Ni nini hasa raia wengi wa Tanzania wanakitaka katika siasa?

Ni nini hasa raia wengi wa Tanzania wanakitaka katika siasa?

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
57,240
Reaction score
90,297
Sidhani kama wengi demokrasia na mambo ya haki ni kipaumbele kwao. Inaonekana wengi wanachotaka ni maendeleo tu bila kujali yamepatikanaje au gharama yake. Lakini pia raia wengi wanapenda viongozi wanaume wahafidhina populists na nationalists.
Screenshot_20260317-193038~2.jpg

20260317_193419.jpg
 
Wanataka kiongozi
1)mzalendo alinde rasilimali za taifa sio kuuza urithi na rasilimali zao.
2)raisi wa wanyonge anayejali minority masikini ambao ndio kundi kubwa
3)anayewawajibisha mafisadi na majizi mapiga dili ambayo yanalitafuna taifa hili..kukomesha UFISADI

tiafa hili tumeliwa sana ...na huo ndio ukweli..tumeliwa sana ..ndugu zangu..tumechezewa..

nchi hii ni tajiri...

asiyeingia mikataba ya kuuza nchi

taifa litabigwa bei(ndugai)
masharti ya kijinga mikataba mibovu ni kichaa tu ndiyr atakayetakubali(JPM)

3)Wanyonge wasisumbuliwe vitambulisho vya wafanya biashara 20,000 kwa mwaka na wakawa huru mwaka mzima bila kusumbuliwa..kupungiziwa utitiri wa kodi ili wafanya biashara ndogo ndogo..KODI KODI

4*MAENDELEO*

5)**huduma bora za elimu bure,maji ,umeme na kwa gharama nafuu

6)Uhuru wa kuabudu--kufungulia makanisa,uhuru wa kisiasa..funguklia wafungwa qa kisiasa..tindu lisu n.k futa kesi za kubumba

7)Haki ya kuishi...** zuia utekaji watu wasiojulikana**

8)Uhuru wa kutoa maoni yao na KUSIKILIZWA

9)Uhuru wa kuchagua viongozi wanaowataka..

10)uwajibikaji wa wanaovunja sheria hasa mafisadi na majizi,watekaji na wauwaji,ripoti za CAG zifanyiwe kazi na watu waone wamewajibishwa majizi..kama ambavyo wanyonge qakikosea kidogo wanawajibishwa na haya majizi mafisadi papa nayo yawajibishwe

11)MAISHA BORA kwa kila ntu..nao wanyonge wafaidi keki ya taifa ..mana hawaa urefu wa kamba ..wengine wanakula kwa urefu qa kamba wao kamba yao ni fupi mno nao wale hayo mema
 
Ninekuwa na nafasi ningeajiri waalimu wa Hesabu 50,000 (Kuanzia msingi hadi kidato cha sita)
Ni ili kuhakikisha rika lijalo linakuwa na uwezo wa kufikiri vizuri tofauti na sasa......
 
Back
Top Bottom