Zanzibar in a siri nyingi!, tafuta kisa cha Sultan kumpachika ujauzoto mjakazi wa mkewe, ili kuficha siri, huyo mjakazi alikwenda kuozeshwa mahali mbali chap chap!, baadaye, mwana sulatan alizaliwa huko mjakazi alikoolewa!. Find out huyo mwana sulatan ni nani?!, tafuta uhusiano kati ya Sultanet ya Brunei na Sultanet ya Zanzibar!, find out who funds CUF and why?!.
Kwa taarifa tuu, CUF ilishinda 1995, ikashinda tena 2000!, pia ikashinda 2005!, na kushinda tena 2010 lakini kote kwa nini hawampi ushindi?!.
Visa vya Zanzibar havikuishia hapo, kuna ndugu tena wengine wawili, watoto wa baba mmoja, mama mmoja, tumbo moja!. CCM ikaamua kumzawadia urais kaka mkubwa, kisa ni kumuenzi baba yao aliyoifanyia makubwa Zanzibar, hivyo ule urais ulikuwa ni wa zawadi ya heshima ya marehemu babsa yao!. Baada ya kaka mtu kumaliza kipindi chake cha urais cha miaka 10!, mdogo mtu akachukua fomu kumrithi kaka mtu!. Chama kikamshauri, kwa vile aliyemaliza ni kaka yake wa tumbo moja, baba mmoja, mama mmoja!, hivyo kumpitisha mdogo mtu, itaonekana kama usultani!, mdogo mtu akagoma na kuibuka na madai mazito!, kuwa eti kama urais ni zawadi kwa mtoto wa yule Mzee waliomuheshimu, then "mtoto halisi aliyestahili ni yeye!".
Zanzibar haieshi vituko!, nataka niwashauri wajumbe wa bunge la katiba kuhakikisha Mwenyekiti wa kudumu anakuwa Mzanzibari, ili hoja ya serikali tatu ikishindwa, ije hoja ya serikali moja ndio itaimarisha haswa muungano na kuwakata kabisa hawa vilimimili na vitimbakwiri vya kutaka kuuvunja huu Muungano wetu adhimu, uliotokana na yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar!.
Mapinduzi Daima!.
Muunganno Milele!.
Pasco