Mcheza Viduku
JF-Expert Member
- Jun 24, 2020
- 1,049
- 2,535
.............hapo kwenye hizo nukta nukta ni sehemu ya salamu na kila mtu atajibu vile atahisi nimemsalimia.
Wapwa kwenye hizi sherehe zetu huwa kuna mambo mengi sana yanatokea, mimi nikiwa mdau mkubwa wa hizi sherehe (MC) ninazo shuhuda nyingi sana za yanayotokea kumbini.
Hapo chini nitaziweka chache, na wewe mwanasherehe mwenzangu unaweza kutushirikisha siku ulipohudhuria sherehe yoyote nini kiliwahi;
Kukufurahisha sana
Kukuchekesha sana
Kukukera sana
Kukuudhi sana
Kukusononesha sana
Kukufedhehesha sana
Kukukasirisha sana
Kukushangaza sana
Kutoka kwa MC, mgeni mualikwa mwenzio, mwanakamati au familia ya wahusika wa sherehe, na ilikuwaje hebu tushirikishane hapa.
USHUHUDA WA KWANZA; kuna baadhi ya sherehe unapofika muda wa chakula taratibu huwa ziko wazi kabisa, wanatangulia maharusi, wanafuatia best man na best lady, halafu wale ma maids wao, baada ya hapo watainuliwa wazazi wa pande zote mbili nk, lakini cha kusikitisha ni kwamba wakitangulia maharusi tu tayari wageni waalikwa wanasimama na kuweka foleni ndeeeeeefu kama vile wanaenda kuchukua mahindi ya msaada kwenye ofisi za kata, HILI JAMBO HUWA LINASIKITISHA SANA.
USHUHUDA WA PILI; Wakati wa kutoa zawadi kuna baadhi ya Mc's wenzangu huwa wanafanya kama kuwadhalilisha wageni kwa kutoa maneno yasiyokuwa na staha kabisa kama vile "wewe kwa suti hiyo uliyovaa huwezi kukosa sh elfu 10 bwana, usiwaangushe wenye suti wenzio, HILI HUWA LINADHALILISHA SANA.
USHUHUDA WA TATU; Wakati huohuo wa zawadi, muda umeshakuwa sio rafiki sana na MC anajitahidi kukimbizana na muda, lakini wanakuja mashangazi na pea ya khanga, pea ya kitenge vikombe vya plastiki na shuka, wataomba mic wanataka waongeeeeee, MC akijaribu kuwasihi kuwa muda sio rafiki utawasikia wanasemea pale pale kwenye mic "MC tumekulipa utufanyie kazi yetu huna mamlaka ya kutupangia fuata matakwa yetu usitupeleke peleke bwana, unakuwa na haraka kama CHA KWANZA" HILI HUWA LINAMDHALILISHA MC, NA WAZAZI.
USHUHUDA WA NNE; Nikiwa mgeni mualikwa siku hiyo Mc aliyekuwa anaongoza ile sherehe alimuita babu aje afungue champagne wakati anajua mzee hawezi, akachombeza eti "babu kama inakushinda tumia meno" mzee akaanza kutumia meno ile champagne ikafunguka na kummwagikia usoni, wapuuzi kama yeye walicheka na kufurahi lakini pale Mc alifanya tendo la kumdhalilisha sana yule mzee, hakuishia hapo......kesho akaitundika mtandaoni kwenye page yake.
Haya ni machache sana kati ya mengi tunayokutana nayo huko ukumbini, kwako wewe ni yapi uliyowahi kuyaona/kuyasikia?
KWAKO MWALIMU KASHASHA.....
Wapwa kwenye hizi sherehe zetu huwa kuna mambo mengi sana yanatokea, mimi nikiwa mdau mkubwa wa hizi sherehe (MC) ninazo shuhuda nyingi sana za yanayotokea kumbini.
Hapo chini nitaziweka chache, na wewe mwanasherehe mwenzangu unaweza kutushirikisha siku ulipohudhuria sherehe yoyote nini kiliwahi;
Kukufurahisha sana
Kukuchekesha sana
Kukukera sana
Kukuudhi sana
Kukusononesha sana
Kukufedhehesha sana
Kukukasirisha sana
Kukushangaza sana
Kutoka kwa MC, mgeni mualikwa mwenzio, mwanakamati au familia ya wahusika wa sherehe, na ilikuwaje hebu tushirikishane hapa.
USHUHUDA WA KWANZA; kuna baadhi ya sherehe unapofika muda wa chakula taratibu huwa ziko wazi kabisa, wanatangulia maharusi, wanafuatia best man na best lady, halafu wale ma maids wao, baada ya hapo watainuliwa wazazi wa pande zote mbili nk, lakini cha kusikitisha ni kwamba wakitangulia maharusi tu tayari wageni waalikwa wanasimama na kuweka foleni ndeeeeeefu kama vile wanaenda kuchukua mahindi ya msaada kwenye ofisi za kata, HILI JAMBO HUWA LINASIKITISHA SANA.
USHUHUDA WA PILI; Wakati wa kutoa zawadi kuna baadhi ya Mc's wenzangu huwa wanafanya kama kuwadhalilisha wageni kwa kutoa maneno yasiyokuwa na staha kabisa kama vile "wewe kwa suti hiyo uliyovaa huwezi kukosa sh elfu 10 bwana, usiwaangushe wenye suti wenzio, HILI HUWA LINADHALILISHA SANA.
USHUHUDA WA TATU; Wakati huohuo wa zawadi, muda umeshakuwa sio rafiki sana na MC anajitahidi kukimbizana na muda, lakini wanakuja mashangazi na pea ya khanga, pea ya kitenge vikombe vya plastiki na shuka, wataomba mic wanataka waongeeeeee, MC akijaribu kuwasihi kuwa muda sio rafiki utawasikia wanasemea pale pale kwenye mic "MC tumekulipa utufanyie kazi yetu huna mamlaka ya kutupangia fuata matakwa yetu usitupeleke peleke bwana, unakuwa na haraka kama CHA KWANZA" HILI HUWA LINAMDHALILISHA MC, NA WAZAZI.
USHUHUDA WA NNE; Nikiwa mgeni mualikwa siku hiyo Mc aliyekuwa anaongoza ile sherehe alimuita babu aje afungue champagne wakati anajua mzee hawezi, akachombeza eti "babu kama inakushinda tumia meno" mzee akaanza kutumia meno ile champagne ikafunguka na kummwagikia usoni, wapuuzi kama yeye walicheka na kufurahi lakini pale Mc alifanya tendo la kumdhalilisha sana yule mzee, hakuishia hapo......kesho akaitundika mtandaoni kwenye page yake.
Haya ni machache sana kati ya mengi tunayokutana nayo huko ukumbini, kwako wewe ni yapi uliyowahi kuyaona/kuyasikia?
KWAKO MWALIMU KASHASHA.....