Ni pale tu Marekani inapotekeleza ahadi zake kwa vitendo ndipo uhusiano kati ya China na Marekani unaweza kuboreka

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111441980302.jpg


Kuanzia Februari hadi Juni, zaidi ya miezi minne baada ya "tukio la puto", Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken hatimaye aliwasili Beijing asubuhi ya tarehe 18 na kufanya ziara ya siku mbili nchini China. Watu wengi wanaojali uhusiano kati ya China na Marekani wanauliza kuwa, kwa nini ziara ya Blinken nchini China imekuwa ikiahirishwa tena na tena? Iliripotiwa kuwa ziara hii ya Blinken imeamuliwa na Rais wa China Xi Jinping na mwenzake wa Marekani Joe Biden walipokutana mjini Bali Novemba mwaka jana, lakini Marekani haikutekeleza ipasavyo makubaliano yaliyofikiwa tangu wakati huo.

Baada ya Marekani kutumia nguvu kuliangusha puto lisilo na rubani la China lililoingia Marekani bila ya kujizuia mwezi Februari, na kueneza uvumi kuwa hili ni puto ya kijasusi, Marekani iliendelea kuikashifu China bila ya msingi katika masuala ya Taiwan, Xinjiang, Hong Kong, na janga la COVID-19, kuharibu uhusiano kati ya China na nchi nyingine, na hata kuitaja China kama tishio dhidi ya utaratibu uliopo wa kimataifa. Katika hali kama hii, hakika China haiwezi kukubali ziara ya Blinken nchini China, mmoja wa wahusika wakuu wa timu ya wanadiplomasia ya rais Biden.

Tukikumbuka kauli iliyotolewa na afisa mmoja mwandamizi wa Marekani kwamba "zungumza na China kwa mtazamo wa nguvu na hadhi", sababu ya kuchelewesha ziara ya Blinken nchini China ni kuijulisha Marekani kwamba labda imezoea kuchukua mtazamo wa umwamba katika kuwasiliana na nchi nyingine, lakini kitendo hiki hakitafanikiwa kabisa wakati inaposhughulika na China. China daima imekuwa ikisisitiza kwamba mawasiliano kati ya nchi na nchi yanapaswa kufanywa katika msingi wa kanuni za kuheshimiana, kuishi pamoja kwa amani, na kunufaishana, iwe ni Marekani au nchi fulani iliyo nyuma kimaendeleo. Jambo hili linapaswa kutambuliwa wazi na Marekani leo.

Hali halisi ni kwamba watu wengi nchini Marekani hawaikubali sera ya sasa ya Marekani kuhusu China. Siku hizi, wanafanyabiashara wengi wakubwa wa Marekani, ikiwa ni pamoja na mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Apple Cook, mwanzilishi wa Starbucks Schultz, mkurugenzi mtendaji wa Tesla Musk, na mwenyekiti wa Taasisi ya Bill and Melinda Gates Foundation, Bill Gates walikuja China, ambapo walipinga "kutengana kwa China na Marekani" kwa vitendo, na kuonyesha matarajio ya pamoja ya kunufaika na fursa za maendeleo za China. Kama waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Marekani Henry Kissinger alivyosema katika mahojiano hivi karibuni, ‘Marekani inajali sana maslahi yake binafsi na itazidi kutengwa na dunia nzima…sera ya sasa ya Marekani kuhusu China lazima ibadilishwe.’ Ni wazi kuwa kuchukua msimamo mkali dhidi ya China kama “usahihi wa kisiasa” ndani ya Marekani hakuwezi kutatua matatizo ya Marekani, na pia ni kitendo kisichowajibika na cha hatari kwa dunia nzima.

Uhusiano kati ya China na Marekani unapaswa kuendelezwa katika mwelekeo mzuri na imara, ambayo sio tu itanufaisha watu wa nchi hizo mbili, lakini pia utakutana na matarajio ya dunia nzima. Lakini kwa sasa, bado kuna matatizo mengi yanayopaswa kutatuliwa kati ya China na Marekani: suala la Taiwan, migogoro ya kibiashara, na zuio la Marekani la kusafirisha bidhaa zenye teknolojia ya juu kwa China. Changamoto hizo haziwezi kutatuliwa katika ziara moja au mazungumzo ya mara moja. Katika siku zijazo, iwapo uhusiano kati ya China na Marekani unaweza kuimarishwa na kuboreshwa inategemea iwapo Marekani inaweza kutekeleza kama ilivyoahidiwa na Blinken, yaani kujitolea kufuata ajenda iliyowekwa na wakuu wa nchi hizo mbili katika mkutano wa Bali, kutotafuta "vita baridi vipya, kutodhamiria kubadili mfumo wa China, kutotafuta kuipinga China kwa kuimarisha uhusiano na washirika wake, kutounga mkono “Taiwan kujitenga na China” nk. Kwani baada ya yote yaliyotokea, sasa jamii ya kimataifa imekuwa na makubaliano kuwa wakati inaposhughulika na nchi kama Marekani, "sio tu wanapaswa kusikiliza maneno yake, lakini pia kuchunguza matendo yake."
 
View attachment 2662713

Kuanzia Februari hadi Juni, zaidi ya miezi minne baada ya "tukio la puto", Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken hatimaye aliwasili Beijing asubuhi ya tarehe 18 na kufanya ziara ya siku mbili nchini China. Watu wengi wanaojali uhusiano kati ya China na Marekani wanauliza kuwa, kwa nini ziara ya Blinken nchini China imekuwa ikiahirishwa tena na tena? Iliripotiwa kuwa ziara hii ya Blinken imeamuliwa na Rais wa China Xi Jinping na mwenzake wa Marekani Joe Biden walipokutana mjini Bali Novemba mwaka jana, lakini Marekani haikutekeleza ipasavyo makubaliano yaliyofikiwa tangu wakati huo.

Baada ya Marekani kutumia nguvu kuliangusha puto lisilo na rubani la China lililoingia Marekani bila ya kujizuia mwezi Februari, na kueneza uvumi kuwa hili ni puto ya kijasusi, Marekani iliendelea kuikashifu China bila ya msingi katika masuala ya Taiwan, Xinjiang, Hong Kong, na janga la COVID-19, kuharibu uhusiano kati ya China na nchi nyingine, na hata kuitaja China kama tishio dhidi ya utaratibu uliopo wa kimataifa. Katika hali kama hii, hakika China haiwezi kukubali ziara ya Blinken nchini China, mmoja wa wahusika wakuu wa timu ya wanadiplomasia ya rais Biden.

Tukikumbuka kauli iliyotolewa na afisa mmoja mwandamizi wa Marekani kwamba "zungumza na China kwa mtazamo wa nguvu na hadhi", sababu ya kuchelewesha ziara ya Blinken nchini China ni kuijulisha Marekani kwamba labda imezoea kuchukua mtazamo wa umwamba katika kuwasiliana na nchi nyingine, lakini kitendo hiki hakitafanikiwa kabisa wakati inaposhughulika na China. China daima imekuwa ikisisitiza kwamba mawasiliano kati ya nchi na nchi yanapaswa kufanywa katika msingi wa kanuni za kuheshimiana, kuishi pamoja kwa amani, na kunufaishana, iwe ni Marekani au nchi fulani iliyo nyuma kimaendeleo. Jambo hili linapaswa kutambuliwa wazi na Marekani leo.

Hali halisi ni kwamba watu wengi nchini Marekani hawaikubali sera ya sasa ya Marekani kuhusu China. Siku hizi, wanafanyabiashara wengi wakubwa wa Marekani, ikiwa ni pamoja na mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Apple Cook, mwanzilishi wa Starbucks Schultz, mkurugenzi mtendaji wa Tesla Musk, na mwenyekiti wa Taasisi ya Bill and Melinda Gates Foundation, Bill Gates walikuja China, ambapo walipinga "kutengana kwa China na Marekani" kwa vitendo, na kuonyesha matarajio ya pamoja ya kunufaika na fursa za maendeleo za China. Kama waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Marekani Henry Kissinger alivyosema katika mahojiano hivi karibuni, ‘Marekani inajali sana maslahi yake binafsi na itazidi kutengwa na dunia nzima…sera ya sasa ya Marekani kuhusu China lazima ibadilishwe.’ Ni wazi kuwa kuchukua msimamo mkali dhidi ya China kama “usahihi wa kisiasa” ndani ya Marekani hakuwezi kutatua matatizo ya Marekani, na pia ni kitendo kisichowajibika na cha hatari kwa dunia nzima.

Uhusiano kati ya China na Marekani unapaswa kuendelezwa katika mwelekeo mzuri na imara, ambayo sio tu itanufaisha watu wa nchi hizo mbili, lakini pia utakutana na matarajio ya dunia nzima. Lakini kwa sasa, bado kuna matatizo mengi yanayopaswa kutatuliwa kati ya China na Marekani: suala la Taiwan, migogoro ya kibiashara, na zuio la Marekani la kusafirisha bidhaa zenye teknolojia ya juu kwa China. Changamoto hizo haziwezi kutatuliwa katika ziara moja au mazungumzo ya mara moja. Katika siku zijazo, iwapo uhusiano kati ya China na Marekani unaweza kuimarishwa na kuboreshwa inategemea iwapo Marekani inaweza kutekeleza kama ilivyoahidiwa na Blinken, yaani kujitolea kufuata ajenda iliyowekwa na wakuu wa nchi hizo mbili katika mkutano wa Bali, kutotafuta "vita baridi vipya, kutodhamiria kubadili mfumo wa China, kutotafuta kuipinga China kwa kuimarisha uhusiano na washirika wake, kutounga mkono “Taiwan kujitenga na China” nk. Kwani baada ya yote yaliyotokea, sasa jamii ya kimataifa imekuwa na makubaliano kuwa wakati inaposhughulika na nchi kama Marekani, "sio tu wanapaswa kusikiliza maneno yake, lakini pia kuchunguza matendo yake."
Umeandika kiushabiki yaan umeandika ukiwa unaonesha kuwa unakandaiza upande mmoja , na ndo waandish tunawategemea nchini
 
Back
Top Bottom