamuzi yako kama umemchoka mkeo na unataka visura wengine and what not--technically we can, na tutachonga tu kama kawaida yetu...

...was not necessarily directed to you; but all people who have something on the side. Ndio maana nasema kama mtu anataka uroda aendelee tu, ila akiukwaa uongozi, tuta-question matendo yako. Lugha inaleta tabu at times.
 
Binafsi hoja alilolitoa huyu Mzee Busara inatupa mwangaza wa dealings za watu tunaowaita viongozi wetu. Kama kiongozi wenu ni mwizi, wafuasi mtaachaje kuwa wezi?

Sula la yeye kutoa risiti za uwongo mbona hilo ndilo linalofanyika katika kila ofisi la umma, ila tunahitaji kiongozi mmoja tumfanye scapegoat tumwaadhibishe mbele ya umma ili tabia hii ikome mara moja. Kama ni Sitta, so be it! Hili ni suala la kushikiliwa bango. Linauma sana pale ninapokatwa mshahara wangu 35% for PAYE alafu mpumbavu mmoja hashikilii community committments na anatumia hizo fedha kumfurahisha kimada wake, this is not fair. Wakati mimi nalazimika kwenda kukopa kwenye banking institutions ili kufidia the gap na kuweza kumudu maisha. This is not fair at all.

Zitto, kijana wangu, umekosea step kuja kumtetea spika na Mbowe. Were you there with them all along kujua kuwa ni watu wasafi?? Come on even I have skeletons in my closet ila skeletons zangu bahati nzuri hazimfikii huyo sitta wala mbowe maana ni personal skeletons!! Hii tabia ya viongozi kutaka wanaowatuhumu kutoa ushahidi badala ya wao kuachia ngazi ili upelelezi ufanyike inabidi hii tabia ikome.

Nimeshuhudia kimada wa kiongozi mkubwa serikalini akijengewa nyumba sinza karibu kabisa na Lion Hotel in one and half months ikakamilika na miukuta mirefu na geti kubwa. Nikashuhudia kimada huyohuyo akinunuliwa samani nyingi za bei kubwa sana kutoka nje na kwa wakati huo alikuwa na mimba, basi ToysRus ilihamia bongo. Lifestyle yake ilikuwa ya hali ya juu mno. Alijaribu kuwa msiri ila haikusaidia kitu because people asked questions na akajikuta she has to go to neighbors funerals and the sort hatimaye ukweli ukajulikana. Tatizo pia ni kwamba ni fedha za umma zilizotumika kujenga ile nyumba usiku na mchana for a month, generators ziliwaka pale hakuna mfano. Kwa nini nasema fedha za umma, yule binti hana elimu whatsoever na hana kazi ila magari ya serikali hayaishi kupeleka maji, kumpelekea chakula, akiumwa basilinakuja gari kumpeleka hospitalini. Akitaka kwenda safari ya mkoani basi linakuja gari kumpeleka kusalimia wazee wake huko na yote ni STJ vehichles.
Nasikia huyo kiongozi baada ya kumaliza muda wake na hakupewa shavu in the following cabinet. Hali ilianza kuwa mbaya pale na nyumba ni ghetto sasa.
Kumbuka there are children of poor people who would have used that money to go to school, pay for medical supplies at a neighbouring local dispensary. But no that money went to toysRus!

Kwa hiyo bwana acha watu tusikie uchungu maana amepewa dhamana na wananchi kuwatumikia basi na watumikie. Kama Mzee busara wa lying and has given us hazy details about Sitta, there are many more we can name for sure in this forum.

I remain.
 
Nadhani huu ni wakati murua wa JF kuwa na kamati itakayokuwa na wataalamu angalau 5 ambao wote humu ndani tutawachagua kutokana na hekima walizozionyesha ili watusaidie katika hiki kipindi kigumu nchini kwetu.

Ili kundi kubwa la mafisadi limegundua kuwa limegundulika na liko mbioni kumalizwa na hata kufungwa. In my humble opinion I believe they are trying to throw darts and smoke screen to everybody else with a clear intention of confusing wananchi who is a FISADI.

I do not condone the so called behavior allegations above against Hon. Speaker but come on when we are trying to deal with massive losses in billion dollar ranges, who really cares about the small time imprest problems??? Mr. Mbowe ameletewa maneno mengi kisa deni la 15 million Tshs!! Are we serious??

So jamani tuangalie uwezekano wa kuwa na tume ya kuchuja mambo tukianza kupata mashambulizi haya ya watu wenye post 1!!

I repeat sisemi tucensor vitu no way<< Nasema tuangalie tu uwezekano wa kugrade au kuflag issue kama hii maybe iletwe huku kwenye vibweka, mpaka mwelekeo uwe mzuri ndio tudwell in.


EL, Rostam and their croonies have more things in the pipeline against them like EPA, BOT, Vodacom, utalii, majengo ya NHC nk so I think tuwe tu careful smoke screen zikija kwa nguvu ili heshima ya JF ibaki palepale na tuweze kudeal zaidi na maswala ambayo yatasaidia nchi na watu wake wote.

My 2 cents
 
Hapa si kwamba kwa kuwa umetongoza na mkakubaliana basi hiyo eti iwe imekwisha!,bali hapa suala ni kwamba umemtongoza nani na umemkubali nani, kama ni kutongoza kuna watu wanawatongoza dada zao au hata kaka zao na wanakubaliana, je kwa mtizamo wako unataka kutuambia kwamba kama inatokea hivyo jamii ikae kimya eti kwa sababu ni makubaliano a watu wawili?.
kuna values jamii haiwezi kuzicompromise na kuacha hali iendelee bila kukemea,

ugoni haujawahi kuwa sahihi hata siku moja kwa kisingizio cha kukubaliana katika kutongozana.


Hilo nakubaliana na wewe kabisa, lakini wenye jukumu la kwanza la kutunza na kulinda ndoa zao siyo jamii ni wana ndoa wenyewe! sisi wengine hata tupige matarumbeta mtu akiamua "kupata" nje ataruka ukuta (no pun intended)
Ni kweli jukumu la kwanza la kutunza ndoa ni la wanandoa wenyewe lakini ni jukumu la jamii kusisitiza kwa nguvu zote umuhimu wa kuheshimu taasisi hii ya ndoa, na inapotokea kwamba mtu asiyeiheshimu taasisi hii ya ndoa ni kiongozi hii inakuwa serious zaidi kutokana na nafasi yake katika jamii ambayo yeye alitakiwa aonyeshe mfano bora.



Ukweli wa Lengo la juhudi zote za kupambana na matitizo ya maadili katika jamii huwa siyo kumaliza tatizo, lengo huwa ni kupunguza tatizo, mfano kuweka sheria kali dhidi ya rushwa lengo ni kuipunguza si kuimaliza , lengo la kuweka sheria kali dhidi ya ubakaji utapunguza wabakaji lakini hutawamaliza,na hivyo hivyo hii tabia kwenda nje ya ndoa haitisha kwa kukemea lakini itapungua



Sipingi hilo, na tuko mstari mmoja. Ninachosema, huwezi kuwalazimisha watu wazima na akili zao kuwa na maadili katika familia kama wameamua kutokuwa nayo utawafunga!?

Nakubaliana na wewe kuwa huwezi kuwalazimisha watu wazima kuwa na maadili katika familia lakini naamini kwamba kwa kuweka scrunity katika matendo wanayoyafanya itasaidia kupunguza tatizo. chukulia mfano kwa kiongozi, iwapo kiongozi atafahamu kwamba kwa matendo yake anahatarisha nafasi yake basi huenda akaacha kujihusisha na matendo ya namna hiyo, na kwa kufikia hapo tutakuwa tumepunguza tatizo la infidelity katika jamii.
 
- Tumemzungumza Kikwete hapa
- Tumemzungumza Mengi hapa
- Tumemzungumza Manji hapa
- Tumemzungumza Amina hapa
- Tumemzungumza Zitto hapa
- Tumemzungumza Slaa hapa
na wengine wengi...

Issue sio ngoma au uaminifu katika ndoa tu. Hili jambo lilishaongelewa hapa JF tena na tena, Sitta na hao wengine wangekua walalahoi, who will give a damn! Ukishakua Public figure things change...mfano Bill Clinton and few US senators that had to resign because of sex scandals
 
Gamba, kama unaangalia viongozi wa siasa kuwa ni mfano wa jamii, you picked the wrong group! usimwangilie mtu mwingine yoyote kuwa mfano wa jinsi ya kuishi kwani watu wana disappoint sana.. believe me.. jiangalie wewe mwenyewe na uwe mfano kwa watoto wako.
 
Mungu ibariki Tanzania, Wabariki viongozi wake...

Kama watanzania wote tutamuomba Mungu (kutoka ndani ya mioyo yetu) wakati tuki-imba wimbo wetu wataifa basi janga la kupata viongozi na vitendo vyao kama kina Lowasa halitotukuta!

Kwasasa hivi viongozi tulionawo hauwezi ukapata hata mmoja ambaye atakua hana kasoro na msafi wa mambo haya ambayo aliyo andikiwa Mhs. Sitta.

Hii imeasiri jamii nzima; kwatulikuwepo Tanzania, ukiwa ndio umemaliza chuo na Umeajiriwa serikalini - mshahara pekeyake ni hautoshi kuendesha maisha yako, hivyo utaanza kutengeneza tabia ya kudokoa huku na kule.

Kama una Mke - nyumbani mapema hakurudiki - kwakuwa lazima utakumbana na msururo wa matatizo yanayohitaji fedha kutatuliwa.

Dawa ni kutafuta kimada nje - ambacho unajua wazi siku za mwanzo invoice haiwi kubwa - siku invoice itakapo ongezeka hapo huonekani (Hungera kwa Mhs Sitta anaweza kumudu zaidi ya Watatu - mambo ya kiislamu hayo - Ruhsa hadi wa-nne!).

Nini hasa ninachotaka kusema, kunahaja ya kuibadilisha jamii nzima - ili tuondokane na production ya viongozi kama hawa ambao tunaowapata hivi sasa. Na hili ni sijambo lasiku mbili!

Hivyo kama jamii itaweka mkakati - kwa mfano - kwanza tushughulikie mambo kama Richmond, EPA na kadhalika; tutakapo fanikisha haya ndiyo tuingie katika hatua nyengine ya udokozi, pamoja na tabiya ya viongozi wetu. Hapa tutaweza kuokoa mamilioni na kupelekwa kwenye jamii.

Kwahiyo nakubaliana na Mhs. Zito kuwa hili suala la Mhs. Sitta ni dogo sana kwa muda huu kulijadili.
 
Pamoja na mada hii kuwa tamu, hebu tujikumbushe hii habari ya Mwanakijiji hapa na kama JF nayo ni sehemu ya mkakati husika.

http://www.klhnews.com/index.php/headlines/agenda-21-yaundwa.php


Wakati habari hii inaandikwa tayari Kikwete, Dk. Slaa, Mengi na Zitto walikwisha kuguswa na kuchafuliwa, sasa kaja Mbowe na baadaye Sitta. Nakumbuka mtu mmoja alimwambia Mbowe, "nitakujibu kwa staili yangu" baada ya mtu huyo kuguswa na mapigo ya wabunge wa Chadema hasa siku ile ilipotolewa kwa mara ya kwanza orodha ya MAFISADI. Kwa wanaokumbuka orodha ile hata hapa JF ilitolewa ikiwa na majina manane (8) likiwamo jina la Kikwete lakini bila ya majina ya Lowassa, Karamagi na Rostam,katika kipindi ambacho BoT (EPA) na Richmond na TICS zilikua zimepamba moto. Majina hayo ambayo yaliongezwa baadaye, yaliwakera wahusika. Sina hakika kama hili lilikua BAHATI MBAYA katika maandalizi ya orodha kwani wananchi waliwajua hawa kuwa ndio vinara wa UFISADI. Ndipo mtu mmoja akawaambia watu, "atajibu kiaana" na kwamba hana haraka na hilo, kwani ni SUALA LA MUDA TU.

Kabla sijahoji USAHIHI wa TAARIFA na kwamba pamoja na kuwa HOJA ya SITTA ni sehemu ya mapambano yetu ya kuhakikisha nchi inakua SAFI, kuna maswali ya kujiuliza, maswali ambayo nilijiuliza alipoanza kushambuliwa Slaa, Zitto na hata Mengi.

-Nilitoa mfano wa polisi (SITTA,SLAA, ZITTO, KILANGO, MWAKYEMBE, MENGI,MBOWE) ambaye 'tunamtuhumu' kwamba hana maadili ambaye AMESHIKA SILAHA na mbele yetu tuna MAJAMBAZI (LOWASSA, ROSTAM, KARAMAGI, CHENGE) yenye silaha yanaua WATANZANIA WENZETU, sasa tutaanza kumshughulikia huyo POLISI kwanza!!? ama tutampa nafasi ayadhibiti majambazi?!!! Hapa lazima tuzingatia kipindi tulichonacho, kwamba sasa ndicho ambacho wanaibuka watu wanaojifanya wana uchungu na nchi, watu ambao awali hawakua wenzetu kabisa, sasa wametoka nje eti ndio wanaona maovu, kuzuia wasishughulikiwe ama kuwatisha POLISI wetu wasipambane nao. KWanza tujue kwamba polisi (WAZALENDO) tulionao ni wachache mno na hawana SILAHA (uwezo) na vyombo vya usafiri (MEDIA) vilivyopo ni vichache (JF, MWANAHALISI, RAIAMWEMA, THISDAY, KLHN) na tunapoanza kugeukana na kugeuza mashambulizi upande wetu, tunampa adui nafasi ya kushinda VITA tuliyoisimamia kwa urahisi mkubwa na baadaye, majambazi hayo yatarudi na kutushughulikia wenyewe (kama walivyowakamata MAC na Mike), watafungia magazeti na mitandao yote na ikibidi wataua watu na NAWAHAKIKISHIA hawatafanya makosa tena ya KUJIAMINI MNO na kutudharau tena (kusema kelele za chura) kama walivyofanya kwa RICHMOND na EPA, sasa wameshajua JF, Mwanahalisi, Thisday, RaiaMwema ni kiboko kwa hiyo wameingia kwa KASI, NGUVU, ARI na PESA 'mpya' na ndugu zangu HISTORIA ITATUHUKUMU, MUNGU ATATULAANI kwa kusema, "Muliniomba nafasi nikawapa, nikawachanganya, mukaichezea kwa kugombana wenyewe kwa wenyewe tena hadharani". Tumeingiliwa ndani ya nyumba, sasa tunagombana wenyewe na wezi WANAPETA. Tumebadili mwelekeo, sasa FISADI ni MBOWE NA SITTA na LOWASSA, KARAMAGI, ROSTAM ni MASHUJAA.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU WALAANI MAFISADI NA MAKUWADI WAO

uliza, hivi kwanza tunataka kufanikisha nini kwa hoja hii? Kwamba Sitta ang'oke? Ili tufanikishe kitu gani katika malengo yetu makuu?
 
ORODHA YA KWANZA YA LIST OF SHAME

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…