Ni sawa kununua gari ya TZS 15 Million huku ukiwa unaishi nyumba ya kupanga chumba na sebule?

Sioni Tatizo, Gari sio Anasa kwa Kasi ya Maendeleo, usafiri unahitaji sana, na Maisha yamebadirika Gari ni kitu cha kawaida Kabisa kwa kasi ya Kukimbizana na Uchumi...
 
Ulaya mtu anaishi kwenye nyumba ya kupanga tena iliyopo chini ya uangalizi ya serikali lakini bado ana miliki AUDI , FERRARI , n.k

ni mtazamo tu vijana wa Tz.
 
Ni kosa la kiufundi lakini linatokea.unakuta mtu una kazi yako na plan yako ni kujenga kidogokidogo baada ya muda flan.Hivyo usimdharau mtu.Kila mtu na maisha yake
 
Tuache unafiki, sasa hivi hela ni ngumu sana, mtu huwezi kupanga kununua gari la shilingi mil. 15 wakati hata kiwanja huna, kama utafanya hivyo basi wewe ni mjinga, suala kusema sijui mishemishe za mjini zinahitaji gari hakuna lolote, mafanikio ya mtu ni uwezo katika kujipatia mlo wa kila siku, mavazi na nyumba ya kujenga mwenyewe.
Kweli mkuu, sometimes humu watu wanajitoa ufahamu kabisa ktk hili.
 
Mkuu hizi gari siku hizi zinapiga hela atari...
Mm mwenyewe nilikua na mindset kama hiyo nikanunua uwanja huko madale kabla hata sijanunua gari eti nijenge kwanza...
Sasa hiv nimekiuza kiwanja nimenunua IST nime muajiri dereva kwa wiki ananiletea laki mbili nakula laki nane kwa mwezi, huu uchawi unao itwa UBER bora usikie kwa jirani ako. Kwa sasa nimeagiza honda fit ili niongeze nguvu niwe nakula 1.6m kwa mwezi sina shida na nyumba, nipo zangu Gomz chumba 45,000 kwa mwezi.
Dah safi sana kiongozi, hayo ndio nayaita maujanja mzee. Kwa hio akili gari yako haiwezi kuwa ya anasa maana inakuingizia pesa ndefu. Gari ya anasa ni ile inayokutia umaskini tu pasi na kukuzalishia pesa.
 
Fanya yako, tumia akili jenga nyumba yako wenye magari waje wapange sio unataka kuziba riziki za wenye nyumba,kwa hiyo wote wajenge halafu wenye biashara ya nyumba wawe vibaka au.
 
Huwezi pangia matumizi ya hela zisizo zako, hata mtu akiamuwa kununua boti, tena atafaidika wakati wa masika, anapeta tu, anaweza lala humo humo, tena liboti likiwa zuri inamaanisha litakuwa na kitanda, vikochi, choo na jiko la kishkaji, yote sawa tu, hela za mtu siyo 1.5trilioni zilizoyeyuka na tunaziulizia.....
Wa kununua ndinga nunua tu, maisha ndio haya, usipoishi maisha utakayo, utayaishi wapi?!
 
Kila mtu life stly yake kachangua nisikia kununu gari ata kama nimepanga fresh tu unajua raha ya usafiri wako mwenyewe mtam
 
Tuache unafiki, sasa hivi hela ni ngumu sana, mtu huwezi kupanga kununua gari la shilingi mil. 15 wakati hata kiwanja huna, kama utafanya hivyo basi wewe ni mjinga, suala kusema sijui mishemishe za mjini zinahitaji gari hakuna lolote, mafanikio ya mtu ni uwezo katika kujipatia mlo wa kila siku, mavazi na nyumba ya kujenga mwenyewe.
kila mtu na vipaumbele vyake!
wacha tununue magari mkuu
 
WanaJF poleni na mihangaiko ya kutwa!

Wale wa mijini hasa Dsm sasaiv wapo kwenye foleni barabarani. Yote maisha.

Nimejiuliza hili swala. Maeneo mengi mjini, watu wengi wanamiliki magari licha ya kwamba wanakaa nyumba za kupanga, mfano unamkuta mtu ana mke na watoto 2 huku akiwa kapanga chumba na sebuleni huko uswazi, lakini wakati huohuo ana miliki gari ya kutembelea ya maana mathalani gari ya kuanzia TZS 10 MIL and above. Mtu huyo unakuta hata kiwanja hana. Hii tabia ipo sana hasa Dsm.

Hii kitu ni sahihi wakubwa au kujikweza na ulimbukeni tu wa maisha ya kuigana?
Wewe usilinganishe gari na nyumba kabisa acha kuunganisha gari na nyumba gari ni kitu kingne mkuuu, unalinganisha gari na nyumba kweli utakuwa wewe ni under 18 hivi unajua faida za gari? Hivi unajua umuhimu wa gari? Hivi unajua heshima Ya gari?

Ukiwa na gari utarahisisha kazi zako Kwa uwepesi zaidi utaenda kazini ukiwa msafi utafika ukiwa msafi utarudi nyumbani ukiwa msafi

Utaenda kanisani na familia Kwa usalama Kwa furaha Kwa heshima mtafika mtarudi mkiwa wasafi
Utaenda kwenye shughuli za kifamilia utafika ukiwa msafi utarudi ukiwa msafi na utafika Kwa Wakati

Utatoka out na familia au mwenyewe utafika Kwa Wakati ukiwa msafi na utarud Kwa Wakati unaoutaka wewe

Sehemu zote hizo utakazoenda utaheshimika na utu wako utaheshimika na wote watakupa heshima yako

Mtu mwenye gari anaheshimika Kwa majirani Kwa marafi Kwa ndugu had kijijini kwenu unaheshimika

Mtu mwenye gari hupata madili mbali mbali madili makubwa na madogo

Mtu mwenye gari hupata mademu kiurahisi na marafiki wa kiume kiurahisi

Mtu mwenye gari hupata marafiki wenye hela mwisho huonyeshwa mbinu za kupata zaidi

Ukiwa na gari Ya 20.000.000 ukifika mahali umekwama utaenda bank utachukua milioni kumi faster utajipanga upya mtu mwenye gari ukikwama utakopa Kwa mtu faster utawekea kadi tofauti na nyumba mtu mwenye gari ukishindwa kabisa utauza gari utajipanga upya gari inauzika kiurahis kuliko nyumba

Ukiona vipi utawekea gari utapata hela utajipanga

Lakini kubwa na zaidi mtu anaemiliki gari usimchezee juu Ya Nyumba huyo ni rahis mno kuja kujenga nyumba kumbuka gari ili uimiliki lazima uwe na hela za pamoja Lakini nyumba mtu unaweza ukaanza kujenga ukiwa na milioni moja

Naomba nikuambie pia kuwa asilimia tisini na tisa wenye majumba Ya kifahari walianza kumilili gari


Hivyo usilinganishe kuanza kumiliki gari au nyumba
 
WanaJF poleni na mihangaiko ya kutwa!

Wale wa mijini hasa Dsm sasaiv wapo kwenye foleni barabarani. Yote maisha.

Nimejiuliza hili swala. Maeneo mengi mjini, watu wengi wanamiliki magari licha ya kwamba wanakaa nyumba za kupanga, mfano unamkuta mtu ana mke na watoto 2 huku akiwa kapanga chumba na sebuleni huko uswazi, lakini wakati huohuo ana miliki gari ya kutembelea ya maana mathalani gari ya kuanzia TZS 10 MIL and above. Mtu huyo unakuta hata kiwanja hana. Hii tabia ipo sana hasa Dsm.

Hii kitu ni sahihi wakubwa au kujikweza na ulimbukeni tu wa maisha ya kuigana?
Wewe ndio unamawazo hasi. Unadhani gari ni starehe au la anasa tu. Hayo mawazo ya kimasikini sana. Nadhani gari huna na hutegemei kumiliki gari. Hao watu wameshajipanga kwa hilo. Umenikumbusha niliponunua tv wakati mwenye nyumba hana. Maneno yalikuwa kama hayo. Acha ujinga.
 
Back
Top Bottom